Elimu ya Fedha

Elimu ya Fedha

Nawezaje kumaintain hali ya uchumi pale nilipo,nisianguke na pia vile vile nawezaje kuifanya hela inifanyie kazi automaticaly hata kama sipo eneo husika la mazingira ya kazi?
Kumaintain hali ya Uchumi hakikisha uzalishaji wako haupungui ila unaongezeka, ukibak na uzalishaji au kipato kilekile overtime Utaona kama umeshuka kwa 7bu thamani ya fedha inashuka na hivyo Utaona huwezi timiza mahitaji yako kama hapo kabla pia mahitaji yanaongezeka kila uchao hivyo kipato kipato kinatakiwa kiongezeke.

Ili pesa ikufanyie kazi lazima uwe na mfumo Wa Biashara ambao umeweka watu unasimamia tu au wekeza kwenye makampuni ambayo wewe sio mtendaji Wa kila siku kwa kununua hisa.


Ukitaka kujua Unahitaji mapato kiasi Gani ili uwe huru kifedha andika matumizi yako halisi ya sasa Kisha andika mapato hapo kwenye budget tafuta tofauti. Kisha andika mahitaji yako halisi Kisha chukua mahitaji halisi toa kipato Utaona huo utofauti.


Kujua namna ya kutoka hapo fuatilia baada ya somo LA Elimu ya Fedha litakuja somo LA Uhuru Wa kifedha ambalo ni mwendelezo Wa Elimu ya Fedha...


Kaa hapa hapa.

Karibu
 
Kumaintain hali ya Uchumi hakikisha uzalishaji wako haupungui ila unaongezeka, ukibak na uzalishaji au kipato kilekile overtime Utaona kama umeshuka kwa 7bu thamani ya fedha inashuka na hivyo Utaona huwezi timiza mahitaji yako kama hapo kabla pia mahitaji yanaongezeka kila uchao hivyo kipato kipato kinatakiwa kiongezeke.

Ili pesa ikufanyie kazi lazima uwe na mfumo Wa Biashara ambao umeweka watu unasimamia tu au wekeza kwenye makampuni ambayo wewe sio mtendaji Wa kila siku kwa kununua hisa.


Ukitaka kujua Unahitaji mapato kiasi Gani ili uwe huru kifedha andika matumizi yako halisi ya sasa Kisha andika mapato hapo kwenye budget tafuta tofauti. Kisha andika mahitaji yako halisi Kisha chukua mahitaji halisi toa kipato Utaona huo utofauti.


Kujua namna ya kutoka hapo fuatilia baada ya somo LA Elimu ya Fedha litakuja somo LA Uhuru Wa kifedha ambalo ni mwendelezo Wa Elimu ya Fedha...


Kaa hapa hapa.

Karibu
Hakika sichezi mbali najiona kwa mbali kabisa future billionaire.
 
MAANA YA AKIBA

 Ni kiasi cha fedha au kitu kinachowekwa kwa ajili ya matumizi ya baadae. Matumizi haya ya baadae ni muhimu yawe na malengo ambayo mtu anahitaji kuyafikia baada ya muda fulani.
 Muda huu unaweza kuwa mrefu au mfupi kulingana na hitaji/lengo lenyewe.
 Vile vile akiba ni muhimu kwa usimamizi mzuri wa fedha ambayo husaidia katika kukabiliana na dharura, kuwekeza mali na kufikia malengo ya kifedha.

UMUHIMU WA KUWEKA AKIBA

 Inasaidia kukuza biashara pamoja na kupunguza madeni
 Kuchukua fursa na kufanya uwekezaji katika mali au biashara na kufikia malengo yetu ya kifedha ya muda mrefu au mfupi.
 Hutusaidia kutenga kiasi cha fedha ili kitusaidie katika matukio mbalimbali katika maisha kama vile kujifungua, ndoa na kifo.
 Husaidia kutatua changamoto wakati wa dharura

CHANGAMOTO KATIKA UWEKAJI WA AKIBA

Katika kuweka akiba, kuna changamoto mbali mbali ambazo huwa zinajitokeza. Baadhi ya changamoto hizo ni pamoja na:

 Kutokuwa na kipato cha uhakika
 Kutokuwa na pesa za ziada
 Kutumia pesa kwenye mambo yasiyo ya lazima
 Kutokuwa na sehemu salama ya kuhifadhia pesa
 Kuwa na madeni mengi
 Kushindwa kupangilia uwekaji wa akiba

MALENGO: MUDA MFUPI NA MUDA MREFU

Lengo la muda mfupi ni lengo linalohitaji muda mfupi au miezi michache ili kulitimiza. Lengo hili linaweza kuwa ni kuanzia miezi sita na si zaidi ya miezi 12 (mwaka mmoja)

Lengo la muda mrefu ni lengo ambalo linahitaji mwaka au zaidi ili kutimia. Hii ni ndoto kubwa ambayo itatimia hapo mbeleni.

MPANGO WA KUWEKA AKIBA

Maswali ya kujiuliza katika kufadhili lengo/malengo yako

 Lengo lako ni nini?
 Ni kiasi gani cha fedha unahitaji kutimiza lengo lako?
 Ni wiki ngapi unahitaji kuweka akiba ya pesa kwa ajili ya lengo lako?
 Ni kiasi gani cha fedha utakuwa unaweka kila wiki?

MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA KUWEKA MPANGO WA AKIBA

 Lengo lenyewe
 Gharama ya lengo (kiasi cha fedha kinachohitajika)
 Muda wa kutimiza lengo (wiki, miezi au miaka)

 Kiasi cha pesa kitakachokuwa kinawekwa kila siku/wiki/mwezi

 Mpangilio wa malengo kulingana na umuhimu wake

MPANGO WA AKIBA

LENGO = GHARAMA YA LENGO GAWANYA KWA MUDA WA KUTIMIZA HILO LENGO

Mfano
lengo ni kuanzisha biashara ya juisi baada ya miezi mitano.

GHARAMA 250,000
MUDA miezi mitano

Mpango kwa kila mwezi ni 250,000/5 = 50,000 hivyo unahitajika kutenga 50,000 kila mwezi ili uweze kufikia lengo la kuanzisha biashara ya juisi baada ya miezi mitano

Endelea kujifunza Hapa hapa
King Rabbit AbouZakariya Political stability Kuna somo jipya hapa
 
MAANA YA MKOPO

  • Mkopo* ni fedha ambayo taasisi za fedha au za mikopo zinatoa kwa wateja wake ili kukidhi mahitaji ya msingi/mtaji na kwa ajili ya kuboresha biashara.
  • Pia ni fedha ambayo mkopaji anaweza kuitumia katika kipindi cha muda mfupi au ndani ya kipindi cha muda fulani, ambapo atatakiwa kufanya marejesho kulingana na riba au gharama waliyokubaliana na mkopeshaji.
  • Fedha hii ni mkopo wa amana na hisa za wateja katika kutoa huduma ya fedha.
  • Kwa hiyo mkopo una gharama zake kupitia riba na gharama za uandaaji.
  • Mkopo si mali ya benki bali ni mali ya wateja wa benki ambapo benki inasimamia fedha za wateja na kuwa mdhamini kwa wateja wanaoomba mikopo.
  • Mkopeshaji anaweza kuwa: Benki, Taasisi za Mikopo au mtu binafsi
  • Riba ni gharama inayolipwa unapotumia pesa ya mkopo

SABABU ZA KUCHUKUA MKOPO

Sababu za kuchukua mkopo ni pamoja na:

1. Kuutumia katika uwekezaji
2. Kushughulikia/kutatua mambo ya dharura
3. Kwa ajili ya kugharamia matumizi ya nyumbani

 Mkopo kwa ajili ya uwekezaji utaleta faida ambayo mkopaji ataitumia kama rejesho la mkopo
 Lakini mkopo wa matukio yasiyotarajiwa na ule wa matumizi ya nyumbani hauwezi kuleta faida, lazima ulipwe kwa chanzo kingine cha mapato

VYANZO VYA MIKOPO

Rafiki, Familia, Taasisi za Mikopo, Benki, Vyama vya Kuweka na Kukopa, k.m SACCOs na VICOBA


MASWALI YA KUJIULIZA KABLA YA KUCHUKUA MKOPO

1. Ratiba ya marejesho ya mkopo ikoje? (kwa wiki au kwa mwezi)
2. Ni kiasi gani nitakua nalipa kama rejesho?
3. Jumla ya marejesho yote ni kiasi gani ikijumuisha na riba?
4. Muda wakupata mkopo. Itanichukua muda gani kupata mkopo?
5. Ni vyanzo gani vya mapato na akiba nitakavyotumia kulipia mkopo?
6. Kama unakopa kwa ajili ya kununua kitu au kifaa: Pindi utakapomaliza mkopo kifaa hicho kitaendelea kutumika kukuletea pesa?
7. Ninahitaji kuweka dhamana ya mkopo? Kama ni ndio, ni ipi?
8. Ni yapi matokeo ya mimi kutolipa mkopo?

MKOPO MZURI NA MKOPO MBAYA

Mkopo mzuri ni mkopo ambao unamsaidia mkopaji kuboresha hali yake ya sasa na kumwezesha kufanya marejesho.

Mkopo mbaya ni mkopo ambao una faida ndogo kulinganisha na gharama, na kupelekea mkopaji kushindwa kulipa.

Maswali Muhimu Kuhusu Mkopo

1. Ni kiasi gani cha fedha zangu mwenye natakiwa kutumia?
2. Nahitaji kiasi gani cha mkopo?
3. Je, mkopo utanisaidia nini ambacho bila kuuchukua nisingekipata?

FAIDA ZA KUKOPA

i. Kupata pesa Zaidi ya zile ulizojiwekea (AKIBA)
ii. Kupata pesa nyingi Zaidi na kwa haraka pale unapopatwa na shida ya ghafla au muda unapokua mdogo katika uwekezaji
iii. Kutatua matatizo yanayojitokeza kwa ghafla

Ni Kipi Kitatokea Endapo Sitalipa Deni Langu?

I. Kutokua na amani muda wote
II. Kupoteza heshima yako
III. Itapelekea kupoteza mali zako, zitauzwa ili kufidia mkopo
IV. Kukosa Imani katika mikopo: hakuna ambaye atakukopesha tena.

Utawala Wa mikopo ni Muhimu sana, usikope kila siku na kila mahali.

Kwa ushauri Wa Masuala Fedha na Mikopo, uandishi Wa proposal ni WhatsApp 0769160382
 
Mbali na kuajiriwa benki ulishawahi kufanya biashsmara gani wewe kama wewe na kufanikisha ikakuwa? Wengine tunamwamini mtu aliyeshawahi kuanzisha na kuikuza biashara, wengi walioajiriwa ni blaablaa nyingi ambazo zinakuonyesha upande mmoja wa Faida tu, changamoto hakuambii
 
Back
Top Bottom