Shark
JF-Expert Member
- Jan 25, 2010
- 29,459
- 29,156
Nimeichukua mahali, Inaweza kukusaidia,
Ushawahi kuwaza kwanini kuna watu maisha yetu daily yanakua yanasukumwa na Mikopo? Ni kwa sababu tunakopa kununua vitu ambavyo baada ya muda wa mkopo na vyenyewe vinakua vimeisha au vimekaribia kuisha thamani. Mfano mzuri ni mkopo wa gari.
Kuna watu tupo radhi kukatwa 248,500/= kwa mwezi kwa muda wa miaka mitano kwa riba ya 18% kwa ajili ya kulipia mkopo wa 10m tuliotumia kununua vits lakini hatupo tayari Kufanya saving ya walau 220,000/= kwa mwezi kwa muda wa miaka mitano ili tuje nunua gari kwa cash yetu.
Sisemi tusinunue hapana maana kila mtu ana mahitaji yake na malengo yake.
Hata kama baada ya miaka 5 gharama ya gari itakua imepanda, bado kwa 220,000/= utakua umeweza kuhifadhi 13.2m ambayo inatosha kabisa kununua gari kwa kipindi hicho, au unaweza ukakuta bei zimeshuka kama sasa.
Najua wengi tutakimbilia kwenye Time Value for money, ila ukweli ni kwamba wengi wetu hatujipangi ni nini tunataka katika muda fulani bali tunakurupuka kutokana na hitaji la mhemuko la mda huo.
Mtu anaamka tu anasema kachoka shida ya usafiri na joto anataka push miguu minne, akichungulia kwenye akaunt salio halitoshi anajaza form chaap anachukua mkopo ili aanze pishana na wenzake sheli. Achana na hizi gharama za mafuta, service na parking tutaziongelea siku ingine.
Wakati unafanya saving ya miaka mitano ili ununue gari unaweza amua kuwekeza hela zako hata kwenye UTT - Vipande ambavyo kila siku vinapanda thamani na baada ya miaka mitano ukajikuta una hela nzuri tu. Miaka mitano ya kumaliza kulipa mkopo unakuta na Vits yenyewe imeshachoka, unajikuta na mshahara kidogo umepanda na unahitaji gari jingine, unajitwika mkopo Mwingine mkubwa kidogo, unaagiza gari ya juu na maisha yanaendelea.
Kwenye mikopo uchawi wake ni riba na miaka ya kulipa tu, ukichemka kufanya maamuzi kwenye haya utasotea mkopo ujute. Ndo mana makonda n madereva wa daladala ukiwachomekea tu utaskia toa gari lako la mkopo cz wanajua wengi hatuwezi afford kununua cash mpaka tuboost na mkopo.
By Albert Man Dea
Instagram & Twitter: @elimu_biashara
Ushawahi kuwaza kwanini kuna watu maisha yetu daily yanakua yanasukumwa na Mikopo? Ni kwa sababu tunakopa kununua vitu ambavyo baada ya muda wa mkopo na vyenyewe vinakua vimeisha au vimekaribia kuisha thamani. Mfano mzuri ni mkopo wa gari.
Kuna watu tupo radhi kukatwa 248,500/= kwa mwezi kwa muda wa miaka mitano kwa riba ya 18% kwa ajili ya kulipia mkopo wa 10m tuliotumia kununua vits lakini hatupo tayari Kufanya saving ya walau 220,000/= kwa mwezi kwa muda wa miaka mitano ili tuje nunua gari kwa cash yetu.
Sisemi tusinunue hapana maana kila mtu ana mahitaji yake na malengo yake.
Hata kama baada ya miaka 5 gharama ya gari itakua imepanda, bado kwa 220,000/= utakua umeweza kuhifadhi 13.2m ambayo inatosha kabisa kununua gari kwa kipindi hicho, au unaweza ukakuta bei zimeshuka kama sasa.
Najua wengi tutakimbilia kwenye Time Value for money, ila ukweli ni kwamba wengi wetu hatujipangi ni nini tunataka katika muda fulani bali tunakurupuka kutokana na hitaji la mhemuko la mda huo.
Mtu anaamka tu anasema kachoka shida ya usafiri na joto anataka push miguu minne, akichungulia kwenye akaunt salio halitoshi anajaza form chaap anachukua mkopo ili aanze pishana na wenzake sheli. Achana na hizi gharama za mafuta, service na parking tutaziongelea siku ingine.
Wakati unafanya saving ya miaka mitano ili ununue gari unaweza amua kuwekeza hela zako hata kwenye UTT - Vipande ambavyo kila siku vinapanda thamani na baada ya miaka mitano ukajikuta una hela nzuri tu. Miaka mitano ya kumaliza kulipa mkopo unakuta na Vits yenyewe imeshachoka, unajikuta na mshahara kidogo umepanda na unahitaji gari jingine, unajitwika mkopo Mwingine mkubwa kidogo, unaagiza gari ya juu na maisha yanaendelea.
Kwenye mikopo uchawi wake ni riba na miaka ya kulipa tu, ukichemka kufanya maamuzi kwenye haya utasotea mkopo ujute. Ndo mana makonda n madereva wa daladala ukiwachomekea tu utaskia toa gari lako la mkopo cz wanajua wengi hatuwezi afford kununua cash mpaka tuboost na mkopo.
By Albert Man Dea
Instagram & Twitter: @elimu_biashara