Escrow kuiadhiri CCM

Escrow kuiadhiri CCM

BAK

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2007
Posts
124,769
Reaction score
288,283
Escrow kuiadhiri CCM


  • Zitto asema ripoti yake haizuiliki
  • CAG kuanika madudu wiki hii
26/10/2014 | Na Abdallah Khamis |



HARAKATI za Chama cha Mapinduzi(CCM),kutaka ripoti ya uchunguzi wa akaunti ya Tegeta Escrow, isijadiliwe bungeni huenda zikagonga mwamba, Tanzania Daima Jumapili, limebaini
.

Jitihada hizo zinaweza kutoweka baada ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG), kukamilisha uchunguzi wake na anatarajia kuwasilisha ripoti hiyo kwa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali inayoongozwa na Zitto Kabwe.

Iwapo ripoti hiyo itawasilisha, inaweza kukipasua Chama Cha Mapinduzi (CCM) na serikali yake ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikituhumiwa kwa kulea na kulinda ufisadi
Tanzania Daima Jumapili, lilidokezwa kuwa CCM inahofia ripoti inaweza kuwagusa vigogo, mawaziri na watendaji wa serikali ambao itamlazimu Rais Jakaya Kikwete, kulivunja baraza la mawaziri.

Inaelezwa kwamba, ripoti hiyo huenda ikawagusa baadhi ya mawaziri waandamizi wa serikali na viongozi wa CCM miongoni mwao, ni wale walioanza harakati za kuwania urais katika uchaguzi ujao.
Kufikishwa bungeni kwa ripoti hiyo, kunatabiriwa litakuwa anguko jingine kwa serikali kama ilivyokuwa mwaka 2008 alipong'oka Waziri Mkuu Edward Lowassa kwa kashfa ya kutoa zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura kwa timu ya Richmond.


Kashfa hiyo ya Richmond ilitengeneza uhasama miongoni mwa makada wa CCM hata kukifanya chama hicho, kipoteza majimbo mengi katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.
Mbali na Richmond kukitesa CCM na serikali pia uhasama wa makada wake umekijengea makundi yanayotishia uhai wake.

Vigogo wa CCM na serikali yake hawataki ripoti hiyo iwasilishwe bungeni kwasababu itawaweka katika wakati mgumu wa kushinda uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika Disemba mwaka huu.
Katika kikao cha Halmashauri Kuu (NEC), ya CCM kilichokaa hivi karibuni mjini Dodoma suala hilo liiibuka ambapo Christopher ole Sendeka, anadaiwa kusimama katika kikao hicho na kueleza wazi kuwa chama chao kinachafuliwa na ufisadi wa IPTL na kwamba fedha hizo zinatumika Dodoma kwenye kampeni za urais.

Madai ya Sendeka, yalizimwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete, akisema kuwa suala la IPTL waliache kwanza maana wanasubiri ripoti ya uchunguzi unaoendelea hivi sasa.

Hata hivyo wakati hali ikionekana kuwa tete, Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge na hesabu za serikali (PAC), Zitto Kabwe,ameshamuandikia barua CAG, kumueleza umuhimu wa ripoti hiyo.
Zitto alisema suala hilo lazima litafika bungeni hata kama CCM hawataki jambo hilo lifike, kwa
sababu kamati yake ndiyo yenye jukumu la kufanyia kazi na kulipeleka huko.

Alisema CAG alitakiwa kutoa taarifa ya uchunguzi huo wiki iliyopita lakini aliomba apeleke taarifa wiki hii.
"Tukishakutana na CAG wiki hii, suala hili litajadiliwa kwenye vikao vya Bunge la 17 au 18, kulingana na mpangilio wa shughuli za Bunge, hili haliwezi kukwepeka"
"Sisi kazi yetu ni kulifikisha bungeni suala hili na wabunge wana uamuzi…hili la kuzuia sidhani kama litafanikiwa" alisema Zitto.
Zitto alibainisha kuwa Oktoba 24 mwaka huu, alimuandikia barua CAG akimueleza umuhimu wa ripoti hiyo kwa taifa.

Katika barua hiyo ambayo Tanzania Daima Jumapili, imefanikiwa kuiona Zitto anasema uchunguzi wa ripoti hiyo utaiokoa nchi na mpasuko unaoweza kujitokeza baada ya wafadhili wa serikali kuacha kutoa misaada kwa Tanzania mpaka ripoti ya Tegeta Escrow itakapowekwa hadharani.

Sehemu ya barua hiyo inasomeka "Kamati imejulishwa na wizara ya fedha na Benki Kuu kwamba uamuzi wa wafadhili kuzuia misaada ya kibajeti unaathiri sana utekelezaji wa bajeti,
Sharti la kutolewa misaada hiyo ni taarifa hii kutolewa kwa vyombo vilivyoomba, kuendelea kuchelewa kutoa taarifa kutaumiza zaidi wananchi kwa kukosa dawa hospitalini na hata mishahara kukosekana"iliandikwa.

Barua hiyo imeongeza kuwa gavana wa Benki Kuu ameijulisha kamati kuwa serikali imeanza kukopa katika soko la ndani na kuathiri uchumi kwa kushindwa na sekta na hivyo kuongeza riba na kusababisha uchumi wa nchi kusinyaa.

Mbali na Zitto, mbunge wa Kigoma Kusini,David Kafulila alisema ripoti hiyo isipowasilishwa bungeni atawasilisha hoja binafsi ya kutokuwa na imani na serikali.
Kafulila alisema anaamini ofisi ya CAG inakabiliwa na shinikizo kutoka kwa vigogo wakubwa serikalini wanaohusika na ufisadi huo.

Alisema uhakika wa jambo hilo unadhihirishwa na muda alioutumia CAG ni zaidi ya ule alioomba bungeni kwamba kazi hiyo ingekamilika baada ya siku 45 na kwamba mpaka jana ni zaidi ya siku 200 zimepita huku ripoti hiyo ikiwa imekaliwa.

"Nashangaa PCCB wamemaliza kazi na kwenda kuikabidhi Ikulu badala ya kumfikishia mwendesha mashtaka(DPP), ili aweze kuwachukulia hatua wahusika kwa kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria, Hosea anapaswa kuwasilisha ripoti yake bungeni kwa sababu aliagizwa na Bunge na siyo Ikulu"alisema Kafulila katika ujumbe mfupi wa simu kwa gazeti hili.

Sakata la Escrow liliibuliwa na Kafulila Mei 8 mwaka huu akiwa bungeni mjini Dodoma na kuwatuhumu baadhi ya vigogo wa serikali kuwa nyuma ya uchotwaji wa dola za marekani kiasi cha milioni 122 sawa na shilingi za kitanzania bilioni 200.

Vigogo waliotajwa na Kafulila ni Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospiter Muhongo na Katibu Mkuu wake, Eliakim Maswi, Waziri wa Fedha Saada Mkuya, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Beno Ndullu, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Frederick Werema na Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Mhandisi Felchesmi Mramba.

Kafulila alisema vigogo hao wamehusika na ufisadi wa fedha hizo zilizokuwa zimewekwa katika akaunti ya Baraza la Usuluhishi la Migogoro ya Kibiashara (ESCROW) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

CC: Tized, Mr Rocky, Fixed Point, Chakaza, Elly B, MziziMkavu, Power to the People, Jasusi, Eiyer, idawa, nguruvi, Mentor, Sikonge, Dingswayo, MANI, tpaul, Bramo, Bulesi Bulldog, Sangarara, MTAZAMO, Erythrocyte, Mag3, Mimibaba, zumbemkuu, Crashwise, amkawewe, Idimi, Ogah, Chakaza, mshana jr, JokaKuu, MWALLA, genekai, PRINCE CROWN, Tuko, Shark, lynxeffect22, samaki2011, MoudyBoka, adolay, Elli, nyabhingi, Janjaweed, S.N.Jilala, MEANDU, Tabby, Candid Scope, August, BONGOLALA, Gefu, Bigirita, Kozo Okamoto, Daudi Mchambuzi
 
tuwashukuru sana wazungu kwa kuingilia kati jambo hili , vinginevyo tungepigwa bila huruma .
 
  • Thanks
Reactions: BAK
CCM, Tanzania, masikini, Wahisani, bajeti, ufisadi, China, Magharibi....

Nikiunganisha haya maneno alafu nikaona jinsi CCM wanavyoliendesha hili suala nakumbuka ule msemo
"Unatishia kujamba wakati unaharisha? Utaumbuka"...
 
Haya mambo ya ufadhili, uhisani ni matatizo. Kwa nini tuwekewe masharti na watu wa nje, hayo ndiyo yawe sababu kuu kuliko matakwa ya wananchi wetu. Ukiangalia serikali yetu inatenda jambo tu pale inapolazimishwa na waitwao wafadhili/wahisani kwa jambo amabalo wananchi wetu wanalidai kwa kitambao kirefu bila mafanikio! Ninakerwa sana na hili. Ni umasikini wetu au ulimbukeni? Tulikuwa huko nyuma na siasa nzuri ya "ujamaa na kujitegemea". Tumeacha ujamaa, je hata kujitegemea pia tumeacha!!?
 
Taifa la Tanzania chini ya ccm ya bwana anga/Mtembezi - kikwete imepoteza utu heshima na maadili yaliyojengwa na waasisi kwa muda mrefu.

1. CCM na serikali yake wamefilisi mashirika ya hifadhi za jamii yote, baada ya kufilisi hazina wamehamia kuteka fedha

zetu za maisha hapo uzeeni, wasivo na aibu wakataka watuwekee na mipaka 60yrs kuchukuwa bila kuwa makini mchwa

hawa wangetafuna hazina zote za mifuko ya hifadhi ya jamii.

2. Sasa hivi serikali ya ccm inaiba kupitia mikataba hewa ya kutengeza, bajeti feki nk ilikuchota fedha zetu

hazina. Kashifa hii nimoja ya kashifa lukuki za mafisadi wa ccm na serikali yake kutuibia ngawira zetu. Hapa tuwashukuru

wazungu japokuwa bado ccm wanawezapindisha ukweli nakutudanganya.

a) Nani aliweka fedha hizi kwenye account hii

b) kwanini ziliwekwa

c) zilitoka wapi na kwanini

d) Vipi usiri kutawala na hata ccm na serikali yake hawataki fedha na account hii vijadiliwe?


CCM na serikali yake wamekosa weledi, heshima na wamegeuka genge la wezi na madikiteta kulazimisha ushenzi

uonekane haki na haki kuonekana ushenzi
, tunasafari ndefu japokuwa tiba ya haya yote ni kuwatowa ccm madarakani.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Haya mambo ya ufadhili, uhisani ni matatizo. Kwa nini tuwekewe masharti na watu wa nje, hayo ndiyo yawe sababu kuu kuliko matakwa ya wananchi wetu. Ukiangalia serikali yetu inatenda jambo tu pale inapolazimishwa na waitwao wafadhili/wahisani kwa jambo amabalo wananchi wetu wanalidai kwa kitambao kirefu bila mafanikio! Ninakerwa sana na hili. Ni umasikini wetu au ulimbukeni? Tulikuwa huko nyuma na siasa nzuri ya "ujamaa na kujitegemea". Tumeacha ujamaa, je hata kujitegemea pia tumeacha!!?

hata mimi nashangazwa na hili jambo, kwanini tushindwe kujiamulia mambo yetu wenyewe
 
Asante mkuu kwa taarifa.
Hili suala linazidi kuumiza vichwa. Naamini mwenye busara na nguvu wataiokoa nchi badala ya mafisadi wachache.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Tanzania Daima Chadema daima Uzushi daima....ati harakati za CCM kuzuia...uzushi mwingine bwana wa kitoto kabisa...Bunge limemtaka CAG afanye ukaguzi na atoe ripoti sasa CCM wanaingiaje hapo?? huu ulafi wa madaraka wa kuzusha utawarudi kwani kila mnachosema kinakuwa ni UONGO...mwisho wa siku gazeti lenu litakosa soko na wanaowafadhili wataacha kuwapa pesa....
Escrow kuiadhiri CCM


  • Zitto asema ripoti yake haizuiliki
  • CAG kuanika madudu wiki hii
26/10/2014 | Na Abdallah Khamis |



HARAKATI za Chama cha Mapinduzi(CCM),kutaka ripoti ya uchunguzi wa akaunti ya Tegeta Escrow, isijadiliwe bungeni huenda zikagonga mwamba, Tanzania Daima Jumapili, limebaini
.

Jitihada hizo zinaweza kutoweka baada ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG), kukamilisha uchunguzi wake na anatarajia kuwasilisha ripoti hiyo kwa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali inayoongozwa na Zitto Kabwe.

Iwapo ripoti hiyo itawasilisha, inaweza kukipasua Chama Cha Mapinduzi (CCM) na serikali yake ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikituhumiwa kwa kulea na kulinda ufisadi
Tanzania Daima Jumapili, lilidokezwa kuwa CCM inahofia ripoti inaweza kuwagusa vigogo, mawaziri na watendaji wa serikali ambao itamlazimu Rais Jakaya Kikwete, kulivunja baraza la mawaziri.

Inaelezwa kwamba, ripoti hiyo huenda ikawagusa baadhi ya mawaziri waandamizi wa serikali na viongozi wa CCM miongoni mwao, ni wale walioanza harakati za kuwania urais katika uchaguzi ujao.
Kufikishwa bungeni kwa ripoti hiyo, kunatabiriwa litakuwa anguko jingine kwa serikali kama ilivyokuwa mwaka 2008 alipong'oka Waziri Mkuu Edward Lowassa kwa kashfa ya kutoa zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura kwa timu ya Richmond.


Kashfa hiyo ya Richmond ilitengeneza uhasama miongoni mwa makada wa CCM hata kukifanya chama hicho, kipoteza majimbo mengi katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.
Mbali na Richmond kukitesa CCM na serikali pia uhasama wa makada wake umekijengea makundi yanayotishia uhai wake.

Vigogo wa CCM na serikali yake hawataki ripoti hiyo iwasilishwe bungeni kwasababu itawaweka katika wakati mgumu wa kushinda uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika Disemba mwaka huu.
Katika kikao cha Halmashauri Kuu (NEC), ya CCM kilichokaa hivi karibuni mjini Dodoma suala hilo liiibuka ambapo Christopher ole Sendeka, anadaiwa kusimama katika kikao hicho na kueleza wazi kuwa chama chao kinachafuliwa na ufisadi wa IPTL na kwamba fedha hizo zinatumika Dodoma kwenye kampeni za urais.

Madai ya Sendeka, yalizimwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete, akisema kuwa suala la IPTL waliache kwanza maana wanasubiri ripoti ya uchunguzi unaoendelea hivi sasa.

Hata hivyo wakati hali ikionekana kuwa tete, Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge na hesabu za serikali (PAC), Zitto Kabwe,ameshamuandikia barua CAG, kumueleza umuhimu wa ripoti hiyo.
Zitto alisema suala hilo lazima litafika bungeni hata kama CCM hawataki jambo hilo lifike, kwa
sababu kamati yake ndiyo yenye jukumu la kufanyia kazi na kulipeleka huko.

Alisema CAG alitakiwa kutoa taarifa ya uchunguzi huo wiki iliyopita lakini aliomba apeleke taarifa wiki hii.
"Tukishakutana na CAG wiki hii, suala hili litajadiliwa kwenye vikao vya Bunge la 17 au 18, kulingana na mpangilio wa shughuli za Bunge, hili haliwezi kukwepeka"
"Sisi kazi yetu ni kulifikisha bungeni suala hili na wabunge wana uamuzi…hili la kuzuia sidhani kama litafanikiwa" alisema Zitto.
Zitto alibainisha kuwa Oktoba 24 mwaka huu, alimuandikia barua CAG akimueleza umuhimu wa ripoti hiyo kwa taifa.

Katika barua hiyo ambayo Tanzania Daima Jumapili, imefanikiwa kuiona Zitto anasema uchunguzi wa ripoti hiyo utaiokoa nchi na mpasuko unaoweza kujitokeza baada ya wafadhili wa serikali kuacha kutoa misaada kwa Tanzania mpaka ripoti ya Tegeta Escrow itakapowekwa hadharani.

Sehemu ya barua hiyo inasomeka "Kamati imejulishwa na wizara ya fedha na Benki Kuu kwamba uamuzi wa wafadhili kuzuia misaada ya kibajeti unaathiri sana utekelezaji wa bajeti,
Sharti la kutolewa misaada hiyo ni taarifa hii kutolewa kwa vyombo vilivyoomba, kuendelea kuchelewa kutoa taarifa kutaumiza zaidi wananchi kwa kukosa dawa hospitalini na hata mishahara kukosekana"iliandikwa.

Barua hiyo imeongeza kuwa gavana wa Benki Kuu ameijulisha kamati kuwa serikali imeanza kukopa katika soko la ndani na kuathiri uchumi kwa kushindwa na sekta na hivyo kuongeza riba na kusababisha uchumi wa nchi kusinyaa.

Mbali na Zitto, mbunge wa Kigoma Kusini,David Kafulila alisema ripoti hiyo isipowasilishwa bungeni atawasilisha hoja binafsi ya kutokuwa na imani na serikali.
Kafulila alisema anaamini ofisi ya CAG inakabiliwa na shinikizo kutoka kwa vigogo wakubwa serikalini wanaohusika na ufisadi huo.

Alisema uhakika wa jambo hilo unadhihirishwa na muda alioutumia CAG ni zaidi ya ule alioomba bungeni kwamba kazi hiyo ingekamilika baada ya siku 45 na kwamba mpaka jana ni zaidi ya siku 200 zimepita huku ripoti hiyo ikiwa imekaliwa.

"Nashangaa PCCB wamemaliza kazi na kwenda kuikabidhi Ikulu badala ya kumfikishia mwendesha mashtaka(DPP), ili aweze kuwachukulia hatua wahusika kwa kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria, Hosea anapaswa kuwasilisha ripoti yake bungeni kwa sababu aliagizwa na Bunge na siyo Ikulu"alisema Kafulila katika ujumbe mfupi wa simu kwa gazeti hili.

Sakata la Escrow liliibuliwa na Kafulila Mei 8 mwaka huu akiwa bungeni mjini Dodoma na kuwatuhumu baadhi ya vigogo wa serikali kuwa nyuma ya uchotwaji wa dola za marekani kiasi cha milioni 122 sawa na shilingi za kitanzania bilioni 200.

Vigogo waliotajwa na Kafulila ni Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospiter Muhongo na Katibu Mkuu wake, Eliakim Maswi, Waziri wa Fedha Saada Mkuya, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Beno Ndullu, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Frederick Werema na Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Mhandisi Felchesmi Mramba.

Kafulila alisema vigogo hao wamehusika na ufisadi wa fedha hizo zilizokuwa zimewekwa katika akaunti ya Baraza la Usuluhishi la Migogoro ya Kibiashara (ESCROW) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

CC: Tized, Mr Rocky, Fixed Point, Chakaza, Elly B, MziziMkavu, Power to the People, Jasusi, Eiyer, idawa, nguruvi, Mentor, Sikonge, Dingswayo, MANI, tpaul, Bramo, Bulesi Bulldog, Sangarara, MTAZAMO, Erythrocyte, Mag3, Mimibaba, zumbemkuu, Crashwise, amkawewe, Idimi, Ogah, Chakaza, mshana jr, JokaKuu, MWALLA, genekai, PRINCE CROWN, Tuko, Shark, lynxeffect22, samaki2011, MoudyBoka, adolay, Elli, nyabhingi, Janjaweed, S.N.Jilala, MEANDU, Tabby, Candid Scope, August, BONGOLALA, Gefu, Bigirita, Kozo Okamoto, Daudi Mchambuzi
 
Natarajia serekali kusukwa upya kwenye lala salama ya mkulu.
 
hata mimi nashangazwa na hili jambo, kwanini tushindwe kujiamulia mambo yetu wenyewe

Unaibiwa na watawala wako kwa kipindi kirefu hujitambui wala huchukui hatua utawezaje kujiamulia mambo yako mwenyewe? Taifa linafikia hadi hatua ya wananchi wake kukosa chakula na kuanza kula mizizi na sehemu nyingine wanakufa viongozi hawana habari hadi mataifa ya nje wayaone bado wakuache ujiamulie mambo yako mwenyewe? Ujue hizo fedha zinazotolewa na wahisani kujazia bajeti yenu ni fedha za walipa kodi wao na hawawezi kukaa kimya viongozi wenu wakigawana hela zao badala ya kuwahudumia wananchi. Unaanda bajeti ya matumizi kwa mategemeo ya hela za kuomba kwa wahisani bado unajigamba uachwe uamue upendavyo? Sasa wewe unao hata uwezo wa kuandika mabandiko jf na bado uelewa ni huu jee wapiga kura wanaosubiri vikapero na fulana wakoje? Kwa nini ccm isiendelee kutawala kwa miaka mingi ijayo?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
tuwashukuru sana wazungu kwa kuingilia kati jambo hili , vinginevyo tungepigwa bila huruma .

Hivi suala la rushwa kwenye nchi yako linahitaji maelekezo tka kwa wazungu???' Mkoroshokigoli
Nakumbuka wiki hii JK alisema 'Hivi unahitaji wazungu waje kukwambia uache kuua raia wako?'
 
Last edited by a moderator:
Siku hiyo ripoti ikiwekwa wazi watu watasema imechakachuliwa maana watu wanarukia tu hilo suala na ukweli hawaujui wanabaki kuamini kile wanachokifikiria wao.
 
Zitto forgot to mention the depreciation of the tzs. BoT have no reserves to intervene because simply they don't have any.

OUR CENTRAL BANK IS BANKRUPT!
 
Tanzania Daima Chadema daima Uzushi daima....ati harakati za CCM kuzuia...uzushi mwingine bwana wa kitoto kabisa...Bunge limemtaka CAG afanye ukaguzi na atoe ripoti sasa CCM wanaingiaje hapo?? huu ulafi wa madaraka wa kuzusha utawarudi kwani kila mnachosema kinakuwa ni UONGO...mwisho wa siku gazeti lenu litakosa soko na wanaowafadhili wataacha kuwapa pesa....

Mkuu kwanini huna uchungu na nchi yako au ni miongoni mwa mafisadi tunaowajadili hapa?
 
Tanzania Daima Chadema daima Uzushi daima....ati harakati za CCM kuzuia...uzushi mwingine bwana wa kitoto kabisa...Bunge limemtaka CAG afanye ukaguzi na atoe ripoti sasa CCM wanaingiaje hapo?? huu ulafi wa madaraka wa kuzusha utawarudi kwani kila mnachosema kinakuwa ni UONGO...mwisho wa siku gazeti lenu litakosa soko na wanaowafadhili wataacha kuwapa pesa....

Hivi ndugu yangu embu tueleze unanufaika na nini katika huu ufisadi wa ccm maana kila taarifa inayojitokeza juu ya ufisadi wa ccm wewe unatetea badilika bwana kuwa mzalendo hata kama wewe ni mfuasi wa ccm.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom