Elewa kwamba pamoja na katazo, kuna bidhaa nyingi tu bado zitafungwa au tutaendelea kuzipata katika mifuko ya plastiki kama hizi hapa

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Nimeshangaa jinsi watu wanavyolichukulia katazo la mifuko ya plastiki Watu wengi kwa kupotoka na kupotosha wanadhani hakutakuwa na hata kitu kimoja kitakachofungwa kwenye mifuko ya plastic. Hiyo sio maana yake, na mtu asikudanganye kuja nyumbani kwako eti anakagua kama una mifuko ya plastic akakuta kuna "packaging" za plastiki akakujia juu au kukudai kitu kidogo.

Katazo la mifuko ya plastiki linahusu hasa maduka (supermarkets)au huduma zinazofungasha vitu unavyonunua katika mifuko ya plastiki, na sio kwa kila kitu

Hizi hapa chini ni baadhi ya bidhaa zitakazoendelea kuwa katika mifuko ya plastiki. Unaweza kuongeza.
  1. Taulo za kike (pedi)
  2. Mabunda ya toilet paper
  3. Six pack za bia
  4. Baadhi ya sabuni
  5. Mifuko ya bidhaa maji inayotolewa na maduka ya duty free ya airport
  6. Karanga za kupakiwa kiwandani
  7. Chips zilizokwisha kufungwa supermarket
  8. Mboga mboga kama njegele au karoti zilizokwisha kufungwa supermarket
  9. Ice unazonunua supermarket
  10. Mito ya kununua dukani
  11. Magodoro ya dukani
  12. Mafiji au TV toka dukani
  13. Pipi
  14. Packet za korosha au karanga za kukaanga
  15. Shati au nguo nyingine za dukani
  16. Bidhaa za courier kama DHL
  17. Mifuko ya dry cleaner
  18. Mikate, maandazi nk ya supermarket au confectionery
  19. Sukari
  20. Chumvi
  21. Nk
 
Kwa mujibu wa wataalamu wa afya na Wizara ya Mazingira hii mifuko ya plastiki sio mizuri kwa kuifadhia chakula ambacho kinaenda kuliwa..Wana JF naomba kuuliza hii mikate,maandazi na keki bila kusahau maziwa fresh na mtindi n.k hivi vyakula vinakuwa vipo salama ndani ya mifuko ya plastiki?na kama havipo salama kesho viondolewe sokoni...
 
Kwa mujibu wa wataalamu wa afya na Wizara ya Mazingira hii mifuko ya plastiki sio mizuri kwa kuifadhia chakula ambacho kinaenda kuliwa..Wana JF naomba kuuliza hii mikate,maandazi na keki bila kusahau maziwa fresh na mtindi n.k hivi vyakula vinakuwa vipo salama ndani ya mifuko ya plastiki?na kama havipo salama kesho viondolewe sokoni...
Google uone europe wanafanyaje maana wao wanajali sana environment. We do not have to invent the wheel!
 
Nafikiria karanga zetu za kitaa, ubuyu, mabarafu, sabuni za unga za kupima nk
 
Nimeshangaa jinsi watu wanavyolichukulia katazo la mifuko ya plastiki Watu wengi kwa kupotoka na kupotosha wanadhani hakutakuwa na hata kitu kimoja kitakachofungwa kwenye mifuko ya plastic. Hiyo sio maana yake, na mtu asikudanganye kuja nyumbani kwako eti anakagua kama una mifuko ya plastic akakuta kuna "packaging" za plastiki akakujia juu au kukudai kitu kidogo.

Katazo la mifuko ya plastiki linahusu hasa maduka (supermarkets)au huduma zinazofungasha vitu unavyonunua katika mifuko ya plastiki, na sio kwa kila kitu

Hizi hapa chini ni baadhi ya bidhaa zitakazoendelea kuwa katika mifuko ya plastiki. Unaweza kuongeza.
  1. Taulo za kike (pedi)
  2. Mabunda ya toilet paper
  3. Six pack za bia
  4. Baadhi ya sabuni
  5. Mifuko ya bidhaa maji inayotolewa na maduka ya duty free ya airport
  6. Karanga za kupakiwa kiwandani
  7. Chips zilizokwisha kufungwa supermarket
  8. Mboga mboga kama njegele au karoti zilizokwisha kufungwa supermarket
  9. Ice unazonunua supermarket
  10. Mito ya kununua dukani
  11. Magodoro ya dukani
  12. Mafiji au TV toka dukani
  13. Pipi
  14. Packet za korosha au karanga za kukaanga
  15. Shati au nguo nyingine za dukani
  16. Bidhaa za courier kama DHL
  17. Mifuko ya dry cleaner
  18. Mikate, maandazi nk ya supermarket au confectionery
  19. Sukari
  20. Chumvi
  21. Nk
Ningependa kujua chakula kilichopikwa kukiifadhi kwenye mifuko ya plastiki hakuna madhara?na hapo naona omeorodhesha vinavyo patikana supermarket je kwa huku mtaani vipi waendelee kutumia vifungashio kwa bidhaa ulizotaja?
 
Back
Top Bottom