Eti ni ndugu yangu khaa

Eti ni ndugu yangu khaa

Latifaa

JF-Expert Member
Joined
Jan 18, 2012
Posts
501
Reaction score
258
Heshima zenu wana jamvi,

Kuna ndugu yangu katoka mamtoni huko Marekani tulikua tunawasiliana vizuri sana kwa email lakini ghafla mawasiliano yakawayameisha kumbe kasharudi bongo miezi minne iliopita yuko hapa dar, alikaa nje kwa miaka 6 hivi yaani na mimi nilikua na hamu yakumuona kishenzi yaani mara sikuhiyo nampigia simu ndugu yangu flani wambali kidogo yuko mkoa nastaajabu ananiambia Leyla kaja umeshaonana nae? khaa nikamwambia siyupo Amerika kwani karudi? akajibu kasharudi tena anasema umemchunia nikastaajabu nitamchuniaje mtu yuko mamtoni mimi niko bongo? basi nikamwambia embu nipe namba yake ya hapa akanipa nikampandia hewani kwani kapokea nimempigia zaidi ya mara kumi hapokei simu nikaamua kutemana nae mara sikuyasiku miezi kama mitatu mbele naona namba yake ananipigia sikujishughulisha kupokea nikaachana nae hadi leoo hiii niko zangu kimya kuna tatizo wapendwa? au mnaniambiaje?
 
mchunie ivoivo mpaka muwe maadui wa kudumu...
 
Acheni utoto.

Akipiga pokea, akiuchuna uchune. Siku na wewe ukijisikia kumkumbuka mpigie, akipokea sawa, asipopokea unapotezea. Hivyo hivyo maisha yanaenda.
 
hapa mie napita tu kwani ndg wakigombana wewe chukua jembe ukalime
 
Heshima zenu wana jamvi,

Kuna ndugu yangu katoka mamtoni huko Marekani tulikua tunawasiliana vizuri sana kwa email lakini ghafla mawasiliano yakawayameisha kumbe kasharudi bongo miezi minne iliopita yuko hapa dar, alikaa nje kwa miaka 6 hivi yaani na mimi nilikua na hamu yakumuona kishenzi yaani mara sikuhiyo nampigia simu ndugu yangu flani wambali kidogo yuko mkoa nastaajabu ananiambia Leyla kaja umeshaonana nae? khaa nikamwambia siyupo Amerika kwani karudi? akajibu kasharudi tena anasema umemchunia nikastaajabu nitamchuniaje mtu yuko mamtoni mimi niko bongo? basi nikamwambia embu nipe namba yake ya hapa akanipa nikampandia hewani kwani kapokea nimempigia zaidi ya mara kumi hapokei simu nikaamua kutemana nae mara sikuyasiku miezi kama mitatu mbele naona namba yake ananipigia sikujishughulisha kupokea nikaachana nae hadi leoo hiii niko zangu kimya kuna tatizo wapendwa? au mnaniambiaje?

Hakuna tatizo, tatizo umeleta mada JF ambapo kila kitu kinaweza kuwa tatizo.

Lakini pia ukiona kimya salama, akikupigia pokea.

Unaweza kuchunia simu kesho ukaambiwa mtu kafariki, na sababu inahusiana na wewe kutopokea simu.

Noma.
 
Latifa...kuwa...fikiria..tafakari ndo uamue moyo wako unataka nini.? Usisikie ya wapita njia.
 
kushobokea wa ng'ambo kutakuponza.......

Labda alihofia usije kumuomba iphone buuuuure....

Ila mbona mambo madogo mjali anayekujali asiyekujali tupa kule
 
Teh aisee naona hii imekaa kike sana(mambo ya kuchuniana, kununiana etc)..Ngoja wenzako wakujibu.....
 
We nae miaka sita ni mingi mambo yanabadilika,kwa kadri miaka inavyoenda kuna baadhi ya watu wanakua wa muhimu sana na wenginwe hawana umuhimu tena japo mtaendelea kusalimiana kama mara chache lkn haimaanishi mmechuniana ,mi naona jambo la kawaida sana,kwnza wakati unampigia una uhakika gani alikua amesave number yako mana na wewe umesema "nikaomba namba yake" dat means ni curent number yake kwa hapa TZ,kwahyo ukute hata haukua kwenye phonebook yake my dia acha kujump into conlusion hizo issue ndg sana sasa vitu kama hivo vikikupa stress ukikutana na issue kubwa kubwa si utazirai wewe!!
 
Mleta mada uko sahihi,tena huyo ndugu yako atakuwa ameishiwa madolali sasa anatafuta ukaribu tena.Anyway uamzi ni wako
 
Kwa nini usipokee tu hiyo simu yake...wakati mwingine ugumu wa mambo twautaka wenyewe!!
Halafu kuna uwezekano uliagiza lundo la mizawadi, sasa mwenzako kakosa wapi atainy'ea kaamua kuingia nchini kimya kimya ili kuepuka kiranga kisimpate...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom