Elimu ya msingi kuwa miaka 6?

Elimu ya msingi kuwa miaka 6?

ragin

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2015
Posts
7,391
Reaction score
9,378
Habarini humu ndani na heri ya mwaka mpya. Ni muda sana sijazurula humu JF,
moja kwa moja niende kwenye mada husika.

Iko hivi nimepata taarifa kuwa elimu ya msingi imekuwa ni miaka 6 kuanzia wanafunzi walioko darasa la 3 mwaka huu. Pia waliopo darasa la nne mwaka huu wao watamalizia miaka 7.

Swali; Je! Ni kweli imeshapangwa hivyo au nilikuwa napotezwa? Kama wameshapanga hivyo ina maana mitaala ya elimu ipo mbioni kubadilishwa au? Je ule mtihani wa darasa la nne wataufanya wakiwa darasa gani au ndo hilohilo?.

Ni hayo tu nisiwachoshe!.
 
habarini humu ndani na heri ya mwaka mpya.
ni mda sana sijazurula humu jf,
moja kwa moja niende kwenye mada husika.
iko hivi nimepata taarifa kuwa elimu ya msingi imekuwa ni miaka 6 kuanzia wanafunzi walioko darasa la 3 mwaka huu. pia waliopo darasa la nne mwaka huu wao watamalizia miaka 7.
swali; je! ni kweli imeshapangwa ivo au nilikuwa napotezwa?
kama wameshapanga ivo ina maana mitaala ya elimu ipo mbioni kubadilishwa au?
je ule mtihani wa darasa la nne wataufanya wakiwa darasa gani au ndo hilohilo?.

ni hayo tu nisiwachoshe!.
Kwanza ondoa neno KUZURULA. Kama ulimaanisha KUZURURA, pia hapa JF sio mahala pa wazururaji. Ebo!
 
Elimu ya tanzania hatuelew wap tuna ipeleka mi najiuliza maswali meng inamana walio soma elimu iyo zaman walikua wanaikosea ama ni vp mana kila leo uta skia grade zimepanda mara zimeshuka asa sielewi ni inakua vp elimu yetuu
 
darasa la nne la zamani, darasa la saba la sasa.... na darasa la sita lijalo... una weza ongeza madarasa mengine... kabla hauja anza kusema wapi tume kosea ni lazima kuwa na kumbu kumbu ya elimu ilipo toka na changamoto zake na uhitaji wa sasa kuzingatia hasa mabadiliko ya sayansi na technology....

ila kama una zoea kubwabwaja huwezi yaona haya... kenya wame angaika sana katika elimu mpaka kufikia hatua ya kupata suluhu... na sasa wana piga hatua...

Pia una weza shangaa kwanini Lugha ya Kizungu isiwe kama somo katika mabadiliko hayo ya madarasa... kama darasa la chekechea mpaka la sita/saba ni kiswahili na kizungu ni somo sio lugha ya kufundishia... nina imani pia tuna weza kutumia lugha yetu kufundishia mpaka vyuo vikuu, kama nchi zingine wafanyavyo... nazani pia tuna weza kuwa taifa la historia na mfano barani africa... kwa mageuzi haya ktk mfumo wetu wa elimu

tukiondoa vitisho na hofu toka kwa wachache...
 
Upuuzi mtupu,,, badala ya kubadilisha lugha ya kufundishia iwe kingereza,,,,mnahangaika na kubadilisha MITAALA YA MADARASA,,,, itasaidia nn
 
Tatizo kila kitu ni siasa, elimu pia ishaharibiwa na wanasiasa wanakurupa na mambo mengi
 
darasa la nne la zamani, darasa la saba la sasa.
hiyo elimu ya zamani ambayo inasemekana ilikuwa bora wakati mwingine ni stori tu kama za kwenye kahawa. kama ilikuwa bora mbona hatujaona matokeo yake kwa maendeleo ya nchi? Maana Tanzania haijawahi kuwa bora kiuchumi huko nyuma kuliko ilivyo hivi sasa. sasa tunajenga barabara za kutosha kwa kiwango cha lami, tunanunua ndege, tunajenga vyuo vikuu n.k
 
hiyo elimu ya zamani ambayo inasemekana ilikuwa bora wakati mwingine ni stori tu kama za kwenye kahawa. kama ilikuwa bora mbona hatujaona matokeo yake kwa maendeleo ya nchi? Maana Tanzania haijawahi kuwa bora kiuchumi huko nyuma kuliko ilivyo hivi sasa. sasa tunajenga barabara za kutosha kwa kiwango cha lami, tunanunua ndege, tunajenga vyuo vikuu n.k
Hao viongoz karibia wote si elimu ya Zamani wanaosimamia Hizo agenda.
 
Hao viongoz karibia wote si elimu ya Zamani wanaosimamia Hizo agenda.
Zamani ipi. Zamani ni kuanzia lini kwenda wapi? maana haya yote yanayooneka sasa yanatekelezwa na waliosomea mfumo huu wa elimu ya sasa. Hizo darasa la nne nilikoma miaka mingi sana na waliosomea elimu hiyo kwenye mfumo ni wachache sasa. ni kwara tu wa kuwatisha vijana wa leo kuwa elimu ya zamani ilikuwa bora wakati hamna lolote. Ni sawasawa na kusema kupitia JKT ndo kuwa na uzalendo wakati Mafisadi wote na wezi wa mali za uuma walipitia JKT na walilewlewa enzi za Mwalimu.
 
nawashukuruni kwa michango ila bado sijapata uhakika wa km ni kweli tutakuwa na miaka 6 y elimu ya msingi..
 
Nimeptia Sera ya Elimu ya mwaka 2014 sijaona hilo. isipokuwa Sera imeelekeza mtoto kusoma Elimu ya awali (chekechea) mwaka moja akiwa katika ya miaka 3 na 5 na mtoto anaruhusiwa kuanza darasa la kwanza akiwa na miaka 4 kulingana na uwezo wa mtoto. hata hivyo suala la kuwa na maiak 6 au 7 haliwezi kuathiri chochote. Cha msingi ni kuwa na mazingira wezaeshi ya kufundishia na kujifunzia kuanzia elimu ya msingi hadi Sekondari.
 
Nimeptia Sera ya Elimu ya mwaka 2014 sijaona hilo. isipokuwa Sera imeelekeza mtoto kusoma Elimu ya awali (chekechea) mwaka moja akiwa katika ya miaka 3 na 5 na mtoto anaruhusiwa kuanza darasa la kwanza akiwa na miaka 4 kulingana na uwezo wa mtoto. hata hivyo suala la kuwa na maiak 6 au 7 haliwezi kuathiri chochote. Cha msingi ni kuwa na mazingira wezaeshi ya kufundishia na kujifunzia kuanzia elimu ya msingi hadi Sekondari.
bado hujanielewa mkuu maana yangu kuu ni kwamba hawa walio darasa la tatu wao wataishia darasa la sita ndio mwisho na sio la saba km tulivozoea.

swali ;; je ni kweli imepitishwa au ni data za watu.?
 
Ndugu yangu, ni kweli kwamba wanasema Elimu ya msingi itakuwa kuanzia darasa la kwanza hadi la sita. Wanadai kwamba baada ya kufika darasa la sita wanafunzi hao wataendelea na masomo mpaka darasa la 10.
Mbaya zaidi ni kwamba inasemekana mpaka sasa hata baadhi ya vitabu vya darasa la tatu bado havipo, wakati huo huo vitabu vya darasa la nne havipo kabisa hata alama ikizingatiwa kuwa shule zimefungua tangu January 8,2018.
Kama ndivyo, maana yake ni kwamba darasa la nne wa mwaka huu 2018 watafanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2020 ikiwa ni pamoja na darasa la tano wa mwaka huu 2018 ambao nao pia watafanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2020.
Yote mema, lakini je, yamefanyika maandalizi ya kutosha ilk kukidhi haja ya wanafunzi hao, yaani watahiniwa wa mwaka 2020 katika mitaala miwili tofauti?
Tusubiri tuone nini kitatokea.
 
Back
Top Bottom