Katika hali isiyo ya kawaida kikao cha madiwani kimevunjika huku baadhi ya madiwani wakitaka kushikana mashati wakipingana kile wanachokiona kuwa ni utaratibu mbovu wa uchaguzi baada ya kutaka kupitisha jina la mwenyekiti wa halmshauri ambaye siyo chaguo la madiwani bali ni maelekezo ya mbowe na timu yake.
Madiwani wasusa kikao na kutoka nje na kurushina maneno makali mbele ya majengo ya ofisi za halmashauri ya wilaya ya Tarime walikopewa hifadhi ya ukumbi wa kufanyia kikao chao wamegawanyika makundi mbalimbali kwenye eneo la halmashauri huku mbunge Ester Matiko na wapambe wake wakijibanza pembeni ya ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Tarime huku akionekana na hasira za kutosha kwa madiwani wake.
Madiwani wasusa kikao na kutoka nje na kurushina maneno makali mbele ya majengo ya ofisi za halmashauri ya wilaya ya Tarime walikopewa hifadhi ya ukumbi wa kufanyia kikao chao wamegawanyika makundi mbalimbali kwenye eneo la halmashauri huku mbunge Ester Matiko na wapambe wake wakijibanza pembeni ya ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Tarime huku akionekana na hasira za kutosha kwa madiwani wake.