ESCROW scandal: Pinda apata watetezi

tpaul

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
27,181
Reaction score
27,781
Kuna taarifa kwamba Pinder amewapanga wabunge kadhaa (majina kapuni) wamtetee bungeni leo ili asiende na maji. Kwa kufanikisha utetezi wao wanadai kwamba Pinder hajahusika yeye binafsi katika ufisadi huu bali ni watendaji wa chini yake ndio wanapaswa kuchukuliwa hatua.

Kete ya pili wanayotumia 'watetezi' hawa ni kwamba ikiwa Pinder alihusika kwenye ufisadi huu basi asingeagiza uchunguzi ufanyike. So the guy is clean and innocent.

Aidha, kuna timu kubwa imetumwa kumtetea Pinder kwenye social media, hasa JF, kwa lengo la kuupotosha umma na kuwafanya wananchi wasadiki kwamba Pinder anaonewa bure.

Kisingizio kingine kitakachotumiwa kumsafisha ni uwepo wa makundi ya urais, 2015 yanayochafuana.

Anyway, ngoja tusubiri tuone hao vibaraka wake wamejipangaje kumtetea kwa kuwa naona kama wanatumia hoja mfu kumsafisha mtu ambaye amechafuka kiasi cha kutosafishika tena. Mbivu na mbichi tutazipata leo bungeni wakati utetezi wa serikali (utakaotolewa na Pinder mwenyewe) utakaporindima.

Nawasilisha
:israel:
 
Serikali(Pinda) ilisema fedha za Escrow sii za umma sasa CAG, Takukuru, PAC wanasema hizi ni fedha za umma sijui atajitetea kwa lipi kama Serikali.
Pinda hana uwezo wa kuwa Rais na yeyote ndani ya CCM hamna mwenye uwezo wa kuwa Rais otherwise ni shida tu watatuletea
 

Pia,kuna kundi lingine limeteuliwa kuendelea kumchafua humu JF na kwingineko.
"" #wewe_ni_miongoni ""
 

Nadhani turudie kuisoma hiyo ripoti mbona imebandikwa humu JF! Pinda anaenda na maji sio kwamba kaiba. Ila alibariki wizi na hakuwa makini katika kutekeleza wajibu wake. Pia alijikuta ameingia kwenye mkumbo wa ku-emphasize kuwa hela ile si ya umma. Kwa hayo tu inatosha hata kuwambia wengine wabaki ila yeye aende. Lakini kwa kuwa tunaamini waliyoyafanya hayawapi hadhi ya kubakia katika nafasi zao, basi waende nae!
 
Hata ile kauli yake ya wapigwe tu, maana wametuchosha!! Hiyo nayo inatosha kuachia ngazi.
 
ukweli ni kwamba pinda amepoteza uhalali na sifa ya kugombea urais TZ. aende akafuge nyuki tu. hauziki hata wafanyeje.
 
kitendo cha kubisha hazikuwa fedha za umma peke yake kinatosha kumuengua achilia mbali mengine ya kiutendaji
 
Wahisani wanajua namna system nzima ilivyopingwa ganzi na kupelekea wizi huu wa kihistoria.....Wahisani wanataka hatua stahiki zichukuliwe si mzaha......Hatuwezi kukwepa ukweli wa viongozi wetu kushindwa kulifanya taifa hili kujitegemea ........hivyo lazima tukidhi matakwa haya yenye nia njema kukomesha wizi uliokomaa ...........naamini wabunge wengi wa CCM na upinzani wataungana na kamati ya akina Zitto kupitisha maazimio yao........PINDA lazima AONDOKE .........
 
PAC hawakuonyesha kwanini wanasema pesa ni za umma. Waache upande mwingine ujitetee.
PAC wame-rely kwa mkurugenzi wa TAKURURU.
Kiuchunguzi ilibidi aseme ni za serikali, lakini CAG na TRA wameongea kitaalam kuwa kuna element ya kodi, ambayo ni mali ya umma.
PAC wangechukua maelezo ya CAG na TRA
 
ukweli ni kwamba pinda amepoteza uhalali na sifa ya kugombea urais TZ. aende akafuge nyuki tu. hauziki hata wafanyeje.

Shida nikwamba,sisi mitandaoni na baadh ya vijana ndo hatumtaki huyu bwana.

Lakini,nyuka ya pazia jamaa(#pinda) anawatu Lukuki wanamhîtaji mno. Kuna wakulima,wafugaji,wavuvi & idadi ndogo ya wafanyabiashara.

#MY_TAKE ,
Huyu jamaa hachafuki kirahisi kwakweli. unless tuwaombe kina Lowasa wakate buti hukohuko mjengoni. Vinginevyo,sijui!!!!!!
 
Upande mwingine hawakufanya uchunguzi wa kina kama uliofanywa na CAG kwa miezi sita kwa kuangalia documents husika ambazo zilikuwa forged na wezi ili kuhakikisha wizi wao unakamilika, na pia hawakuangalia ushahidi toka bank ulionyesha zile pesa zote ziliwekwa na Tanesco na hivyo ni pesa za walipa kodi wa Tanzania tofauti na tulivyotaka kuaminishwa na wahuni na wezi kwamba pesa zile si za umma. Kwa hiyo utetezi wao utakuwa ni kubwabwaja tu na kutoa povu ili kumkingia kifua P.Pinda. Tumemchoka lazima atimuliwe tu.

 

pinda hamna kitu,
 

Sasa wewe "mtoto" unaamini uchafu wa mtu unapimwa na idadi ya watu waliopo nyuma yake!
 
CAG hakusema fedha ni za umma.
 
inawezekana hukuwa makini wakati ripoti inawasilishwa mkuu., pesa za escrow zilikuwa za umma kwa sababu zifuatazo. 1. Ni pesa ambazo zilitoka tanesco kwa walipa kodi. 2. Kutokana na tanesco kulalamikia iptl kulipwa zaidi kuliko inavyostahili mwishoni kulikuwa na zidio ambalo lilipaswa kurudishwa tanesco. 3. Kulikuwa na kodi ya V.A.T. Mkuu pinda hachomoki kwa sababu T.R.A ni taasisi ya serikali je pinda alishindwa kuwahoji ili kupata ukweli?
 
Kwa kauli yake ile wapigwe tu, pinda alipaswa kuondoka kwenye ofisi ya umma zamani sana, tatizo bunge letu linamadhaifu yake makubwa sana! Watetezi wake wengine wanajulikana kama kina sendeka, ebu tusubiri tuone!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…