Engine oil gani ni nzuri kwa Gari aina ya IST?

Yes...kwa ist si vizuri kutumia hiyo oil...hiyo ni nzito sana
Mkuu nashukuru sana kwa maelezo mazuri. Mimi gari yangu ni Subaru Impreza cc1500. Wakati gari imekuja service ya awali kabla sijaitumia ilitumika Castro oil 20w50. Kwa kuzingatia maoni ya wadau humu ni kuwa sio oil sahihi. Je, nibadilishe nitumie 5w30 au niendelee na hiyo 20w50?
 
Angalizo wakuu kama gari yako ishaejda makilomita mengi na ushaweka sana oil zetu zile mineral oil SAE 40 ,20W 50W angalia sana ukihamia kwny hzi full synthetic na nyepesi kama 5W 30 oil inaeza vuja mana zinapenya penya sana coz ni nyepesi...

So utapo hamia huko kwny hizo nyepesi uwe makini kucheki level kama mkweche wako ushavuka kilomita laki moja other wise baki tu huko kwny hzo nzito nzito
 
Mkuu nashukuru sana kwa maelezo mazuri. Mimi gari yangu ni Subaru Impreza cc1500. Wakati gari imekuja service ya awali kabla sijaitumia ilitumika Castro oil 20w50. Kwa kuzingatia maoni ya wadau humu ni kuwa sio oil sahihi. Je, nibadilishe nitumie 5w30 au niendelee na hiyo 20w50?
Mkuu bado hujachelewa..nakushauri shift from 20w50 to 5w30 au 10w30 haraka iwezekanavyo....
Hizi oil zenye namba kubwa kama sae 40 na hizo 50 ni nzuri zaidi kwa high mileage engines na heavy duty vehicles kama madala dala, canter, fuso..

Hizi gari zetu ndogo za petrol inapendekezwa zaidi oil ambazo ni multi grade na viscosity yake iwe 30 at optimum operating temperature..

Go for 5w 30/ 10 w 30 mkuu....unaweza kutumia hiyo hiyo Castrol, total au kampuni nyingine yoyote inayoaminika..
 
Mkuu bado hujacelewa..nakushauri shift from 20w50 to 5w30 au 10w30 haraka iwezekanavyo....
Hizi oil zwnye namba kubwa kama sae 40 na hizo 50 ni nzuri zaidi kwa high mileage engines na heavy duty vehicle kama madala dala, canter, fuso..

Hizi gari zetu ndogo za petrol inapendwkezwa zaidi oil ambazo ni multi grade na viscosity yake iwe 30 at optimum operating temperature..

Go for 5w 30/ 10 w 30 mkuu....unaweza kutumia hiyo hiyo Castrol, total au kampuni nyingine yoyote inayoaminika..
Asante sana. Nitazingatia ushauri wako.
 
Wadau nina ist ya 2006, juzi niliipiga sehemu radiator ikapinda ikagusa fan na kuzuia fan kuzunguka... Kulikopelekea motor kuungua.

Baada ya motor kuungua fan ikashndwa kuzunguka na mashine ikaanza kuheat.

Shida yangu ni kuwa nishaweka motor zingine kama 2 hivi na bado injini inaheat kwa kilometer chache tu hata 30 hazifiki na maji yanaisha kabisa.

Nb.
Rejeta haivuji, sasa hapa solution ipo vipi.
Je kuna aina ya moto special kwa hizi gari, au fan special,. Na ni wapi naweza nikaipata na kwa gharama gani maaana nateseka saana na nina safari. Ya kwenda bukoba week ijayo.
 
Wadau nina ist ya 2006, juzi niliipiga sehemu radiator ikapinda ikagusa fan na kuzuia fan kuzunguka... Kulikopelekea motor kuungua.

Baada ya motor kuungua fan ikashndwa kuzunguka na mashine ikaanza kuheat.

Shida yangu ni kuwa nishaweka motor zingine kama 2 hivi na bado injini inaheat kwa kilometer chache tu hata 30 hazifiki na maji yanaisha kabisa.

Nb.
Rejeta haivuji, sasa hapa solution ipo vipi.
Je kuna aina ya moto special kwa hizi gari, au fan special,. Na ni wapi naweza nikaipata na kwa gharama gani maaana nateseka saana na nina safari. Ya kwenda bukoba week ijayo.

blades za mota uliyoweka na uliyotoa zinalingana?
vipi mzunguko wa motor upo sawa ? kuna motor zinazunguka anti clockwise, kuna zingine clockwise , hizi zinatofautiana kufunga na kama fundi alikosea hilo matokeo yake ni kuchemsha , gari ikiwa sationary inachemsha pia?
 
Hizi namba kila moja ina tafsiri yake.
Unapokuta mfano 5W 30. Namba ya kwanza kabla ya W inawakilisha uzito wa oil. Kadri namba inavyozidi kuwa ndogo, ndivyo oil inavyozidi kuwa thin hivyo kuwezesha better performance at the cold start.

W simply inawakilisha winter wengine wanasema Weight wengine wanasema Watt...lakini inawakilisha Winter..

30 inawakilisha viscosity ( ile hali ya oil kuwa kama ina nata nata fulani hivi.)
Hii ina maana kwamba injini inpopata joto lake la juu ambalo linatakiwa ili ifanye kazi vizuri, viscosity ya oil hii bado itabaki katika kipimo hicho cha 30 ambacho kimewekwa na watengenezaji, hali kadhalika kwa oil namba 40 au 50

Kwa mantic hii oil 5w 30 ni nyepesi kuliko 10w 30.

Oil hizi zenye namba mbili yaani 5w 30 kwa lugha nyingine zinaitwa multi grade oils....ni oil ambayo imetengenezwa kufanya kazi katika mazingira ya baridi sana na joto sana.

Lakini hizi SAE 40 za kawaida ni mono garde....hizi ni maalumu kwa mazingira ya joto tu...na ndiyo maana kwa siai tulioko huku Arusha ikifika lile baridi la mwezi wa saba, kama gari ni ndogo na umeweka SAE 40, ukiliwasha asubuhi utasikia injini inavuma sana kwa muda mrefu...injini ikishafikia joto kiasi fulani ndiyo unaona inatulia...wakati unasubiri injini ipate moto, unakuwa unasaga vyuma..

Ukifuatilia zamani nchi zenye baridi kama huko Ulaya, walikuwa na oil za aina mbili..nzito kwa ajili ya msimj wa joto na nyepesi kwa ajili ya msimu wa baridi....watu walilazimika kumwaga oil msimu wa bari na kuweka oil nyepesi ya kukabiliana na baridi...hali kadhalika msimu wa joto, walimwaga oil nyepesi na kuweka nzito.

Kuepuka purikushani hizo, ndiyo Society of Automobiles Engineers (SAE) wakaja na oil ambayo ni mult grade mfano 5w30, 10w 30,10w40 n.k....oil hii ukishaiweka haichagui baridi wala joto wewe ni kuangalia tu muda wa service ukifika unaimwaga.

Hatari ya SAE 40 kwa garo dogo, haijalishi unaishi Dar au Arusha.... ukiwasha gari asubuhi wakati injini imepoa, oil hii kitaalam huchelewa kufika sehemu za juu za injini kutokana na uzito wake...pale inapichelewa, vyuma vinaendelea kusagana na unaendelea kuua injini yako taratibu...

SAE 40 ukitumia kwa magari makuu kuu sana haina shida...mfano madaladala au gari ambalo mileage imeenda juu sana pengine zaidi ya 180000km..
kuna oil wanasema inafaa kwa gari ambayo imeenda sana kilometer, je kati ya 5W30 na 10W30 ipi inafaa kwa iliyoenda kilometer nyingi? na je vipi kuhusu 5W40 ni bora kuliko hizo mbili hapo juu?
 
blades za mota uliyoweka na uliyotoa zinalingana?
vipi mzunguko wa motor upo sawa ? kuna motor zinazunguka anti clockwise, kuna zingine clockwise , hizi zinatofautiana kufunga na kama fundi alikosea hilo matokeo yake ni kuchemsha , gari ikiwa sationary inachemsha pia?
Duh kweli inahitaji ufundi.... Nisaidie utundu wa kugundua izo blades pamoja na iyo anti clockwise
 
blades za mota uliyoweka na uliyotoa zinalingana?
vipi mzunguko wa motor upo sawa ? kuna motor zinazunguka anti clockwise, kuna zingine clockwise , hizi zinatofautiana kufunga na kama fundi alikosea hilo matokeo yake ni kuchemsha , gari ikiwa sationary inachemsha pia?
Kingine mwambie kuweka maji kwenye Radiator sio sawa. Siku hizi tuna coolants
 
Wadau nina ist ya 2006, juzi niliipiga sehemu radiator ikapinda ikagusa fan na kuzuia fan kuzunguka... Kulikopelekea motor kuungua.

Baada ya motor kuungua fan ikashndwa kuzunguka na mashine ikaanza kuheat.

Shida yangu ni kuwa nishaweka motor zingine kama 2 hivi na bado injini inaheat kwa kilometer chache tu hata 30 hazifiki na maji yanaisha kabisa.

Nb.
Rejeta haivuji, sasa hapa solution ipo vipi.
Je kuna aina ya moto special kwa hizi gari, au fan special,. Na ni wapi naweza nikaipata na kwa gharama gani maaana nateseka saana na nina safari. Ya kwenda bukoba week ijayo.
Ni dm nikuelekeze mbinu
 
Naomba kuuliza kidogo, ikiwa gar ina km laki 2 zen nikabadili injin na kuweka nyingine, bado maswala ya kilometa kwenye matumiz ya oil yana husika tenaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
Ukibadilisha engine hapo ni sawa na umerudisha nyuma milage number ya gari sababu umeipa engine nyingine... So unatakiwa hata total milage pale ureset.... ianze upya.
 
kuna oil wanasema inafaa kwa gari ambayo imeenda sana kilometer, je kati ya 5W30 na 10W30 ipi inafaa kwa iliyoenda kilometer nyingi? na je vipi kuhusu 5W40 ni bora kuliko hizo mbili hapo juu?
Kama gari limeshaenda km nyingi sana mathalani zaidi ya 150k, 5w40 au 10w40 ndiyo pahala pake
 
blades za mota uliyoweka na uliyotoa zinalingana?
vipi mzunguko wa motor upo sawa ? kuna motor zinazunguka anti clockwise, kuna zingine clockwise , hizi zinatofautiana kufunga na kama fundi alikosea hilo matokeo yake ni kuchemsha , gari ikiwa sationary inachemsha pia?
Aisee nimeenda kwa fundi karekebisha kitu kidgo saana sasa sijuh km itahiti au raha..

Anadai feni ilikuwa inapuliza nnje kwemye rejeta badala ya kuvuta ndani... Kuna switch kachomoa akachomoa kitu ndani ya switch akageuza switch akarudishia basi..

Hapa ndio nipo natest ntaleta mrejesho
 
Aisee nimeenda kwa fundi karekebisha kitu kidgo saana sasa sijuh km itahiti au raha..

Anadai feni ilikuwa inapuliza nnje kwemye rejeta badala ya kuvuta ndani... Kuna switch kachomoa akachomoa kitu ndani ya switch akageuza switch akarudishia basi..

Hapa ndio nipo natest ntaleta mrejesho
yap
ndio nilichomaanisha , nilikuuliza kama gari ikiwa stationary ina heat, hukurespond.
kwa kawaida kama blades zinapuliza nje gari ikiwa starionary tatizo la kuchemsha halijioneshi maana kunakuwa hakuna air resistance, ila ukianza kutembea hewa ya nje inapuliza ndani na feni inapuliza nje , hapo kunakuwa hakuna air movement, na gari inachemsha kirahisi kabisa
 
Aisee nimeenda kwa fundi karekebisha kitu kidgo saana sasa sijuh km itahiti au raha..

Anadai feni ilikuwa inapuliza nnje kwemye rejeta badala ya kuvuta ndani... Kuna switch kachomoa akachomoa kitu ndani ya switch akageuza switch akarudishia basi..

Hapa ndio nipo natest ntaleta mrejesho
Hawa mafundi wa uchochoroni hawa wanabalaa kweli kweli.
 
Back
Top Bottom