ERTUGRUL BEY
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 11,593
- 21,636
Kukufuru Kwa lugha isiyo rasmi ni Hali ya kumlaumu Mola wetu Kwa kutotutimizia au kutufanyia jambo letu Fulani.
Na
Kushukuru ni kufurahia au kuikubali neema mbali mbali ambazo ametujalia au ametupa Mola wetu.
Kwa bahati mbaya Sana watu wengi Tunapenda kumkufuru Mungu na Kusahau neema mbali mbali ambazo ametujalia kama wanadamu,huwa tuna angalia vitu vinavyopendwa na nafsi zetu kama magari,majumba na anasa nyingine mbali mbali,tukivikosa hivyo basi hapo kufuru inaanza,kwanini Mimi Mungu hajanipa nyumba? Au hajanipa kazi nzuri? Na mambo kama hayo.
Lakini
Tunasahau neema ya afya,Uhai,macho,masikio na viungo vilio kamilika,je ni wangapi ni vipofu,viziwi na walemavu?
Hakika Allah hawapendi watu ambao wanakufuru neema mbali mbali walizopewa,na hayo ni makosa makubwa Sana.
Tunatakiwa kushukuru Kwa kila Jambo ambalo tumepewa na Allah,huna gari lakini Una afya njema,Una uwakika wa Kula Milo mitatu Kwa siku hakika hiyo ni neema,kwasababu kuna watu Kula Yao ni shida Sana.
Kwa kila ulichonacho kiwe Kikubwa au kidogo basi mshukuru Mola wako hakika yeye huwapend Sana watu wanaoshukuru,na wanao shukuru huongezewa kila siku.
Hapa namkumbuka Malcom ambaye sasa ni marehemu ambaye allikuwa mtoto wa Masudi Kipanya hakika Allah amrehemu, pamoja na kuwa mlemavu na WA kitandani Mda wote lakini alikuwa mtu WA kushukuru na siku zote alitufundisha namna ya kumshukuru Mungu Kwa kila Jambo,binafsi nilikuwa namkubali Sana Katu hakutetereka katika Imani yake Kwa Mola wake.
Hivyo ndivyo tunavyotakiwa tuishi na kushukuru Kwa kila Jambo. Mwenyezi Mungu anasema:
Mkinikumbuka Nitawakumbuka, Mnishukuru na wala Msinikufuru
Ni hayo Tu!
Kazakh destroyer
baby zu
Mademoiselle
Na
Kushukuru ni kufurahia au kuikubali neema mbali mbali ambazo ametujalia au ametupa Mola wetu.
Kwa bahati mbaya Sana watu wengi Tunapenda kumkufuru Mungu na Kusahau neema mbali mbali ambazo ametujalia kama wanadamu,huwa tuna angalia vitu vinavyopendwa na nafsi zetu kama magari,majumba na anasa nyingine mbali mbali,tukivikosa hivyo basi hapo kufuru inaanza,kwanini Mimi Mungu hajanipa nyumba? Au hajanipa kazi nzuri? Na mambo kama hayo.
Lakini
Tunasahau neema ya afya,Uhai,macho,masikio na viungo vilio kamilika,je ni wangapi ni vipofu,viziwi na walemavu?
Hakika Allah hawapendi watu ambao wanakufuru neema mbali mbali walizopewa,na hayo ni makosa makubwa Sana.
Tunatakiwa kushukuru Kwa kila Jambo ambalo tumepewa na Allah,huna gari lakini Una afya njema,Una uwakika wa Kula Milo mitatu Kwa siku hakika hiyo ni neema,kwasababu kuna watu Kula Yao ni shida Sana.
Kwa kila ulichonacho kiwe Kikubwa au kidogo basi mshukuru Mola wako hakika yeye huwapend Sana watu wanaoshukuru,na wanao shukuru huongezewa kila siku.
Hapa namkumbuka Malcom ambaye sasa ni marehemu ambaye allikuwa mtoto wa Masudi Kipanya hakika Allah amrehemu, pamoja na kuwa mlemavu na WA kitandani Mda wote lakini alikuwa mtu WA kushukuru na siku zote alitufundisha namna ya kumshukuru Mungu Kwa kila Jambo,binafsi nilikuwa namkubali Sana Katu hakutetereka katika Imani yake Kwa Mola wake.
Hivyo ndivyo tunavyotakiwa tuishi na kushukuru Kwa kila Jambo. Mwenyezi Mungu anasema:
Mkinikumbuka Nitawakumbuka, Mnishukuru na wala Msinikufuru
Ni hayo Tu!
Kazakh destroyer
baby zu
Mademoiselle