Eti 2023 tunaendelea Kukufuru au Kushukuru?

Eti 2023 tunaendelea Kukufuru au Kushukuru?

ERTUGRUL BEY

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
11,593
Reaction score
21,636
Kukufuru Kwa lugha isiyo rasmi ni Hali ya kumlaumu Mola wetu Kwa kutotutimizia au kutufanyia jambo letu Fulani.

Na

Kushukuru ni kufurahia au kuikubali neema mbali mbali ambazo ametujalia au ametupa Mola wetu.

Kwa bahati mbaya Sana watu wengi Tunapenda kumkufuru Mungu na Kusahau neema mbali mbali ambazo ametujalia kama wanadamu,huwa tuna angalia vitu vinavyopendwa na nafsi zetu kama magari,majumba na anasa nyingine mbali mbali,tukivikosa hivyo basi hapo kufuru inaanza,kwanini Mimi Mungu hajanipa nyumba? Au hajanipa kazi nzuri? Na mambo kama hayo.

Lakini

Tunasahau neema ya afya,Uhai,macho,masikio na viungo vilio kamilika,je ni wangapi ni vipofu,viziwi na walemavu?

Hakika Allah hawapendi watu ambao wanakufuru neema mbali mbali walizopewa,na hayo ni makosa makubwa Sana.

Tunatakiwa kushukuru Kwa kila Jambo ambalo tumepewa na Allah,huna gari lakini Una afya njema,Una uwakika wa Kula Milo mitatu Kwa siku hakika hiyo ni neema,kwasababu kuna watu Kula Yao ni shida Sana.

Kwa kila ulichonacho kiwe Kikubwa au kidogo basi mshukuru Mola wako hakika yeye huwapend Sana watu wanaoshukuru,na wanao shukuru huongezewa kila siku.

Hapa namkumbuka Malcom ambaye sasa ni marehemu ambaye allikuwa mtoto wa Masudi Kipanya hakika Allah amrehemu, pamoja na kuwa mlemavu na WA kitandani Mda wote lakini alikuwa mtu WA kushukuru na siku zote alitufundisha namna ya kumshukuru Mungu Kwa kila Jambo,binafsi nilikuwa namkubali Sana Katu hakutetereka katika Imani yake Kwa Mola wake.

Hivyo ndivyo tunavyotakiwa tuishi na kushukuru Kwa kila Jambo. Mwenyezi Mungu anasema:

Mkinikumbuka Nitawakumbuka, Mnishukuru na wala Msinikufuru

Ni hayo Tu!


Kazakh destroyer
baby zu
Mademoiselle
 
Lakini sio rahisi sana kukumbuka fadhila za Mungu pale linapotokea jambo baya katika maisha. Ukitaka kutuona wanadamu tulivyo angalia tunavyoishi pamoja. Wengi wetu utakuta mwenza ana mazuri mengi ameshayafanyaga. Lakin siku akifanya baya moja na kweli likawa baya sio rahisi kukumbuka zuri lolote alowahi kulifanya. Tena utamshutumu na kumsema kwa kashfa kana kwamba hajawahi kuwa mtu mzuri hapo nyuma.

Najaribu kusema, kushukuru sio tendency ya kibinadamu. Hata mwanadamu umpe dunia..kushukuru si fungu lake. Hawa kaumbwa, wakapewa wale tunda la kila.mti lakin yeye kaona haitoshi na nililokatazwa acha nalo nile.

Unapewa 5000, lakin unaitaka na hiyo 5 Mungu alokukataza tena kwa order maalum. We are generally never thankful inshort.
 
03:40

Njoo vile popo hawalali usiku..
 
Mwanadamu asili yake kama akikosa nuru ya elimu na muongozo ni dhaalimu tena mjinga mno, mlalamishi na aliyekosa shukrani tena akipata kuona amejitosheleza hata kwa masaa tu basi utamuona anavuka mpaka.

Hizi ndizo tabia mbaya za mwanaadamu tunapaswa kujiepusha nazo kwa muda wote wa maisha yetu.
 
Mwanadamu asili yake kama akikosa nuru ya elimu na muongozo ni dhaalimu tena mjinga mno, mlalamishi na aliyekosa shukrani tena akipata kuona amejitosheleza hata kwa masaa tu basi utamuona anavuka mpaka.

Hizi ndizo tabia mbaya za mwanaadamu tunapaswa kujiepusha nazo kwa muda wote wa maisha yetu.
watu awawezi kuwacha tabia hizi kwa sababu wengi wao hawana utambuzi wa neema za mungu mvua ikizidi ua jua analaumiwa binadamu
 
Lakini sio rahisi sana kukumbuka fadhila za Mungu pale linapotokea jambo baya katika maisha. Ukitaka kutuona wanadamu tulivyo angalia tunavyoishi pamoja. Wengi wetu utakuta mwenza ana mazuri mengi ameshayafanyaga. Lakin siku akifanya baya moja na kweli likawa baya sio rahisi kukumbuka zuri lolote alowahi kulifanya. Tena utamshutumu na kumsema kwa kashfa kana kwamba hajawahi kuwa mtu mzuri hapo nyuma.

Najaribu kusema, kushukuru sio tendency ya kibinadamu. Hata mwanadamu umpe dunia..kushukuru si fungu lake. Hawa kaumbwa, wakapewa wale tunda la kila.mti lakin yeye kaona haitoshi na nililokatazwa acha nalo nile.

Unapewa 5000, lakin unaitaka na hiyo 5 Mungu alokukataza tena kwa order maalum. We are generally never thankful inshort.
Kweli kabisa usemayo madam Mademoiselle kitu shukrani Kwa Binadamu wengi ni mtihani Sana kitu ambacho Tunatakiwa kupambana Sana ili tukiingize katika Maisha yetu ya kawaida.

Kama ulivyosema ubaya WA siku moja basi unaharibu mazuri yote ya miaka nenda Rudi,Lau kuwa tungekuwa tunakumbuka mazuri tunayo fanyiwa kama tunavyokumbuka ubaya hakika tusingekuwa na mifarakano ya mara Kwa mara.

Mwenye kushukuru siku zote huwa na Amani na furaha,kwasababu anashukuru Kwa kila Jambo ambalo anakutana nalo maishani mwake.

Ndio maana kuna watu wengine hawana neema kubwa Sana lakini ni watu wenye furaha na tabasamu Mda wote kwakuwa wanashukuru Kwa kila jambo
 
Mwanadamu asili yake kama akikosa nuru ya elimu na muongozo ni dhaalimu tena mjinga mno, mlalamishi na aliyekosa shukrani tena akipata kuona amejitosheleza hata kwa masaa tu basi utamuona anavuka mpaka.

Hizi ndizo tabia mbaya za mwanaadamu tunapaswa kujiepusha nazo kwa muda wote wa maisha yetu.
Kweli kabisa mkuu

Na akipata vile vile hujiona kapata Kwa ujanja wake na kuwaona wengine wote wazembe,na hakawikii Kusahau neema za Mola wake kuwa ndio kamuwezesha kupata hayo aliyo yapata.

Hakika binadamu ni mwingi WA kukosa fadhila kabisa
 
watu awawezi kuwacha tabia hizi kwa sababu wengi wao hawana utambuzi wa neema za mungu mvua ikizidi ua jua analaumiwa binadamu
Kweli kabisa mkuu na haya yote yanatokana na kukosa elimu ya kumjua Mola wake, Lau kuwa angemjua Mola wake na hekima zake na uwezo basi siku zote angekuwa mtu WA kushukuru na sio Kukufuru.
 
Na ktk dua nzuri ya kuiomba ni Ewe mola wangu nijalie mimi ni kudhukuru, nikushuru na uniwezeshe kutekeleza ibada zako.
Ni dua ya kawaida kwa kuisoma lakina naona maisha yotr yako kwenye hii dua
 
Mwanadamu asili yake kama akikosa nuru ya elimu na muongozo ni dhaalimu tena mjinga mno, mlalamishi na aliyekosa shukrani tena akipata kuona amejitosheleza hata kwa masaa tu basi utamuona anavuka mpaka.

Hizi ndizo tabia mbaya za mwanaadamu tunapaswa kujiepusha nazo kwa muda wote wa maisha yetu.
Amina
 
Na ktk dua nzuri ya kuiomba ni Ewe mola wangu nijalie mimi ni kudhukuru, nikushuru na uniwezeshe kutekeleza ibada zako.
Ni dua ya kawaida kwa kuisoma lakina naona maisha yotr yako kwenye hii dua
Naam swadakta ukhty umesema vyema kabisa
 
Kweli kabisa mkuu

Na akipata vile vile hujiona kapata Kwa ujanja wake na kuwaona wengine wote wazembe,na hakawikii Kusahau neema za Mola wake kuwa ndio kamuwezesha kupata hayo aliyo yapata.

Hakika binadamu ni mwingi WA kukosa fadhila kabisa
Kuna jamaa huku alianzisha mada eti anawashangaa sana watu wanaoishi nyumba za kupanga mpaka leo.
 
Back
Top Bottom