Je, Ni uhaba wa wataalam au ndiyo mazoea ya kupenda vya bure na rushwa!!
Tembelea website na blog za Bongo, ziwe za serikali, mashirika makubwa au za watu binafsi utashuhudia mwenyewe ninachokieleza hapa. Page hazina mpangilio (page alignment and inconsistency), hazivutii (matumizi mabaya ya typography, rangi na picha), vigumu kupata unachokitafuta (usability issues), maelezo yasiyoeleweka (no useful content and lack of clarity) na mengine mengi.
Mfano mzuri ni website ya serikali iliyokupewa msukumo mkubwa na rais wa Marekani Barak Obama iitwayo www.opengov.go.tz. Madhumuni yake yalikuwa kuwashirikisha wananchi katika masuala na shughuli za serikali ili kuhamasisha uwazi (promote transparency). Kama hilo ndio lengo lake, si lazima uwe na degree kufahamu kwamba pamoja na mambo mengine kinachohitajika kwenye website kama hii ni maelezo sahihi (useful content); user interaction kama emails na forms; na muonekano (look) ambavyo vitamshawishi mwananchi kushiriki (encourage public engagement). Kinachonishangaza ni upungufu wa ubora wa website hii kwa vitu basic kabisa ambavyo hata mwanafunzi (junior web developer) angeweza kufanya.
Orodha ya mifano ya website zisizo na ubora ni ndefu ila ona hizi chache ambazo ungetegemea ziwe angalau afadhali.
Nao wapenda kublog wameongezeka hivyo kumekuwa na ongezeko kubwa la blog na hali hii haioneshi dalili ya kupungua. Hata hivyo ubora wa blog hizo ni wa kutisha. Kwa lugha rahisi kabisa ni kwamba ‘zimelipuliwa' hakuna ujuzi. Wanablog wengi wanatumia free google hosting (yaani .blogspot). Elements zimebandikwa kila upande kwenye page hivyo msomaji anabaki ku-guess wapi pa kwenda. Nyingine hata maandishi hayaonekani.
Hivi majuzi tu nikiwa kwenye jamii forum kuna msomaji mmoja alikuwa anauliza wasomaji wengine ni wapi anapoweza kupata .com domain ya bure. Mwingine anaulizia internet ya bure. Ni swala la kushangaza kuona jinsi tunavyoitaka teknolojia bure bila kujali ubora.
Katika kulichambua swala hili nimeona kuna sababu kuu zifuatatzo:
Binafsi nakubaliana kwamba hali ya mtanzania wa kawaida ni ngumu si ajabu ubora wa vitu ni mdogo. Hata hivyo iweje hata makampuni na serikalini bado hakuna ubora? Tatizo ni kwamba tumejenga mazoea ya kupenda vya bure na kutokujali ndiyo sababu inayopelekea hata tunapopata nafasi za uongozi iwe serikalini au kampuni binafsi bado tunajikuta kuchagua urahisi (cheap) na kusahau ubora (sacrifice quality)!
Swala la rushwa na ubinafsi linachukua nafasi kubwa. Katika uchunguzi wangu nilishtuka kusikia kiasi kilichotumika kutengeneza website ya kampuni moja kulinganisha na ubora wa website hiyo. Ni dhahiri kwamba bajeti iliyoidhinishwa haikutumika ipasavyo. Aidha kampuni ililipa bei ya juu kwa mtu au kampuni iliyotengeneza website hiyo au kuna mtu kabakiza chenji.
Kuhusu swala la upungufu wa wataalamu bado sikubaliani nalo. Japokuwa tuko nyuma, kuna vijana wengi wa kitanzania wenye ujuzi na wanaoweza kufanya kazi nzuri. Tuchukulie mfano mzuri wa ‘michuzi' blog iliyopata mafanikio makubwa. Mmiliki wa blog hii japokuwa anatumia free google service, ni dhahiri anatumia wataalamu wa tecknolojia kumtengenezea blog inayopendeza na kukidhi matakwa ya mtumiaji wakati yeye akitumia muda wake kuweka bidii kwenye fani yake ya ‘uandishi na upigaji picha' (yaani content). Sio ajabu kwanini anafanikiwa sana.
Mifano mingine ni hizi website zifuatazo ambazo naamini zimetengenezwa na watanzania:
Ukweli ni kwamba kuna matatizo ya kiuchumi, cultural na hata uongozi mbaya katika ngazi mbalimbali. Ukichukulia kwamba dunia ya sasa ni ya Internet, matatizo haya yanarudisha nyuma mafanikio ya nchi. Kwa kuwa hakuna physical contact kati ya msomaji na mwandishi, website ni kama kioo cha mwandishi. Hakuna mtu mwenye akili zake anayeweza kuamini kazi yako au kukuchukulia serious kama website yako imelipuliwa.
Kila mtu ana ujuzi wake. Ni unprofessional kutaka kufanya kila kitu peke yako. Wakati mwingine inabidi kutoa kidogo ili upate zaidi. Si lazima ulipe mamilion, kuna watu wenye ujuzi watakaokufanyia kazi nzuri kwa bei nafuu..shop around utawapata.
Mwisho ni kwa wajuzi na wataalam wa teknolojia. Kumbukeni teknolojia inabadilika kila siku hivyo tuna kila sababu ya kuendelea kujifunza mambo mapya constantly. Baadhi ya software tools nzuri kuzijua kwa maswala ya internet ni:
For Developers: PHP, Javascript, Wordpress, Joomla, CSS, ajax, JQuery, etc.
For Designers: Graphics - Photoshop, Gimp, etc.
goody@goodytechnology.co.uk
Tembelea website na blog za Bongo, ziwe za serikali, mashirika makubwa au za watu binafsi utashuhudia mwenyewe ninachokieleza hapa. Page hazina mpangilio (page alignment and inconsistency), hazivutii (matumizi mabaya ya typography, rangi na picha), vigumu kupata unachokitafuta (usability issues), maelezo yasiyoeleweka (no useful content and lack of clarity) na mengine mengi.
Mfano mzuri ni website ya serikali iliyokupewa msukumo mkubwa na rais wa Marekani Barak Obama iitwayo www.opengov.go.tz. Madhumuni yake yalikuwa kuwashirikisha wananchi katika masuala na shughuli za serikali ili kuhamasisha uwazi (promote transparency). Kama hilo ndio lengo lake, si lazima uwe na degree kufahamu kwamba pamoja na mambo mengine kinachohitajika kwenye website kama hii ni maelezo sahihi (useful content); user interaction kama emails na forms; na muonekano (look) ambavyo vitamshawishi mwananchi kushiriki (encourage public engagement). Kinachonishangaza ni upungufu wa ubora wa website hii kwa vitu basic kabisa ambavyo hata mwanafunzi (junior web developer) angeweza kufanya.
Orodha ya mifano ya website zisizo na ubora ni ndefu ila ona hizi chache ambazo ungetegemea ziwe angalau afadhali.
- Tanzania Revenue http://www.tra.go.tz/;
- Chadema http://www.chadema.or.tz;
- University Commission TCU Website
Nao wapenda kublog wameongezeka hivyo kumekuwa na ongezeko kubwa la blog na hali hii haioneshi dalili ya kupungua. Hata hivyo ubora wa blog hizo ni wa kutisha. Kwa lugha rahisi kabisa ni kwamba ‘zimelipuliwa' hakuna ujuzi. Wanablog wengi wanatumia free google hosting (yaani .blogspot). Elements zimebandikwa kila upande kwenye page hivyo msomaji anabaki ku-guess wapi pa kwenda. Nyingine hata maandishi hayaonekani.
Hivi majuzi tu nikiwa kwenye jamii forum kuna msomaji mmoja alikuwa anauliza wasomaji wengine ni wapi anapoweza kupata .com domain ya bure. Mwingine anaulizia internet ya bure. Ni swala la kushangaza kuona jinsi tunavyoitaka teknolojia bure bila kujali ubora.
Katika kulichambua swala hili nimeona kuna sababu kuu zifuatatzo:
- hali ngumu ya kimaisha;
- (2) kupenda vya bure;
- (3) rushwa; na
- (4) upungufu wa wataalam.
Binafsi nakubaliana kwamba hali ya mtanzania wa kawaida ni ngumu si ajabu ubora wa vitu ni mdogo. Hata hivyo iweje hata makampuni na serikalini bado hakuna ubora? Tatizo ni kwamba tumejenga mazoea ya kupenda vya bure na kutokujali ndiyo sababu inayopelekea hata tunapopata nafasi za uongozi iwe serikalini au kampuni binafsi bado tunajikuta kuchagua urahisi (cheap) na kusahau ubora (sacrifice quality)!
Swala la rushwa na ubinafsi linachukua nafasi kubwa. Katika uchunguzi wangu nilishtuka kusikia kiasi kilichotumika kutengeneza website ya kampuni moja kulinganisha na ubora wa website hiyo. Ni dhahiri kwamba bajeti iliyoidhinishwa haikutumika ipasavyo. Aidha kampuni ililipa bei ya juu kwa mtu au kampuni iliyotengeneza website hiyo au kuna mtu kabakiza chenji.
Kuhusu swala la upungufu wa wataalamu bado sikubaliani nalo. Japokuwa tuko nyuma, kuna vijana wengi wa kitanzania wenye ujuzi na wanaoweza kufanya kazi nzuri. Tuchukulie mfano mzuri wa ‘michuzi' blog iliyopata mafanikio makubwa. Mmiliki wa blog hii japokuwa anatumia free google service, ni dhahiri anatumia wataalamu wa tecknolojia kumtengenezea blog inayopendeza na kukidhi matakwa ya mtumiaji wakati yeye akitumia muda wake kuweka bidii kwenye fani yake ya ‘uandishi na upigaji picha' (yaani content). Sio ajabu kwanini anafanikiwa sana.
Mifano mingine ni hizi website zifuatazo ambazo naamini zimetengenezwa na watanzania:
- Bunge Parliament of Tanzania;
- Michuzi blog MICHUZI;
- Vavavuum blog VaVaVuum | Kwa Watanzania Wote;
- Tanzania UNDP UNDP in Tanzania - Home;
Ukweli ni kwamba kuna matatizo ya kiuchumi, cultural na hata uongozi mbaya katika ngazi mbalimbali. Ukichukulia kwamba dunia ya sasa ni ya Internet, matatizo haya yanarudisha nyuma mafanikio ya nchi. Kwa kuwa hakuna physical contact kati ya msomaji na mwandishi, website ni kama kioo cha mwandishi. Hakuna mtu mwenye akili zake anayeweza kuamini kazi yako au kukuchukulia serious kama website yako imelipuliwa.
Kila mtu ana ujuzi wake. Ni unprofessional kutaka kufanya kila kitu peke yako. Wakati mwingine inabidi kutoa kidogo ili upate zaidi. Si lazima ulipe mamilion, kuna watu wenye ujuzi watakaokufanyia kazi nzuri kwa bei nafuu..shop around utawapata.
Mwisho ni kwa wajuzi na wataalam wa teknolojia. Kumbukeni teknolojia inabadilika kila siku hivyo tuna kila sababu ya kuendelea kujifunza mambo mapya constantly. Baadhi ya software tools nzuri kuzijua kwa maswala ya internet ni:
For Developers: PHP, Javascript, Wordpress, Joomla, CSS, ajax, JQuery, etc.
For Designers: Graphics - Photoshop, Gimp, etc.
goody@goodytechnology.co.uk