Elimu ya Fedha

Elimu ya Fedha

Kaaya10

Member
Joined
Dec 11, 2017
Posts
37
Reaction score
53
Habari wana Jamii forum,

Mimi ni Mwalimu Wa Elimu ya Fedha.

Nna uzoefu Wa kufundisha na kufanya kazi Bank zaidi ya miaka 6

Naandika business proposal kwa ajili Biashara

Nashauri Biashara masuala ya Fedha na Hususani Mikopo.

Nitaandaa somo LA Elimu ya fedha hapa

Mada zitakua ni:-

Bajeti
Akiba
Utawala Wa mikopo

Zote zitakusaidia uwe na Uhuru Wa kifedha.
 
Habari wana Jamii forum,

Mimi ni Mwalimu Wa Elimu ya Fedha.

Nna uzoefu Wa kufundisha na kufanya kazi Bank zaidi ya miaka 6

Naandika business proposal kwa ajili ya Biashara

Nashauri Biashara masuala ya Fedha na Hususani Mikopo.


Nitaandaa somo LA Elimu ya fedha hapa

Mada zitakua ni:-

Bajeti
Akiba
Utawala Wa mikopo

Zote zitakusaidia uwe na Uhuru Wa kifedha.

Nitafute kwa Huduma hizo
 
Kama kipata change ni laki mbili kwa mwezi, natakiwa ni save bei gani?

Nitumie njia gani kuongeza kipato, while am employed
 
Kama kipata change ni laki mbili kwa mwezi, natakiwa ni save bei gani?

Nitumie njia gani kuongeza kipato, while am employed
Kiasi cha kuweka akiba hakipo constant ila hakikisha unaweka akiba, standard ya akiba ni 20% ambayo ndo formula inatumiwa na mfuko ya hifadhi ya jamii. Pia ukiwa kazini angalia kitu gani unauwezo Wa kufanya na hujaanza kukifanya ukifanye kikuingizie pesa mfano part time sehemu nyingine au kuanzisha Biashara etc
 
Kama kipata change ni laki mbili kwa mwezi, natakiwa ni save bei gani?

Nitumie njia gani kuongeza kipato, while am employed
Pia kuweka akiba vizuri weka lengo mfano lengo ni kununua pikipiki au kufungua Biashara 2M, then gawanya muda ambao ukifika Unataka uwe na hiyo Biashara mfano miezi 5 maana yake 2M/5 unapata 400k kila mwezi sasa hakikisha kila mwezi unaweka hiyo
 
Habari wana Jamii forum,

Mimi ni Mwalimu Wa Elimu ya Fedha.

Nna uzoefu Wa kufundisha na kufanya kazi Bank zaidi ya miaka 6

Naandika business proposal kwa ajili Biashara

Nashauri Biashara masuala ya Fedha na Hususani Mikopo.

Nitaandaa somo LA Elimu ya fedha hapa

Mada zitakua ni:-

Bajeti
Akiba
Utawala Wa mikopo

Zote zitakusaidia uwe na Uhuru Wa kifedha.
Karibu ukaribie mkuu ulonayo utuelimishe.
 
Pia kuweka akiba vizuri weka lengo mfano lengo ni kununua pikipiki au kufungua Biashara 2M, then gawanya muda ambao ukifika Unataka uwe na hiyo Biashara mfano miezi 5 maana yake 2M/5 unapata 400k kila mwezi sasa hakikisha kila mwezi unaweka hiyo
Nimekuelewa vizuri..
 
 Bajeti ni mpango unaogawanya mapato kwenye matumizi mbalimbali

 Ni mpango unaoonyesha mchanganuo wa mapato na matumizi kwa ajili ya jambo au mambo yanayotarajiwa kufanywa.

 Ni muhtasari wa makadirio ya mapato na jinsi yatakavyotumika ndani ya muda ulioweka.

 Vile vile bajeti ni matarajio au makisio ya mapato na matumizi

UMUHIMU WA BAJETI

 Inarahisisha kufanya maamuzi ya namna ya kufanya matumizi na kuweka akiba

 Inasaidia kuwa na matumizi ya tahadhari kufuatana na mapato

 Inasaidia kuwa na nidhamu ya kujiwekea akiba.

 Kama ikizingatiwa, inasaidia kufikia malengo ya kifedha mtu aliyojiweka

 Inasaidia kuwa na usimamizi mzuri wa fedha

MUUNDO WA BAJETI

Bajeti ina sehemu kuu mbili nazo ni;-

i. Mapato

Hapa unahorodhesha mapato yako yote ambayo unategemea kupata katika kipindi husika, mfano, mshahara, kusuka, kufua nguo, kuuza nguo n.k baada ya hapo unapata jumla ya mapato sehemu ya kwanza

ii. Matumizi

Hapa pia unaweka jinsi utakavyo tumia mapato yako hapo juu mfano, nauli, chakula, vocha, unapata jumla, baada ya jumla lazima uweke kipengele cha AKIBA

Jambo ya mwisho ni unachukua mapato unatoa matumizi kujua kama una ziada au pungufu.

BAJETI YA NYUMBANI NA BIASHARA

 Bajeti ya nyumbani ni mpango unaoonyesha mchanganuo wa mapato na matumizi muhimu kwa ajili ya shughuli au mambo ya nyumbani

 Bajeti ya biashara ni ile ambayo inahusu shughuli mbalimbali zinazohusiana na mapato na matumizi muhimu yaliyoelekezwa kwenye biashara husika.

UMUHIMU WA KUTENGANISHA BAJETI YA NYUMBANI NA BIASHARA

 Kujua mapato halisi yatokanayo na biashara na kuweza kuainisha matumizi yake

 Kujua matumizi halisi ya nyumbani na kuweza kuyatofautisha na ya biashara


HITAJI LA LAZIMA NA HITAJI LISILO LA LAZIMA

HITAJI LA LAZIMA ni kile kitu ambacho ukikosa huwezi kuishi mfano chakula, nyumba

HITAJI LISILOLAZIMA ni kile kitu ambacho ukikosa utaendelea na maisha kawaida mfano vilevi, starehe

Mahitaji kua lazima au sio lazima inategemea mtu na mtu mfano kuna mtu kulingana na shughuli zake gari ni hitai la lazima na mtu mwingine sio lazima.

KALENDA YA MSIMU

 Kalenda ya misimu ni dhana ambayo inasaidia kuonyesha mapato na matumizi kwa kuendana na miezi AU msimu fulani

 Inasaidia kuonyesha mapato ya kila mwezi na namna matumizi yanavyokuwa.

 Vile vile huonyesha uhalisia wa vyanzo mbali mbali vya matumizi

 Huonesha miezi ambayo kuna uzidio wa kipato au uzidio wa matumizi

 Husaidia mtu kujipanga kujua miezi ambayo kipato ni kidogo ataishi vipi kwa kuweka akiba miezi yenye kipato kikubwa.
 
Kuna watu Wana matumizi ya fujo sana ila Cha ajabu dili za hela haziwakauki
Wanajua kutafuta ila wanashida kwenye kuweka akiba, haina faida pesa wanayopata ni sawa na kujaza gunia Maji Japo kwa muda huo anaonekana kavunja
 
Nawezaje kumaintain hali ya uchumi pale nilipo,nisianguke na pia vile vile nawezaje kuifanya hela inifanyie kazi automaticaly hata kama sipo eneo husika la mazingira ya kazi?
 
Back
Top Bottom