Sera mpya ya elimu inayotarajiwa kuanza kutumika muda wowote kuanzia sasa pale matayarisho yatakapokamilika, pamoja na mambo mengine inatarajiwa kupunguza muda wa kusoma elimu ya msingi kutoka miaka 7 ya sasa hadi miaka 6.
Kwa mujibu wa Naibu waziri wa TAMISEMI Joseph Kakunda, sera hiyo iliyozinduliwa na Rais Kikwete mwaka 2014 itaanza kutekelezwa hapa nchini mara baada ya maandalizi ya utekelezaji wake kukamilika. Chini ya sera hiyo mfumo mpya wa elimu utakuwa 1+6+4+2+3+ yani mwaka mmoja wa chekechea, miaka sita shule ya msingi, miaka minne sekondari (0-level), miaka miwili sekondari (A-level), na miaka mitatu au zaidi ya elimu ya juu, badala ya mfumo wa sasa wa 1+7+4+2+3+.
[HASHTAG]#Mytake[/HASHTAG]:
Naipongeza serikali kwa sera hii mpya ya elimu. Ukweli ni kwamba maika 7 ilikuwa mingi sana kwa elimu ya msingi. Inafika mahali mnaanza kurudiarudia tu mambo yaleyale. Mimi nilipokuwa darasa la 5 nilikuwa najaribu kufanya mitihani ya darasa la 7 na ninafaulu. So naamini tukiwawezesha vizuri watoto wetu na kuweka mikakati bora ya elimu miaka 6 inawatosha kabisa.
Suala la msingi tuboreshe maslahi ya walimu na tuwalipe stahiki zao zote ili wawe na moyo wa ufundishaji, then tuboreshe miundombinu ya kujifunzia ikiwa ni pamoja na madarasa, na tuhakikishe mtaala wa elimu unaandaliwa vizuri katikia namna itakayomfanya mwanafunzi amalize darasa la sita akiwa na uelewa wa mambo anuai.
Wingi wa miaka sio tija sana. Leo tuna watoto wanasoma miaka 7 na bado wanaenda sekondari hawajui kusoma wala kuandika. Unajiuliza wamefaulu vipi. So jibu hapa ni kwamba bado miundombinu ya elimu, maslahi ya walimu na mtaala wa elimu havijaboreshwa. Mtoto wa namna hii hata akikaa darasani miaka 10 bado hawezi kubadilika.
Sera hii mpya ya elimu itasaidia kupunguza muda wa kukaa shuleni na hivyo kuwawezesha vijana kufikia ndoto zao mapema.
Nchi nyingi zilizoendelea wamerahisisha mfumo wa elimu. Kwa muda mfupi unakuta mtu ameshahitimu masomo yake. Unakutana na kijana ana miaka 19 tayari ni graduate, ana degree yake moja. Wakati hapa bongo miaka 19 jitu liko form 3 au form 2. Hapo bado hujafeli form 4 uanze kupiga mark time za kureseat. Yani hadi unakuja kupata degree na mvi zimeota.
Kwa hiyo naipongeza sana serikali na naitaka ikamilishe maandalizi haraka ili sera hiyo ianze mapema iwezekanavyo.!