Eti NIWE NAYE kwasababu tu ananipenda?

tindikalikali

JF-Expert Member
Jan 14, 2011
4,855
1,117
Wana jf, kuna msichana ambaye nimekuwa naye toka 2008, mazingira yalitukutanisha wakati huo nikiwa na maumivu ya kuachwa. Niliamua kuwa naye nikiamini pengine moyo wangu uliovunjika utabadilika na kupenda tena. Kadri siku zilivyokwenda ndivyo nilivyobaini kwamba simpendi., nilijivika ujasiri wa kumwambia lakini hakunielewa. Mpaka muda huu nnavyoandika haya, nimegandwa mithili ya ruba, nashindwa jinsi ya kumwacha. Jamani sipendi kuendelea kudanganya, nafsi yangu inanisuta kwa sina malengo yeyote kwake.
 
leave her nice and slow...vinginevyo utakuja juta coz moyo wako huja ridhika naendo hivyo ukiwa nae utakuta una kasirika kasirika tu bila sababu
 
Inauma sana jamani,kumpenda mtu kama anavyokupenda then kuja kuambiwa alikuwa na maana sana kipindi ukiwa na maumivu ya kuachwa na sasa humpendi....mueleweshe tu na zaidi sitisha vitu ambavyo mlikuwa mnafanya pamoja kama kissing,sex,outings na mengineyo,ataelewa tu with time....nakusihi usimuumize zaidi kwa maneno ya kashfa au hata kumuonyesha mwanamke mwingine....mheshimu tu na muelewe kuwa anapita kugumu nae kwenye maisha yake.......!!!
 
Inauma sana jamani,kumpenda mtu kama anavyokupenda then kuja kuambiwa alikuwa na maana sana kipindi ukiwa na maumivu ya kuachwa na sasa humpendi....mueleweshe tu na zaidi sitisha vitu ambavyo mlikuwa mnafanya pamoja kama kissing,sex,outings na mengineyo,ataelewa tu with time....nakusihi usimuumize zaidi kwa maneno ya kashfa au hata kumuonyesha mwanamke mwingine....mheshimu tu na muelewe kuwa anapita kugumu nae kwenye maisha yake.......!!!

nashukuru kwa ushauri wako, huwa najitahidi kutowasiliana naye, lakini haishi kunitafuta, muda mwingine anakuja nyumban bila taharifa, na kibaya zaidi sina mtu mwingine.
 
leave her nice and slow...vinginevyo utakuja juta coz moyo wako huja ridhika naendo hivyo ukiwa nae utakuta una kasirika kasirika tu bila sababu

Kumuacha mtu "nice and slow" ndio kupi huko? Halafu maumivu yake ya kichwa yatapungua?
 
Kumuacha mtu "nice and slow" ndio kupi huko? Halafu maumivu yake ya kichwa yatapungua?

ndo kama alivyo muelekeza mwenzako hapo chin kua aache baadhi ya vitu walivyo kua wana fanya pamoja ila pole pooooooooole sio ghafla tu coz ina uma balaaaaaa
 
hahahahaha lol
Vijana wasaiv tunambwembwe sana,
Sijui tunataka nini katika mapenzi, au tunatamani mapenzi yatupe nini zaidi.
Kwa case ulivyotuambia, ushauri wa busara unaweza kuwa umwache tu mtoto wa watu.
Lakini kuna ukweli kwamba ni bora sana kupendwa kuliko kupenda.....
Maamuzi katika maisha yetu tunaamua kwa akili zetu na tunajenga wenyewe,
Mapenzi yanakuwa mabaya na kuona mapungufu ya mwenzio unapoanza kulinganisha,
Ila tena ukweli mmoja ni kuwa mara zote si rahisi sana kupata mtu wa kukuambia
"nakupenda" na akaweza kuisimamia kauli yake kwa vitendo........
Mwache binti wa watu, ila utakuja mda utahitaji upendwe japo kidogo tu
 
hahahahaha lol
Vijana wasaiv tunambwembwe sana,
Sijui tunataka nini katika mapenzi, au tunatamani mapenzi yatupe nini zaidi.
Kwa case ulivyotuambia, ushauri wa busara unaweza kuwa umwache tu mtoto wa watu.
Lakini kuna ukweli kwamba ni bora sana kupendwa kuliko kupenda.....
Maamuzi katika maisha yetu tunaamua kwa akili zetu na tunajenga wenyewe,
Mapenzi yanakuwa mabaya na kuona mapungufu ya mwenzio unapoanza kulinganisha,
Ila tena ukweli mmoja ni kuwa mara zote si rahisi sana kupata mtu wa kukuambia
"nakupenda" na akaweza kuisimamia kauli yake kwa vitendo........
Mwache binti wa watu, ila utakuja mda utahiraji upendwe japo kidogo tu

Kama kwake ni bora kupendwa kuliko kupenda na mwenzake pia anastahili hivyo hivyo!!Acheni ubinafsi....kama humpendi mtu mwache akapendwe huko mbele kwa mbele!
 
Kama kwake ni bora kupendwa kuliko kupenda na mwenzake pia anastahili hivyo hivyo!!Acheni ubinafsi....kama humpendi mtu mwache akapendwe huko mbele kwa mbele!

Ila Lizzy, mbona nimeainisha vitu vingi tu hapo.
Pia nilijua mpo watu kama nyie ndio maana pia nikasema "amwache mtoto wa watu"
Ila mtu utaacha watu wangapi? ili ufikie hicho unachokitaka? Je, hiyo kitu ni realistic?
 
Kama kwake ni bora kupendwa kuliko kupenda na mwenzake pia anastahili hivyo hivyo!!Acheni ubinafsi....kama humpendi mtu mwache akapendwe huko mbele kwa mbele!

ni kweli unachokisema, nimechoka tena sina hisia hata kidogo kwake.
 
hahahahaha lol
Vijana wasaiv tunambwembwe sana,
Sijui tunataka nini katika mapenzi, au tunatamani mapenzi yatupe nini zaidi.
Kwa case ulivyotuambia, ushauri wa busara unaweza kuwa umwache tu mtoto wa watu.
Lakini kuna ukweli kwamba ni bora sana kupendwa kuliko kupenda.....
Maamuzi katika maisha yetu tunaamua kwa akili zetu na tunajenga wenyewe,
Mapenzi yanakuwa mabaya na kuona mapungufu ya mwenzio unapoanza kulinganisha,
Ila tena ukweli mmoja ni kuwa mara zote si rahisi sana kupata mtu wa kukuambia
"nakupenda" na akaweza kuisimamia kauli yake kwa vitendo........
Mwache binti wa watu, ila utakuja mda utahitaji upendwe japo kidogo tu

ni kweli unachokisema, lakini kuwa na mtu eti kwasababu tu anaweza kusema "nakupenda" na akasimamia anachokisema, sidhan kama ni sahihi.
 
Pole kaka. Nachokushauri kama huna mapenzi nae kuwa makini. Kuna wadada wakipenda mtu na ameshajua (maana umesema umemwambia) huna mapenzi nae, anaweza kutumia ujanja wa kijinga kukukamata. Kama bado una do nae usishangae anakwambia ana ujauzito wako. Epuka kuleta watoto wa nje ya ndoa duniani. Ninaona kila dalili ya huyo dada kujishikisha mimba.

Kuna mdada amezaa na shemeji yangu shem hamfeel kabisa ingawa wakati wanazaa mapenzi yalikuwepo. Basi huyu mdada ananambiaga yaani shem wako akikosea tu kukubali ku do na mimi basi nazaa mtoto wa pili kwani nampenda sana na sitaki kuzaa na wanaume tofauti.
 
Vipi unauonaje msimamo wake kuhusu swala zima la TiGo?Kama hapendi,hii inaweza kuwa njia rahisi ambayo yeye mwenyewe anaweza kukuacha.Nadhani umenielewa kiutu uzima au vipi!!
 
Inaonyesha wewe ni staki nataka.hebu maanisha,na umwambie kwa msisitizo usimpotezee muda bint.
 
Pole kaka. Nachokushauri kama huna mapenzi nae kuwa makini. Kuna wadada wakipenda mtu na ameshajua (maana umesema umemwambia) huna mapenzi nae, anaweza kutumia ujanja wa kijinga kukukamata. Kama bado una do nae usishangae anakwambia ana ujauzito wako. Epuka kuleta watoto wa nje ya ndoa duniani. Ninaona kila dalili ya huyo dada kujishikisha mimba.

Kuna mdada amezaa na shemeji yangu shem hamfeel kabisa ingawa wakati wanazaa mapenzi yalikuwepo. Basi huyu mdada ananambiaga yaani shem wako akikosea tu kukubali ku do na mimi basi nazaa mtoto wa pili kwani nampenda sana na sitaki kuzaa na wanaume tofauti.

nyumba kubwa
Hivi unazaaje na mtu usiye mfeel?In my silly mind nilikuwa najua watu wanasahaugi zana/rubber, in those cases where the passion can not withstand any logical reasoning! ??? But, hey who knows maybe ur shem yeye ni mtu wa...........................

tindikalikali
Its a tough pill to swallow that a man you have loved and believed to have been feeling the same way for about 2 years, or so Hakupendi tena. Especially in a situation like yours where there is not even another woman, in the horizon replacing her, that she can blame and/or vent off on. Id say do as Michelle has suggested above, "sitisha vitu ambavyo mlikuwa mnafanya pamoja kama kissing,sex,outings .........."
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom