sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,033
Siwezi kuongea kwa niaba ya watu wenye asili ya africa wote wanaopenda hip hop, wawe wabongo, wamarekani weusi, waingereza , n.k, lakini wacha nitoe maoni yangu, Eminem is the goat (great of all time),
bigie na 2pac walikuwa hot lakini nadiriki kusema vifo vyao vilikuwa vikubwa mno kuliko muziki wao, ni kama Neymar na Mbappe wangetutoka mapema, hakika majina yao yangekuzwa mno kuliko walipo kwa sasa, Watu wangekua wanaamini Neymar na mbappe ndio wangekuwa wanastahili Ballon Dor kila mwaka. Kuijua stable longetivity ya msanii ni kitu muhimu sana,
Kwangu mimi hali ni tofauti, huwa sijali rangi, nachojali ni lyrics, delivery, word play, kucheza na speed, pumzi, nk, na hapa ndipo napojua hakuna msanii wa kumfikia eminem kukitendea miujiza kipaza sauti na kutumia kalamu vizuri kuandaa lyrics amazing.
Sote tunajua hip hop ilitengenezwa na kuchochewa na watu weusi, na hapa ndipo kuna baadhi ya watu wenye hii asili wanakuwa wagumu mno kukubali uhalisia kwamba Eminem ni mzungu na anafanya poa zaidi ya rappers weusi, hisia zinatumika kupinga badala ya kutumia akili kukubali ukweli.
Laiti Eminem angekuwa ni mweusi, basi ni wazi kabisa eminem angechukua ni Michael Jackson wa Hip hop
Pia ukija huku kwenye mitindo huru frreestyles na cyphers, eminem yuko vizuri.
Waliowahi kuingia 18 zake wengi walipotezwa, pengine cheo sahihi cha kumpa Eminem ni "Un-beefwithable"
Nimeweka videos za mnyama anakamua live hapa, karibu kuzicheki