Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Wakati Tanzania leo ikiadhimisha miaka 11 tangu kufariki kwa Baba wa Taifa Mwl. Julius K. Nyerere, maadhimisho hayo yanafanyika kitaifa mkoani kigoma ikiambatana na na kuzimwa kwa mwenge wa uhuru. Habari nilizozipata ni kuwa meneja wa SIDO mkoani kigoma aliyefahamika kwa jina la Daniel Njowelo amewekwa rumande kwa amri ya mkuu wa wilaya ya kigoma Bw. John Mongella.
Sababu ya Bw. Mongella kumuweka ndani meneja huyo wa SIDO ni kuwa kuna miradi ya vikundi vidogo vidogo inayokadiriwa kufikia Shilingi bilioni 7 ilitarajiwa kuzinduliwa. Jiwe la msingi la miradi hiyo inasemekana kuwa lilijengwa na SIDO ili siku ya kuwasili mwenge hapo kigoma basi uzinduzi ufanyike ambapo Raisi kikwete alitarajiwa kufanya uzinduzi huo. Kituko ni kuwa jiwe la msingi lilitakiwa kufunikwa kwa kitambaa ili siku ya ufunguzi mkuu wa kaya anafunua kitambaa kuashiria uzinduzi huo badala yake jiwe hilo la msingi likawa liko wazi tu hadi siku ya leo ambapo mkuu wa kaya akazindia hiyo miradi kwa kufuta vumbi tu.
Jambo hilo halikufanyika na alipotafutwa meneja huyo wa SIDO alikutwa akiwa katika bar moja akipata yale maji ya pale ilala bila wasiwasi wowote na kujikuta akisombwa msobemsobe hadi polisi.
Sababu ya Bw. Mongella kumuweka ndani meneja huyo wa SIDO ni kuwa kuna miradi ya vikundi vidogo vidogo inayokadiriwa kufikia Shilingi bilioni 7 ilitarajiwa kuzinduliwa. Jiwe la msingi la miradi hiyo inasemekana kuwa lilijengwa na SIDO ili siku ya kuwasili mwenge hapo kigoma basi uzinduzi ufanyike ambapo Raisi kikwete alitarajiwa kufanya uzinduzi huo. Kituko ni kuwa jiwe la msingi lilitakiwa kufunikwa kwa kitambaa ili siku ya ufunguzi mkuu wa kaya anafunua kitambaa kuashiria uzinduzi huo badala yake jiwe hilo la msingi likawa liko wazi tu hadi siku ya leo ambapo mkuu wa kaya akazindia hiyo miradi kwa kufuta vumbi tu.
Jambo hilo halikufanyika na alipotafutwa meneja huyo wa SIDO alikutwa akiwa katika bar moja akipata yale maji ya pale ilala bila wasiwasi wowote na kujikuta akisombwa msobemsobe hadi polisi.