Magulumangu
JF-Expert Member
- Jan 7, 2010
- 3,047
- 452
Katika Pitapita zangu nimekuta watu wakibishana, ebwana eee acha embe la kibada Kiboko mtu wangu, mmoja akadakia hilo cha mtoto wewe nenda Kahama huko embe la kujidondokea mwanangu ukionja huachi, mwingine kasema hiiiiiiiiiiii Hamjaenda Ntwara nyie kula kila aina ya embe dodo, embe sindano na kibao, Kaja jamaa mwingine huyu alionekana Shomile, nyiye nendeni Bukoba maembe dodo ya kumwaga....swali je, wewe unapenda embe gani? Lile la Kibada(Karibu na Mjini), La Kahama chapa ng'ombe, Kwa Nshomile wazee wa Katerero au huko Ntwara Kumnyima Ntu dhambi?