Escrow: Kumbe PAC walituingiza choo cha sokoni (Part I)

Escrow: Kumbe PAC walituingiza choo cha sokoni (Part I)

UONGO WA RIPOTI YA PAC KUHUSIANA NA SAKATA LA ESCROW - PART 1.

Ripoti ya PAC Ukurasa wa 6 (kwa nakala iliyokuwa kwenye tovuti ya Bunge) unanukuliwa hivi:

“Mheshimiwa Spika, gharama hizi zilikoma kulipwa moja kwa moja kwa IPTL mwaka 2007 baada ya TANESCO kubaini kuwa IPTL inakokotoa gharama hizo kwa msingi wa USD 38.16 milioni (ambayo ni sehemu ya mkopo wa USD 105 milioni uliochukuliwa na wanahisa kutoka Umoja wa Mabenki ya Malaysia (Consortium of Malaysian Banks) ambao baadaye ulinunuliwa na Standard Chartered Bank ya Hong Kong) badala ya mtaji wa uwekezaji wa kiasi cha Sh. 50,000 uliosajiliwa BRELA na hivyo kufanya tozo ya capacity charges kuwa kubwa. Endapo ungetumika mtaji wa uwekezaji wa Sh. 50,000/= katika kukokotoa capacity charges TANESCO ingekuwa inalipa tozo ndogo kuliko ilivyo sasa.
Mheshimiwa Spika, kutokana na kutoridhishwa na kiwango cha capacity charges kilichokuwa kinatozwa na IPTL mnamo mwaka 2004, TANESCO ilifungua Shauri la Pili ICSID kupinga kiasi kikubwa cha tozo ya capacity charges. Uamuzi wa Baraza ilikuwa ni kwamba Wanahisa waketi na Mteja wao (TANESCO) na kukubaliana kuhusu kanuni ya ukokotoaji wa tozo hiyo.
Mheshimiwa Spika, mpaka tunapowasilisha Taarifa hii Bungeni, Uamuzi wa ICSID-2 kwamba IPTL ikae na TANESCO kwa ajili ya kukokotoa upya capacity charges haujatekelezwa, hivyo TANESCO wanaendelea kulipa USD. 2.6 milioni (sawasawa na shilingi 4,511,000,000/= kwa mwezi) kila mwezi kama capacity charges kwa IPTL izalishe au isizalishe umeme. Hivyo, utekelezaji wa Mkataba wa uzalishaji wa umeme kati ya IPTL na TANESCO umetawaliwa na migogoro toka ulipoanza mpaka sasa.”

NOTE:

Paragraph ya kwanza iliyonukuliwa hapo juu inadai mwaka 2007 TANESCO ilibaini tatizo halafu kwenye paragraph inayofuatia TANESCO ikaamua kufungua shauri ICSID mwaka 2004 kutokana na kutoridhishwa yale waliyoyabaini mwaka 2007. Tatizo linagunduliwa 2007 halafu unaenda kulifungulia shauri ICSID mwaka 2004?

FACTS:

• Hakuna kesi yoyote iliyofunguliwa ICSID mwaka 2004 na TANESCO.
• Kesi pekee iliyopata kufunguliwa ICSID na TANESCO ni ile kesi/shauri namba ARB/98/8 iliyofunguliwa mwaka 1998 na kutolewa uamuzi mwaka 2001. Kesi/shauri hilo linarejewa (referred as) kama ICSID-1 kwenye Ripoti ya PAC.

USHAHIDI:

• Ripoti ya PAC haijaweza kutuambia hiyo kesi iliyofunguliwa mwaka 2004 na kurejewa kama ICSID-2 ilikuwa kesi/shauri namba ngapi. Kwenye Ripoti yaPAC, ICSID-1 ilitajwa kama kesi iliyofunguliwa mwaka 1998 na namba yake kutajwa kama ARB/98/8 lakini Ripoti hiyo hiyo imeshindwa kutuambia namba ya kesi ya ICSID-2.
• Hivyo hivyo, hukumu ya kesi/shauri la ICSID-1 iliambatanishwa kwenye Ripoti ya PAC kama Kiambatanisho Na. 2 lakini Ripoti hiyo ya PAC haikuambatanisha hukumu ya hiyo kesi ICSID-2.
• Hata kwenye tovuti ya ICSID, hakuna kesi/shauri lolote lililofunguliwa na TANESCO 2004 ama kutolewa hukumu/maamuzi February 2004. Isitoshe hakuna kesi/shauri lolote lilifunguliwa na TANESCO zaidi ya ile kesi/shauri la ICSID-1.

HUKUMU YA ICSID-2 INACHANGANYWACHANGANYWA:

• Kwanza kwa sababu kulikuwa hakuna na kesi/shauri lililofunguliwa na TANESCO mwaka 2004 ICSID, ina maana pia kulikuwa hakuna hukumu ya hiyo kesi/shauri. Japo hiyo hukumu haipo lakini hukumu ya hiyo kesi/shauri imekuwa ikitajwa mara kadhaa. Kwenye paragraph ya pili hapo juu hiyo hukumu ya kesi isiyokuwepo inaelezwa kama “Uamuzi wa Baraza ilikuwa ni kwamba Wanahisa waketi na Mteja wao (TANESCO) na kukubaliana kuhusu kanuni ya ukokotoaji wa tozo hiyo” na kwenye paragraph inayofuatia kama “Uamuzi wa ICSID-2 kwamba IPTL ikae na TANESCO kwa ajili ya kukokotoa upya capacity charges haujatekelezwa...”. Kuna tofauti ya kukubaliana “kanuni ya ukokotoaji” na “kukutoa upya”. Kwa kiengereza ni “agree on formula to calculate” na “recalculate”.

TAREHE YA HUKUMU YA ICSID-2


Ukurasa wa 6 wa Ripoti ya PAC ulidai kuwa “mnamo mwaka 2004, TANESCO ilifungua Shauri la Pili ICSID kupinga” na kwenye Ukurasa wa 34 wa Ripoti ya PAC inadai inadai “.. (a) Kutekelezwa kwa uamuzi uliotolewa na Kituo cha Usuluhishi wa Migogoro ya Uwekezaji cha Kimataifa (ICSID) mwezi Februari 2004 (ICSID 2). Aidha ICSID 2 ilielekeza TANESCO na IPTL kukokotoa upya kiwango cha capacity charges”. Ni vigumu kuamini kuwa shauri linafunguliwa ICSID mwaka 2004 (hata kama lilifunguliwa tarehe 1 January 2004) likaja kupata ufumbuzi February 2004. Kama ilivyoelezwa hapo juu kulikuwa hakuna shauri lililofunguliwa na TANESCO kule ICSID mwaka 2004.


UZITO WA ICSIDI-2 KWENYE RIPOTI:


Hoja kuu ya Ripoti ya PAC ni kuwa fedha za Escrow zilikuwa “zimechotwa” kwa sababu makubaliano kati ya TANESCO na IPTL hayakuzangatia madai ya TANESCO yaliyopelekea kufungua ICSID-2 na uamuzi uliotolewa kwenye hukumu ya hiyo kes/shauri la ICSID-2. Tumeona hakuna ICSID-2 lakini uamuzi wa hukumu ya ICSID-2 imetumiwa kujenga hoja kuu mara kadhaa kwenye ripoti. Hiyo hukumu imetajwa kwenye ukurasa wa 6 (mara mbili), 23, 26, 34, 40 (mara mbili).


HITIMISHO:

Tuhuma kubwa zinatolewa kuwa fedha za Escrow zilitolewa kuilipa IPTL bila ya kuzingatia maamuzi ya kesi/shauri ICSID-2 kwenye kurasa hizo zote juu. ICSID-2 haiko, na hukumu ya ICSID-2 na tuhuma zote zinazohusisha ICSID-2 nazo ni TUHUMA ZA UONGO. Ripoti ya PAC imelidangaya Bunge na Taifa zima kwa ujumla.
Documents zote hapa: http://www.orcis.com/escrow

*Imeletwa kwenu kwa hisani kubwa ya Salim Khatri.
Go away! Njia pekee ya kumaliza ujambazi huu ni kwa fedha zetu kurejeshwa na wahusika kutiwa nguvuni
 
bwana jR sio mjinga kiasi hicho na huwa apigi madili Ya kijinga
Sawa pesa ni za IPTL na kubali
escrow ilikuwa na 306bl
Hisa za JR. 30% Ya hizo hela ni kama 92.bl hapo ni nje Ya hisa na Machmar anachokuwa zinazobaki . Sasa SINGASINGA yeye alichukua hayo mauzo Ya escrow ndo kununulia hisa za IPTL hiyo umuiona kwenye dunia ipi kama sio ufisadi?

si nasikia ruge ukiachia plot hajatoa hata sent kuchangia mtaji wa iptl?
 
mleta mada hapa kaua bend,hapa hata lisu lazima jasho litoke
 
UONGO WA RIPOTI YA PAC KUHUSIANA NA SAKATA LA ESCROW - PART 1.

Ripoti ya PAC Ukurasa wa 6 (kwa nakala iliyokuwa kwenye tovuti ya Bunge) unanukuliwa hivi:

“Mheshimiwa Spika, gharama hizi zilikoma kulipwa moja kwa moja kwa IPTL mwaka 2007 baada ya TANESCO kubaini kuwa IPTL inakokotoa gharama hizo kwa msingi wa USD 38.16 milioni (ambayo ni sehemu ya mkopo wa USD 105 milioni uliochukuliwa na wanahisa kutoka Umoja wa Mabenki ya Malaysia (Consortium of Malaysian Banks) ambao baadaye ulinunuliwa na Standard Chartered Bank ya Hong Kong) badala ya mtaji wa uwekezaji wa kiasi cha Sh. 50,000 uliosajiliwa BRELA na hivyo kufanya tozo ya capacity charges kuwa kubwa. Endapo ungetumika mtaji wa uwekezaji wa Sh. 50,000/= katika kukokotoa capacity charges TANESCO ingekuwa inalipa tozo ndogo kuliko ilivyo sasa.
Mheshimiwa Spika, kutokana na kutoridhishwa na kiwango cha capacity charges kilichokuwa kinatozwa na IPTL mnamo mwaka 2004, TANESCO ilifungua Shauri la Pili ICSID kupinga kiasi kikubwa cha tozo ya capacity charges. Uamuzi wa Baraza ilikuwa ni kwamba Wanahisa waketi na Mteja wao (TANESCO) na kukubaliana kuhusu kanuni ya ukokotoaji wa tozo hiyo.
Mheshimiwa Spika, mpaka tunapowasilisha Taarifa hii Bungeni, Uamuzi wa ICSID-2 kwamba IPTL ikae na TANESCO kwa ajili ya kukokotoa upya capacity charges haujatekelezwa, hivyo TANESCO wanaendelea kulipa USD. 2.6 milioni (sawasawa na shilingi 4,511,000,000/= kwa mwezi) kila mwezi kama capacity charges kwa IPTL izalishe au isizalishe umeme. Hivyo, utekelezaji wa Mkataba wa uzalishaji wa umeme kati ya IPTL na TANESCO umetawaliwa na migogoro toka ulipoanza mpaka sasa.”

NOTE:

Paragraph ya kwanza iliyonukuliwa hapo juu inadai mwaka 2007 TANESCO ilibaini tatizo halafu kwenye paragraph inayofuatia TANESCO ikaamua kufungua shauri ICSID mwaka 2004 kutokana na kutoridhishwa yale waliyoyabaini mwaka 2007. Tatizo linagunduliwa 2007 halafu unaenda kulifungulia shauri ICSID mwaka 2004?

FACTS:

• Hakuna kesi yoyote iliyofunguliwa ICSID mwaka 2004 na TANESCO.
• Kesi pekee iliyopata kufunguliwa ICSID na TANESCO ni ile kesi/shauri namba ARB/98/8 iliyofunguliwa mwaka 1998 na kutolewa uamuzi mwaka 2001. Kesi/shauri hilo linarejewa (referred as) kama ICSID-1 kwenye Ripoti ya PAC.

USHAHIDI:

• Ripoti ya PAC haijaweza kutuambia hiyo kesi iliyofunguliwa mwaka 2004 na kurejewa kama ICSID-2 ilikuwa kesi/shauri namba ngapi. Kwenye Ripoti yaPAC, ICSID-1 ilitajwa kama kesi iliyofunguliwa mwaka 1998 na namba yake kutajwa kama ARB/98/8 lakini Ripoti hiyo hiyo imeshindwa kutuambia namba ya kesi ya ICSID-2.
• Hivyo hivyo, hukumu ya kesi/shauri la ICSID-1 iliambatanishwa kwenye Ripoti ya PAC kama Kiambatanisho Na. 2 lakini Ripoti hiyo ya PAC haikuambatanisha hukumu ya hiyo kesi ICSID-2.
• Hata kwenye tovuti ya ICSID, hakuna kesi/shauri lolote lililofunguliwa na TANESCO 2004 ama kutolewa hukumu/maamuzi February 2004. Isitoshe hakuna kesi/shauri lolote lilifunguliwa na TANESCO zaidi ya ile kesi/shauri la ICSID-1.

HUKUMU YA ICSID-2 INACHANGANYWACHANGANYWA:

• Kwanza kwa sababu kulikuwa hakuna na kesi/shauri lililofunguliwa na TANESCO mwaka 2004 ICSID, ina maana pia kulikuwa hakuna hukumu ya hiyo kesi/shauri. Japo hiyo hukumu haipo lakini hukumu ya hiyo kesi/shauri imekuwa ikitajwa mara kadhaa. Kwenye paragraph ya pili hapo juu hiyo hukumu ya kesi isiyokuwepo inaelezwa kama “Uamuzi wa Baraza ilikuwa ni kwamba Wanahisa waketi na Mteja wao (TANESCO) na kukubaliana kuhusu kanuni ya ukokotoaji wa tozo hiyo” na kwenye paragraph inayofuatia kama “Uamuzi wa ICSID-2 kwamba IPTL ikae na TANESCO kwa ajili ya kukokotoa upya capacity charges haujatekelezwa...”. Kuna tofauti ya kukubaliana “kanuni ya ukokotoaji” na “kukutoa upya”. Kwa kiengereza ni “agree on formula to calculate” na “recalculate”.

TAREHE YA HUKUMU YA ICSID-2


Ukurasa wa 6 wa Ripoti ya PAC ulidai kuwa “mnamo mwaka 2004, TANESCO ilifungua Shauri la Pili ICSID kupinga” na kwenye Ukurasa wa 34 wa Ripoti ya PAC inadai inadai “.. (a) Kutekelezwa kwa uamuzi uliotolewa na Kituo cha Usuluhishi wa Migogoro ya Uwekezaji cha Kimataifa (ICSID) mwezi Februari 2004 (ICSID 2). Aidha ICSID 2 ilielekeza TANESCO na IPTL kukokotoa upya kiwango cha capacity charges”. Ni vigumu kuamini kuwa shauri linafunguliwa ICSID mwaka 2004 (hata kama lilifunguliwa tarehe 1 January 2004) likaja kupata ufumbuzi February 2004. Kama ilivyoelezwa hapo juu kulikuwa hakuna shauri lililofunguliwa na TANESCO kule ICSID mwaka 2004.


UZITO WA ICSIDI-2 KWENYE RIPOTI:


Hoja kuu ya Ripoti ya PAC ni kuwa fedha za Escrow zilikuwa “zimechotwa” kwa sababu makubaliano kati ya TANESCO na IPTL hayakuzangatia madai ya TANESCO yaliyopelekea kufungua ICSID-2 na uamuzi uliotolewa kwenye hukumu ya hiyo kes/shauri la ICSID-2. Tumeona hakuna ICSID-2 lakini uamuzi wa hukumu ya ICSID-2 imetumiwa kujenga hoja kuu mara kadhaa kwenye ripoti. Hiyo hukumu imetajwa kwenye ukurasa wa 6 (mara mbili), 23, 26, 34, 40 (mara mbili).


HITIMISHO:

Tuhuma kubwa zinatolewa kuwa fedha za Escrow zilitolewa kuilipa IPTL bila ya kuzingatia maamuzi ya kesi/shauri ICSID-2 kwenye kurasa hizo zote juu. ICSID-2 haiko, na hukumu ya ICSID-2 na tuhuma zote zinazohusisha ICSID-2 nazo ni TUHUMA ZA UONGO. Ripoti ya PAC imelidangaya Bunge na Taifa zima kwa ujumla.
Documents zote hapa: http://www.orcis.com/escrow

*Imeletwa kwenu kwa hisani kubwa ya Salim Khatri.

Hata kama unavyo urge ni kweli, lakini bado hujajenga hoja kwa nini TEGETA ESCROW sio ufisadi ila ni malipo halali. Kwa nini PAC iligushi nyaraka za usajili?Kwa nini watu walipwe pesa na wote na watumishi wa serikali (mawaziri, mawaziri au wabumge wastaafu, majaji nk), kwa nini pesa itolewa haraka haraka katika account na pengine account hizo kufungwa? Na kubwa zaidi, tunajua Seth alikuwa katika scandal ya Kenya ya Goldenberg, tena katajwa safari nyingi sana na report ya wikileak. Iweje FISADI tena mkubwa hivi aruhusiwe kuwekeza kwa mradi sawa na ule ule alo fanya Kenya?Maswali ni mengi sana, ambayo kwayo tu bila hata uchunguzi wa CAJ na PAC akili hata ya mtoto inaelewa kuna ufisadi hapa. Ilichotusaidia kamati ya Zito ni details tu basi.
 
Hapo tumedanganywa hapa huwezi kumuona Tumbiri wala Nyepesi kujibu hoja hizi
 
UONGO WA RIPOTI YA PAC KUHUSIANA NA SAKATA LA ESCROW - PART 1.

Ripoti ya PAC Ukurasa wa 6 (kwa nakala iliyokuwa kwenye tovuti ya Bunge) unanukuliwa hivi:

“Mheshimiwa Spika, gharama hizi zilikoma kulipwa moja kwa moja kwa IPTL mwaka 2007 baada ya TANESCO kubaini kuwa IPTL inakokotoa gharama hizo kwa msingi wa USD 38.16 milioni (ambayo ni sehemu ya mkopo wa USD 105 milioni uliochukuliwa na wanahisa kutoka Umoja wa Mabenki ya Malaysia (Consortium of Malaysian Banks) ambao baadaye ulinunuliwa na Standard Chartered Bank ya Hong Kong) badala ya mtaji wa uwekezaji wa kiasi cha Sh. 50,000 uliosajiliwa BRELA na hivyo kufanya tozo ya capacity charges kuwa kubwa. Endapo ungetumika mtaji wa uwekezaji wa Sh. 50,000/= katika kukokotoa capacity charges TANESCO ingekuwa inalipa tozo ndogo kuliko ilivyo sasa.
Mheshimiwa Spika, kutokana na kutoridhishwa na kiwango cha capacity charges kilichokuwa kinatozwa na IPTL mnamo mwaka 2004, TANESCO ilifungua Shauri la Pili ICSID kupinga kiasi kikubwa cha tozo ya capacity charges. Uamuzi wa Baraza ilikuwa ni kwamba Wanahisa waketi na Mteja wao (TANESCO) na kukubaliana kuhusu kanuni ya ukokotoaji wa tozo hiyo.
Mheshimiwa Spika, mpaka tunapowasilisha Taarifa hii Bungeni, Uamuzi wa ICSID-2 kwamba IPTL ikae na TANESCO kwa ajili ya kukokotoa upya capacity charges haujatekelezwa, hivyo TANESCO wanaendelea kulipa USD. 2.6 milioni (sawasawa na shilingi 4,511,000,000/= kwa mwezi) kila mwezi kama capacity charges kwa IPTL izalishe au isizalishe umeme. Hivyo, utekelezaji wa Mkataba wa uzalishaji wa umeme kati ya IPTL na TANESCO umetawaliwa na migogoro toka ulipoanza mpaka sasa.”

NOTE:

Paragraph ya kwanza iliyonukuliwa hapo juu inadai mwaka 2007 TANESCO ilibaini tatizo halafu kwenye paragraph inayofuatia TANESCO ikaamua kufungua shauri ICSID mwaka 2004 kutokana na kutoridhishwa yale waliyoyabaini mwaka 2007. Tatizo linagunduliwa 2007 halafu unaenda kulifungulia shauri ICSID mwaka 2004?

FACTS:

• Hakuna kesi yoyote iliyofunguliwa ICSID mwaka 2004 na TANESCO.
• Kesi pekee iliyopata kufunguliwa ICSID na TANESCO ni ile kesi/shauri namba ARB/98/8 iliyofunguliwa mwaka 1998 na kutolewa uamuzi mwaka 2001. Kesi/shauri hilo linarejewa (referred as) kama ICSID-1 kwenye Ripoti ya PAC.

USHAHIDI:

• Ripoti ya PAC haijaweza kutuambia hiyo kesi iliyofunguliwa mwaka 2004 na kurejewa kama ICSID-2 ilikuwa kesi/shauri namba ngapi. Kwenye Ripoti yaPAC, ICSID-1 ilitajwa kama kesi iliyofunguliwa mwaka 1998 na namba yake kutajwa kama ARB/98/8 lakini Ripoti hiyo hiyo imeshindwa kutuambia namba ya kesi ya ICSID-2.
• Hivyo hivyo, hukumu ya kesi/shauri la ICSID-1 iliambatanishwa kwenye Ripoti ya PAC kama Kiambatanisho Na. 2 lakini Ripoti hiyo ya PAC haikuambatanisha hukumu ya hiyo kesi ICSID-2.
• Hata kwenye tovuti ya ICSID, hakuna kesi/shauri lolote lililofunguliwa na TANESCO 2004 ama kutolewa hukumu/maamuzi February 2004. Isitoshe hakuna kesi/shauri lolote lilifunguliwa na TANESCO zaidi ya ile kesi/shauri la ICSID-1.

HUKUMU YA ICSID-2 INACHANGANYWACHANGANYWA:

• Kwanza kwa sababu kulikuwa hakuna na kesi/shauri lililofunguliwa na TANESCO mwaka 2004 ICSID, ina maana pia kulikuwa hakuna hukumu ya hiyo kesi/shauri. Japo hiyo hukumu haipo lakini hukumu ya hiyo kesi/shauri imekuwa ikitajwa mara kadhaa. Kwenye paragraph ya pili hapo juu hiyo hukumu ya kesi isiyokuwepo inaelezwa kama “Uamuzi wa Baraza ilikuwa ni kwamba Wanahisa waketi na Mteja wao (TANESCO) na kukubaliana kuhusu kanuni ya ukokotoaji wa tozo hiyo” na kwenye paragraph inayofuatia kama “Uamuzi wa ICSID-2 kwamba IPTL ikae na TANESCO kwa ajili ya kukokotoa upya capacity charges haujatekelezwa...”. Kuna tofauti ya kukubaliana “kanuni ya ukokotoaji” na “kukutoa upya”. Kwa kiengereza ni “agree on formula to calculate” na “recalculate”.

TAREHE YA HUKUMU YA ICSID-2


Ukurasa wa 6 wa Ripoti ya PAC ulidai kuwa “mnamo mwaka 2004, TANESCO ilifungua Shauri la Pili ICSID kupinga” na kwenye Ukurasa wa 34 wa Ripoti ya PAC inadai inadai “.. (a) Kutekelezwa kwa uamuzi uliotolewa na Kituo cha Usuluhishi wa Migogoro ya Uwekezaji cha Kimataifa (ICSID) mwezi Februari 2004 (ICSID 2). Aidha ICSID 2 ilielekeza TANESCO na IPTL kukokotoa upya kiwango cha capacity charges”. Ni vigumu kuamini kuwa shauri linafunguliwa ICSID mwaka 2004 (hata kama lilifunguliwa tarehe 1 January 2004) likaja kupata ufumbuzi February 2004. Kama ilivyoelezwa hapo juu kulikuwa hakuna shauri lililofunguliwa na TANESCO kule ICSID mwaka 2004.


UZITO WA ICSIDI-2 KWENYE RIPOTI:


Hoja kuu ya Ripoti ya PAC ni kuwa fedha za Escrow zilikuwa “zimechotwa” kwa sababu makubaliano kati ya TANESCO na IPTL hayakuzangatia madai ya TANESCO yaliyopelekea kufungua ICSID-2 na uamuzi uliotolewa kwenye hukumu ya hiyo kes/shauri la ICSID-2. Tumeona hakuna ICSID-2 lakini uamuzi wa hukumu ya ICSID-2 imetumiwa kujenga hoja kuu mara kadhaa kwenye ripoti. Hiyo hukumu imetajwa kwenye ukurasa wa 6 (mara mbili), 23, 26, 34, 40 (mara mbili).


HITIMISHO:

Tuhuma kubwa zinatolewa kuwa fedha za Escrow zilitolewa kuilipa IPTL bila ya kuzingatia maamuzi ya kesi/shauri ICSID-2 kwenye kurasa hizo zote juu. ICSID-2 haiko, na hukumu ya ICSID-2 na tuhuma zote zinazohusisha ICSID-2 nazo ni TUHUMA ZA UONGO. Ripoti ya PAC imelidangaya Bunge na Taifa zima kwa ujumla.
Documents zote hapa: http://www.orcis.com/escrow

*Imeletwa kwenu kwa hisani kubwa ya Salim Khatri.

Mbona mnakuwa kama akili hizipo sawa? Ww unafikili takukuru,CAG,POLICE na bunge wamedanganya?acha kupotosha umma wewe kama una babayako subili utalidhi ujinga badae tuachie kwanza hil taifa cc umoja wa katiba ya wananchi.
 
uongo wa ripoti ya pac kuhusiana na sakata la escrow - part 1.

Ripoti ya pac ukurasa wa 6 (kwa nakala iliyokuwa kwenye tovuti ya bunge) unanukuliwa hivi:

“mheshimiwa spika, gharama hizi zilikoma kulipwa moja kwa moja kwa iptl mwaka 2007 baada ya tanesco kubaini kuwa iptl inakokotoa gharama hizo kwa msingi wa usd 38.16 milioni (ambayo ni sehemu ya mkopo wa usd 105 milioni uliochukuliwa na wanahisa kutoka umoja wa mabenki ya malaysia (consortium of malaysian banks) ambao baadaye ulinunuliwa na standard chartered bank ya hong kong) badala ya mtaji wa uwekezaji wa kiasi cha sh. 50,000 uliosajiliwa brela na hivyo kufanya tozo ya capacity charges kuwa kubwa. Endapo ungetumika mtaji wa uwekezaji wa sh. 50,000/= katika kukokotoa capacity charges tanesco ingekuwa inalipa tozo ndogo kuliko ilivyo sasa.
Mheshimiwa spika, kutokana na kutoridhishwa na kiwango cha capacity charges kilichokuwa kinatozwa na iptl mnamo mwaka 2004, tanesco ilifungua shauri la pili icsid kupinga kiasi kikubwa cha tozo ya capacity charges. Uamuzi wa baraza ilikuwa ni kwamba wanahisa waketi na mteja wao (tanesco) na kukubaliana kuhusu kanuni ya ukokotoaji wa tozo hiyo.
Mheshimiwa spika, mpaka tunapowasilisha taarifa hii bungeni, uamuzi wa icsid-2 kwamba iptl ikae na tanesco kwa ajili ya kukokotoa upya capacity charges haujatekelezwa, hivyo tanesco wanaendelea kulipa usd. 2.6 milioni (sawasawa na shilingi 4,511,000,000/= kwa mwezi) kila mwezi kama capacity charges kwa iptl izalishe au isizalishe umeme. Hivyo, utekelezaji wa mkataba wa uzalishaji wa umeme kati ya iptl na tanesco umetawaliwa na migogoro toka ulipoanza mpaka sasa.”

note:

Paragraph ya kwanza iliyonukuliwa hapo juu inadai mwaka 2007 tanesco ilibaini tatizo halafu kwenye paragraph inayofuatia tanesco ikaamua kufungua shauri icsid mwaka 2004 kutokana na kutoridhishwa yale waliyoyabaini mwaka 2007. Tatizo linagunduliwa 2007 halafu unaenda kulifungulia shauri icsid mwaka 2004?

Facts:

• hakuna kesi yoyote iliyofunguliwa icsid mwaka 2004 na tanesco.
• kesi pekee iliyopata kufunguliwa icsid na tanesco ni ile kesi/shauri namba arb/98/8 iliyofunguliwa mwaka 1998 na kutolewa uamuzi mwaka 2001. Kesi/shauri hilo linarejewa (referred as) kama icsid-1 kwenye ripoti ya pac.

Ushahidi:

• ripoti ya pac haijaweza kutuambia hiyo kesi iliyofunguliwa mwaka 2004 na kurejewa kama icsid-2 ilikuwa kesi/shauri namba ngapi. Kwenye ripoti yapac, icsid-1 ilitajwa kama kesi iliyofunguliwa mwaka 1998 na namba yake kutajwa kama arb/98/8 lakini ripoti hiyo hiyo imeshindwa kutuambia namba ya kesi ya icsid-2.
• hivyo hivyo, hukumu ya kesi/shauri la icsid-1 iliambatanishwa kwenye ripoti ya pac kama kiambatanisho na. 2 lakini ripoti hiyo ya pac haikuambatanisha hukumu ya hiyo kesi icsid-2.
• hata kwenye tovuti ya icsid, hakuna kesi/shauri lolote lililofunguliwa na tanesco 2004 ama kutolewa hukumu/maamuzi february 2004. Isitoshe hakuna kesi/shauri lolote lilifunguliwa na tanesco zaidi ya ile kesi/shauri la icsid-1.

Hukumu ya icsid-2 inachanganywachanganywa:

• kwanza kwa sababu kulikuwa hakuna na kesi/shauri lililofunguliwa na tanesco mwaka 2004 icsid, ina maana pia kulikuwa hakuna hukumu ya hiyo kesi/shauri. Japo hiyo hukumu haipo lakini hukumu ya hiyo kesi/shauri imekuwa ikitajwa mara kadhaa. Kwenye paragraph ya pili hapo juu hiyo hukumu ya kesi isiyokuwepo inaelezwa kama “uamuzi wa baraza ilikuwa ni kwamba wanahisa waketi na mteja wao (tanesco) na kukubaliana kuhusu kanuni ya ukokotoaji wa tozo hiyo” na kwenye paragraph inayofuatia kama “uamuzi wa icsid-2 kwamba iptl ikae na tanesco kwa ajili ya kukokotoa upya capacity charges haujatekelezwa...”. Kuna tofauti ya kukubaliana “kanuni ya ukokotoaji” na “kukutoa upya”. Kwa kiengereza ni “agree on formula to calculate” na “recalculate”.

Tarehe ya hukumu ya icsid-2


ukurasa wa 6 wa ripoti ya pac ulidai kuwa “mnamo mwaka 2004, tanesco ilifungua shauri la pili icsid kupinga” na kwenye ukurasa wa 34 wa ripoti ya pac inadai inadai “.. (a) kutekelezwa kwa uamuzi uliotolewa na kituo cha usuluhishi wa migogoro ya uwekezaji cha kimataifa (icsid) mwezi februari 2004 (icsid 2). Aidha icsid 2 ilielekeza tanesco na iptl kukokotoa upya kiwango cha capacity charges”. Ni vigumu kuamini kuwa shauri linafunguliwa icsid mwaka 2004 (hata kama lilifunguliwa tarehe 1 january 2004) likaja kupata ufumbuzi february 2004. Kama ilivyoelezwa hapo juu kulikuwa hakuna shauri lililofunguliwa na tanesco kule icsid mwaka 2004.


Uzito wa icsidi-2 kwenye ripoti:


Hoja kuu ya ripoti ya pac ni kuwa fedha za escrow zilikuwa “zimechotwa” kwa sababu makubaliano kati ya tanesco na iptl hayakuzangatia madai ya tanesco yaliyopelekea kufungua icsid-2 na uamuzi uliotolewa kwenye hukumu ya hiyo kes/shauri la icsid-2. Tumeona hakuna icsid-2 lakini uamuzi wa hukumu ya icsid-2 imetumiwa kujenga hoja kuu mara kadhaa kwenye ripoti. Hiyo hukumu imetajwa kwenye ukurasa wa 6 (mara mbili), 23, 26, 34, 40 (mara mbili).


Hitimisho:

Tuhuma kubwa zinatolewa kuwa fedha za escrow zilitolewa kuilipa iptl bila ya kuzingatia maamuzi ya kesi/shauri icsid-2 kwenye kurasa hizo zote juu. Icsid-2 haiko, na hukumu ya icsid-2 na tuhuma zote zinazohusisha icsid-2 nazo ni tuhuma za uongo. Ripoti ya pac imelidangaya bunge na taifa zima kwa ujumla.
Documents zote hapa: http://www.orcis.com/escrow

*imeletwa kwenu kwa hisani kubwa ya salim khatri.

hata mje na facts zaaje ukweli utabaki kuwa j.kikwete amewalinda wezi walokwapua mabilioni ya umma na wakagawana kama njugu.
Na mbaya zaidi wengine wakabeba kwenye kifuko ya sandalusi!
<<<ikiwa ag alibainika kukiuka taratibu za ushauri wa kifedha basi hata mchakato mzima wote ulikuwa ni kharamu!
 
where did the escrow fund go? hili ndo swali
 
Nilicho jifunza katika matukio kama EPA, Escrow, Richmond, Tan Gold nk, si police, TISS wala chombo chochote cha ulinzi kilichowahi hata kunusa, yote is either vyombo vya habari au wapinzani; to me hawa ndio wanaongoza nchi.
 
Sitaki kuamini kuwa ripoti nzima itakosa uhalali kutokana na kasoro hii ila nachoamini ni kuwa kunahitajika ufafanuzi kidogo tu au kufanya marekebisho ya kiuandishi tu.

hoja kwamba hakukua na ISCID -2 ndo ishu
 
yani rukeni juu, tueni chini, laleni, simameni,jikunjeni kama chura ila ukweli uko wazi kuwa Kikwete anatetea wizi wa ESCROW kwasababu yeye ndio mnufaika mkuu wa sakata hili.
mpaka sasa wahisani hawana hamu na sisi kwa uwizi huu wa uliofanywa na wateule wa raisi na raisi mwenyewe.

Hii itakuja kuingia kwenye historia. Kwamba mfanya biashara anayefanya biashara "halali" analipwa hela zake kisha anaamua kugawa mabilioni na mamilioni kwa Watendaji wakuu wa serikali mawizarani, RITA, Ikulu, makanisani, TRA na kwingine lakini wote waliofanikisha fedha hizo kutoka.
Huyu ndiye Mfanyabiashara "mwema sana" kuliko hata Bill Gates. Hivyo ndio wanavyotaka kutuaminisha. Sawa, sisi kama Watanzania wanaweza kutulazimisha kukubali kuwa huo ndio ukweli wenyewe lakini ABADANI hilo haliwezekani kwa wale wahisani wanaokusanya kodi kwa raia wao ili kipatokane cha kutupatia sisi kuendesha serikali yetu. Hawatakubali hizi ngonjera.
Hii ni sawa na issue ya RADA, walituambia tunaibiwa sisi tukasema hamna kitu kama hicho. Wakafuatilia na fedha ikapatikana na kuamriwa irudishwe. La ajabu bila aibu eti tukaiita CHENJI YA RADA na bila aibu majadiliano yakatinga Bungeni kubishania jinsi ya kupanga matumizi ya fedha hizo huku tukishindwa kuwafanya kitu wahusika zaidi ya kuwapa vyeo vya wenyeviti wa kamati ya bajeti ili wazipangie bajeti fedha za Chenji ya rada.
Kuna wakati utafika hapa duniani mtu akitaka kukutukana anasema " Wewe mjinga kama Mtanzania!"
 
ImageUploadedByJamiiForums1419709626.767464.jpg
Hiki ndicho kinachofanyika kwa sasa. Na ni bahati mbaya sana falsafa hii imeshavamia hapa JF kwa nguvu kubwa na watu wako kazini.
 
Hiviiiiiiii,let say ni kweli hela zote ni za IPTL,swali la msingi la kujiuliza ni, je hakuwa na kazi nazo hadi agawe kama njugu kama kweli zote ni halali yake kweli?????,inawezekana hela yako halali ukaigawa kama njugu kwa kiasi hcho kweli,hakuna mazingira ya rushwa kweli?????
rushwa ili apate nini ili hali yeye kauza hisa zake?
 
au labda siku hizi ukitaka kuuza hisa mpaka utoe rushwa labda
 
Watanzania tulikua wajinga na wapumbavu kwa kiasi kikubwa. Sasa wajinga wameanza kupungua na ipo siku wataisha kabisa na Tanzania ya waerevu na wazalendo itazaliwa. Hili ndilo mleta mada na CCM hawalioni. Hawaoni mabadiliko yalivyo na kasi katika nchi hii, washinda na kulala wakizania wataendelea kututawala kwa ujinga wetu. Na Mungu atakua upande wetu kwani hatawaamsha hadi pale watakapoanguka.

KIM KARDASH ngoja niamini kuwa haya uliyoyaandika ni mashiko kweli na hivyo fedha zote ni halali kwenda IPTL kama unavyotaka tuamini. Lakini (hata raisi anakiri kuwa) kodi haikulipwa kwa makosa ya AG. Adhabu ya kuikosesha mapato serikali zaidi ya 30bn ni kujiuzulu tu? Eti sasa wameiomba IPTL ilipe kodi, WANAIOMBA. Ni aibu gani hii.

Jambo jingine ndugu yangu hata kama fedha zote zile ni halali kwa IPTL, je utakatishaji wa fedha ulifanywa ili kumficha nani? Uchukuaji fedha Mkombozi Bank na Stanbic ulifuta sheria za nchi kweli? Kama utakubali utakasishaji ulifanywa, je hakuna wa kuwajibika? Lipite tu kama nchi haina watu? Tunaenda wapi?

Ndugu yangu mtoa mada, serikali na Chama cha Mapinduzi hata kikitakasika katika sakata hili la ESCROW lakini bado harufu ya madudu mengi yanayoendelea kufanywa haitaisha. Kubaliana na mimi tunahitaji mabadiliko makubwa kama tuna dhamira ya kweli ya maendeleo yanayowanufaisha Watanzania wote.
 
Back
Top Bottom