Geza Ulole
JF-Expert Member
- Oct 31, 2009
- 59,203
- 79,433
Ndugu wana-JF imefika wakati jukwaa hili la fikra nyerevu kujiuliza kama inafikia hatua Mh Rais anaona hamna umuhimu wa kufuta kazi jamaa zake wabadhirifu kwa kisingizio eti cha kusema serikali haipaswi kushinikizwa, je sisi tuliochoka na tunaoumia na ubadhirifu ulikidhiri wa serikali yake, tufanye nini? Kama Rais aliyepewa ridhaa na sisi na akatusi imani yetu kwa kutoangalia tunavyoteseka na ubadhirifu wa mawaziri wake, je hatuna aja ya kuitisha kura ya kutokuwa na imani nae? Je hatuna haja ya kuingia mitaani kushurutisha atoke madarakani? Ee Mungu saidia ujasiri wa Watanzania katika kipindi hiki kigumu cha serikali isiyo sikivu na ya kutumia mabavu kulindana na tuonyeshe njia bora ya kudai haki! Hii nchi ni yetu sote!