Electronic Passport hupatikana kwa muda gani?

Electronic Passport hupatikana kwa muda gani?

Qj_

Senior Member
Joined
Feb 16, 2017
Posts
157
Reaction score
155
Kwa hapa Mwanza nikifanya process za hii Electronic Passport nitaipata baada ya mda gani. Passport inahitajika kabla ya terehe 3 mwezi wa 11.
images%20(8).jpg
 
Wadau njooni mnipe information hapa. Kama kuna mtu alishawahi fanyia Mwanza process ya passport hua inachukua mda gani kutoka?
 
Una cheti cha kuzaliwa, kitambulisho cha taifa, cheti cha kuzaliwa au affidavit ya mzazi wako? Kama ndio utaipata kabla ya muda huo.
 
Yeah nina kilakitu
 
Kama una kitambulisho cha Taifa nadhani process haita kuwa refu wengi wamefeli kupata kwa kutokuwa na vitambulisho vya Taifa
 
Kama una viambatanisho vyote ni Siku 21 za kazi, hakikisha hakuna kasoro, majina yawe sawa, kama kuna kasoro kwenye majina basi nenda kwa mwanasheria yupo hapo jengo LA Nyumba atakusaidia ( affidavit)

Nili submit kila kitu trh 2 passport nikapata trh 27.mwezi huo huo. Hakuna mbwembwe Siku hizi, andaa 150000 weka mpesa yako utalipia online.
 
Kama una viambatanisho vyote ni Siku 21 za kazi, hakikisha hakuna kasoro, majina yawe sawa, kama kuna kasoro kwenye majina basi nenda kwa mwanasheria yupo hapo jengo LA Nyumba atakusaidia ( affidavit)

Nili submit kila kitu trh 2 passport nikapata trh 27.mwezi huo huo. Hakuna mbwembwe Siku hizi, andaa 150000 weka mpesa yako utalipia online.
Ilikua mwezi wa ngapi huo?
 
Kama una viambatanisho vyote ni Siku 21 za kazi, hakikisha hakuna kasoro, majina yawe sawa, kama kuna kasoro kwenye majina basi nenda kwa mwanasheria yupo hapo jengo LA Nyumba atakusaidia ( affidavit)

Nili submit kila kitu trh 2 passport nikapata trh 27.mwezi huo huo. Hakuna mbwembwe Siku hizi, andaa 150000 weka mpesa yako utalipia online.
Hii process ulifanya ilikua mwezi wa ngapi?
 
Kwa hapa Mwanza nikifanya process za hii Electronic Passport nitaipata baada ya mda gani. Passport inahitajika kabla ya terehe 3 mwezi wa 11.View attachment 899985
Hakikisha una
1. Kitambulisho cha taifa
2. Cheti cha kuzaliwa
3. Affirdavit ya mzazi mmoja
4. Barua ya mwaliko au uthibitisho wowote wa safari
5. Application form ambayo utakuwa umeapply online(utalipia 20,000)
6. Barua ya mtendaji wa kijiji/kata kama sio mwajiriwa.
7. Uthibitisho wa shughuli zako unazofanya i.e barua ya mwajiri kama ni mfanyakazi e.t.c
8. Kitambulisho cha kazi kama ni mwajiriwa
9. Barua ya ombi la passport
Wanaweza wakahitaji zaidi kulingana na madhumuni ya safari yako na pia shuguli zako e.t.c
Ingia kwenye hii link utapata kila kitu ikiwemo namna ya kujaza ombi lako online
Online ppt form

Sehemu inayosumbuaga sana ni hapo uhamiaji mkoa kwa maombi ambayo unaombea mkoani ila ukishakamilisha kila kitu na wakapitisha basi ombi lako likishaenda Dar ni chap tu passport yako itatumwa.
Hakikisha wanajua kuwa tarehe unayosafiri imekaribia as watakusaidia uweze kupata kwa haraka kabla ya safari
Ukienda siku ya kwanza kama wakikuambia kuna kitu bado hujakamilisha waambie wakague wakuambie kila ambacho kinamiss maana inawezekana vinamiss vitu vingi ila wakakuambia kimoja tu halafu siku ukirudi tena ndo wanakuambia hicho kingine unajikuta unaenda na kurudi mara nyingi.
Kila kitu utakachotoa kopi i.e cheti cha kuzaliwa, kitambulisho cha taifa e.t.c hakikisha kinathibitishwa(kupigwa muhuri) na mwanasheria/hakimu, sijui kama hili ni lazima lakini mimi waliniambia nikapige muhuri.

Kwa ushauri wangu usiwe mtu wa story nyingi za kuelezea kwa nini huna unapoulizwa document ambayo huna, we nenda kaitafute(utaipataje utajua mwenyewe) usipende sana kuvunja sheria au kutofuata inachosema we ikunje halafu pita, mara nyingi wanachotaka ni kuiona suala la kuwa genuine au sio hawataangalia sana isipokuwa kwa zile document za kitaifa zinazojulikana na kila mtu kama birth certificate na kitambulisho cha taifa. Kumbuka na yeye anapoipeleka kwa mkuu wake inabidi akaanze kuelezea story za kwa nini document fulani haipo na hapo unakuwa unawapa kazi ya ziada kwa hiyo hawapendi sana hizo story.

Kila la heri.
 
nami nataka ku-re new yangu ila wazazi wangu hawana cheti cha kuzaliwa! Nifanyeje?
 
nami nataka ku-re new yangu ila wazazi wangu hawana cheti cha kuzaliwa! Nifanyeje?
Hilo nalo neno, maana kuna wengine wazazi wao hawakuwa na hivyo vyeti enzi zao na wengine sio tu wapo na hawana ila walifariki pengine muombaji alikuwa mtoto sana....
 
Hilo nalo neno, maana kuna wengine wazazi wao hawakuwa na hivyo vyeti enzi zao na wengine sio tu wapo na hawana ila walifariki pengine muombaji alikuwa mtoto sana....
Utatumia Affidavit (kiapo cha kuzaliwa)
 
Hakikisha una

4. Barua ya mwaliko au uthibitisho wowote wa safari

7. Uthibitisho wa shughuli zako unazofanya i.e barua ya mwajiri kama ni mfanyakazi e.t.c
8. Kitambulisho cha kazi kama ni mwajiriwa
.
Si kila anayeomba passport anasafiri na ana kazi .Passport huhitajika kwa ajili ya kufanya mitihani ya nje kama vile ya BRITISH COUNCIL ya IELTS (International English Language Testing System na kwa ajili ya kuomba scholarship,Nchi zote za Afrika mashariki ni Tanzania tu yenye haya masharti na imani kuwa mtu huomba passport kwa sababu anasafiri!!!!!!!!! VERY SAD.Mtu anataka afanye mitihani au aombe scholarship fomu ya kuomba passport inakomaa andika nchi unakoenda na ambatanisha uthibitisho wa safari!!!!!!!! ha ha ha
 
Ni ndani ya siku 7 kwa gharama ya Tshs. 150,000/= au ndani ya masaa 24 kwa gharama ya Tshs. 1,000,000/= hizo ni bei halali za serikali.
 
Kama una viambatanisho vyote ni Siku 21 za kazi, hakikisha hakuna kasoro, majina yawe sawa, kama kuna kasoro kwenye majina basi nenda kwa mwanasheria yupo hapo jengo LA Nyumba atakusaidia ( affidavit)
.
Rwanda inachukua siku nne kupata passport mpya ku renew inachukua siku mbili sisi siku 21 aiseee gonga hapo chini

ORDINARY PASSPORT

PROCESSING TIME

Four (4) working days for first application and two (2) working days for renewal
 
Back
Top Bottom