Enziiii za Mwalimu


asante mkuu kwa kutukumbusha yote maana tumepata story za kutuvunja mbavu.nimekugongea thanks
 
Nimevaa chachacha, na sokdi ndefu kidogo, mfuko wa rambo ndo wa kubebea madaftari ndani.
Ilikuwa kuweka Andazi kwemye mfuko wa kaptula kitu rahisi sana hujiulizi!!
Siku ya kufunga shule ile Ijumaa unahakikisha umeficha kiboko chako mkitawanyika namchapa fimbo kama 3 za haraka haraka mbaya wangu hasa monitors na siku hiyo nilikuwa mahakikisha nimekaa nao karibu kabisa!!!
 
Reactions: ram
chachacha walikua wanaita ma batatanga halafu vikaja viatu kama mokasin hv ila vilikua vya plastiki waliita utanikoma saa nane jua likiwa kali vinakua vya moto sana pia unazikumbuka kaptura za marudufu?ilikua kama khaki hv enzi hizo waziri mkuu sokoine
 

tehe tehe tehe izo chacha ikifika mida ya jua kali weeee
 
Na ole wako usahau dada yake Juma anaitwa nani (Roza) kwenye Kiswahili kwenye vitabu vile 'Tujifunze Lugha Yetu' Kwenye English lazima ujue Mr & Mrs. Daud na watoto wao Musa na Neema wanaosoma Mtakuja Primary School. Those were the good old days!!!!
 
Reactions: ram
Kwenye Jiografia ilikuwa lazima usome:-
  • Wafanyakazi wa Tanzania drs la nne (mfano kilimo cha pamba Maswa, Kilimo cha Muhogo Newala)
  • Wafanyakazi wa Africa drs la 5 (mfano kilimo cha kakao Ghana, Kilimo cha Karanga Gambia)
  • Wafanyakazi wa Ulimwengu drs la 6 (nakumbuka ufungaji wa ng'ombe wa maziwa Denmark)
  • Wafanyakazi wa africa mashariki drs la 7
Jamani Kawambwa na Mulugo wanashindwa tu hata ku copy na ku paste hiyo mitaala ya zamani???

 
Reactions: ram

Ongezea kulima shamba la shule na utamaduni!

Siku moja moja Mazingaombwe na Kisamama!
 
Yoooote waseme CHIPUKIZI sikuwahi kucheza lakini ilinitesa sana kisaikolojia!

Niliwaza hivi siku nikichaguliwa kucheza na vile viboko itakuwaje?
 
Enzi hizo viatu ni raba za DH,au viatu fulani vya plastiti toka KENYA ukivipaka mafuta ya kula vinang'aa mbaya ila balaa lake ikifika saa sita mchana lazima uvivue coz vilikuwa vinachoma sana.

Mengine yalikuwa ni haya:
-Mfukoni lazima ubebe mahindi ya kukaanga au maembe
-Usipowahi Number asubuhi imekula kwako
-Utoro ilikuwa ni issue ya kawaida kutokana na walimu kuwa wakali sana
-ukiwa time keeper ulikuwa unaonekana wa matawi
 
Reactions: ram
Nimecheka sana, nakumbuka halaiki, shamba la shule mkichoka sana wakati wa kupanda basi wale madarasa ya juu wanachimba shimo kubwa wanamwaga mbolea na mbegu mahindi kiroba nzima mwl akija mnaondoka mmemaliza! Kasheshe kupalia msipowahi kuyafukia ayaone...fimbo zinatembea shambani uko uko. Bendi ya shule ikiongoza parade na ukaguzi jumatatu... Twilumba schoolbag ilikuwa ya jinja unaishonea kaua kwa mbele🙂. Hakukuwa na ripot ila kufunga shule mnatajiwa wa kwanza hadi wa mwisho...mitumba ikiitwa kafa ulaya na kudharauliwa sana japo nzuri... tulikuwa tukivaa nguo zetu za jinja au khanga toka Mwatex. Kwaya na mpira ilikuwa juu sana shule yetu enzi za Abraham Thawe ilikuwa inashinda kila leo. I miss those old good days
 
Na ole wako usahau dada yake Juma anaitwa nani (Roza) kwenye Kiswahili kwenye vitabu vile 'Tujifunze Lugha Yetu' Kwenye English lazima ujue Mr & Mrs. Daud na watoto wao Musa na Neema wanaosoma Mtakuja Primary School. Those were the good old days!!!!

Ntale uko sahihi kabisa zile story za juma na Roza zilikuwa the best, nakumbuka story za mtakuja primary school na maweni primary school. Wakati huo kila shule ina store ya kuhifadhia madawati na yalikwepo kibao nashangaa ni kwa nini baada ya mwinyi kukamata hatamu shule zikafilisika. Nilikuwa najitahidi kuwahi shule hata nifanyeje namkuta mchizi flani keshafika kafagia na amekoka moto anaota hahaha sumbawanga hiyo 32 yrs ago!
 
Yoooote waseme CHIPUKIZI sikuwahi kucheza lakini ilinitesa sana kisaikolojia!

Niliwaza hivi siku nikichaguliwa kucheza na vile viboko itakuwaje?

Aisee mpaka leo siipendi na sitaki kusikia chipukizi nilipewa magwanda yenye chawa nikayatupa barabarani nikalala mbele hawakuniona tena!
 

Vipi jtano siku ya usafi viboko vilivyokuwa vinatembea! Hapo asubuhi umekuja na dumu la kuchotea maji na ufagio wako. Time keeper mara nyingi utamkuta mdada msaaafi ndo anapewa kazi hiyo na achelewi bwana
 
Je mmewahi kuficha mdundo wa ngoma kubwa.au kutembea nai ili watu wasiuwahi wakapiga ngoma.
 
Unakumbuka tobo bao?ilikuwa noma ukipigwa tobo,lazima ukimbie ukashike mti mliokubaliana kushikwa ili kuepuka kipigo.
 

Wewe utakuwa wa enzi za Mwinyi, siyo Enzi za Mwalimu.
 

Hahahaa, shamba la shule!..hivi sku hizi hakuna hizi habari na EK?
 
Hahahaa, shamba la shule!..hivi sku hizi hakuna hizi habari na EK?

mashamba ya shule ilikuwa ni maalumu kufundishia elimu ya kujitegemea, hata hivyo hayakudumu kwenye miaka ya 80 hivi yalikuwa hamna na zilibaki bustani tu pembezoni mwa shule. Shule za kulipia mfano za Mission kama Nyakahoja hawakuwa nayo haya vibustani vidogo tu. Lakini kikubwa elimu wakati ule ilikuwa nzuri ya kumfanya mtu ajiamini
 

Ukweli kabisa Mama Joe nakumbuka shuleni kwetu walifundisha mpaka ufundi, useremala, kutengeneza vigae vya kuezekea, na waliofanya vizuri walizawadiwa zana za kufanyia kazi!..SIPATI PICHA LEO TUNGEKUWA WAPI KAMA TUNGEKUWA NA MFUMO MZURI WA ELIMU!
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…