Selous
JF-Expert Member
- Jan 13, 2008
- 1,325
- 144
Alisema anayekaimu nafasi hiyo kwa sasa ni Naibu Katibu Mkuu wa Umoja huo, Amina Makillagi.
Ok, labda mwandishi alikosea lakini huyu nae hana nidhamu.
Kwa mujibu wa Makame, UWT inasikitishwa na uvumi ambao umesambaa kuwa Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Sophia Simba, wana mkono katika kufukuzwa kwa Mwilima.
Alisema kwa mujibu wa Katiba, Mwenyekiti wa chama ambaye ni Rais Kikwete, anajulishwa wakati wa uteuzi wa jina la Katibu Mkuu, lakini wakati wa kufukuzwa kazi si lazima apewe taarifa.
Kikatiba Mwenyekiti wa UWT, Sophia Simba, ndiye anapendekeza jina la Katibu Mkuu na kumpelekea Mwenyekiti wa chama (Kikwete), na baada ya hapo Mwenyekiti analipeleka Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), kisha linarudishwa katika Baraza Kuu kwa ajili ya kupigiwa kura ya kulipitisha, sasa hao wanaolipitisha jina ndio hao hao wenye uwezo wa kumfukuza kazi, Sophia Simba, Rais Kikwete hawajui lolote kuhusu kufukuzwa kwa Mwilima, alisema
Ok, labda mwandishi alikosea lakini huyu nae hana nidhamu.