Hivi ni kigezo gani hutumika kumuita mtu dikteta?Mi wananikera sana!
Mkuu,
Kwenye udikteta;
1. Kiongozi wa nchi yeye ndie mtu pekee wa kuongoza na hakutakuwa na wa kumpinga. Yaani hakuna upinzani na hata kama upo atatumia sababu na asasi zake mbalimbali kubinya ukuaji wa upinzani huo.
Mfano wa kiongozi kama huyo ni Robert Mugabe, Meles Zenawi na wengine wengi tu. Hawa wamepata madaraka kwa mtutu wa bunduki kwahio hawaoni sababu ya kuwaondoa kwenye madaraka waliyoyapigania.
2. Kwenye udikteta kiongozi au dikteta hazingatii katiba ya nchi katika kutawala watu wake- yaani katiba iliyopo inatosha na haina haa ya kuibadili, yupo juu ya sheria na hatambui kisheria uwepo wa upinzani juu yake, kwamba kuna wananchi ambao wana mawazo tofauti.
3. Kwenye udikteta uamuzi wa kiongozi ni wa mwisho (absolute power) na haupingwi na kila wakati huenda kwenye vyombo vya habari kuwakumbusha wananchi uwepo wake na kwamba wasisahu jambo hilo. Pia taarifa mbalimbali za propaganda hutayarishwa na kurushwa kupitia vyombo hivyo ambavyo vingi humilikiwa na serikali yake.
Taarifa na propaganda hizi hubeza, hukejeli, huponda, huzodoa na wakati mwingine kukashifu upinzani na kusema kwamba hakuna mwenye sifa za kuongoza jamii isipokuwa kiongozi huyo mtukufu.
4. Kwenye udikteta hakuna bunge, uchaguzi, na mara kwa mara huwepo amri ya kutotembeo hovyo hovyo mabarabarani, kutangazwa hali ya hatari muda wowote ule na madudu mengine mengi tu.
Sasa zipo aina mbalimbali za udikteta, mifano ni udikteta wa kikatiba, udikteta wa kijeshi, udikteta wa kijamaa (kama ilivyokuwa Yugoslavia na baadae hayati mwalimu Nyerere akaiga na kuleta vijiji vya ujamaa), udikteta wa kujiita mzalendo yaani kama ule unaotumiwa na Robert Mugabe kule Zimbabwe.
Mugabe anasema Afrika ni ya wafrika na ardhi ni yao na wana haki asilimia 90 ya umiliki na mgeni hana chake isipokuwa kama akiomba na kupewa kibali.
Udikteta wa kikatiba na kijeshi siku hizi unachanganywa na mifano ni Rwanda na Uganda ambapo maraisi Kagame na Museveni wanatumia mbinu hiyo kuongoza nchi hizo kwamba kukiwa na dharura wao wanatawala kijeshi ingawa katiba haiwapi nguvu zaidi lakini wakiwa wanajeshi wanatoa amri mbalimbali za kutawala kijeshi.
Kwahio mtu ataitwa dikteta kama atafanya mambo hayo na kwamba hatoweza kuruhusu mtu mwingine achukue madraka mpaka mauti yatakapomkuta au ugonjwa wa kupooza au kuondolewa kwa nguvu.
Basi mkuu nimejitahidi kueleza kwa kifupi lakini hili eneo ni pana na lina umuhimu kulifuatilia kwani limejaa elimu nzuri sana.