GE2025 Esther Bulaya aomba Kura huku akinyeshewa na Mvua

GE2025 Esther Bulaya aomba Kura huku akinyeshewa na Mvua

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Zikiwa zimesalia siku chache kabla ya uchaguzi mkuu wa rais, wabunge na madiwani kufanyika nchini Tanzania, mgombea ubunge wa Bunda Mjini mkoani Mara kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Esther Bulaya ameendelea na kampeni zake licha ya mvua kunyesha.

Bulaya akiwa kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika jana Jumatano, Oktoba 22, 2025 katika Mtaa Mabanzuni, Kata ya Balili, alinadi sera za chama hicho kwa wananchi wa jimbo hilo huku akiwahakikishia kuwa, endapo watampa ridhaa ya kuwa mbunge wao, atashirikiana na Serikali kuhakikisha ujenzi wa ofisi za Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (Tanapa) Kanda ya Magharibi unafanyika hususan katika Kata ya Balili.

Soma: Bulaya, Esther Mathiko washindwa kung'ara kura za maoni

Amesema uwepo wa ofisi hizo utasaidia kudhibiti uharibifu unaosababishwa na tembo ambao wamekuwa changamoto kubwa kwa wakulima wa eneo hilo.

 
Hao vijana si ajabu wamelipwa buku10 ten na wakavumilia adhaa yote ile ya baridi na mvua.
Vijana wanamna hii wanamchango mdogo sana kwenye hii nchi
 
Safi ,wamatumbi hata hakuna haja ya kutumia akili kuwashika
 
Hata sisi kwenye utafutaji mvua sio ishu ... Huyonae ni ktafutaji tu hayupo kwa ajiri ya wananchi
 
Askari wake mmoja anaukosefu wa culcium kwenye ngoko na kavaa la luumpaa lamaa

Njaa tupu, halafu unakua je mwanamke na kipara halafu unasuka Rasta.! 😎
 
Back
Top Bottom