Source:Mananchi newspapers, 09/03/10
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, katika kipindi cha kati ya , Novemba mwaka jana hadi mwishoni mwa wiki iliyopita, raia wanane wa China, walikuwa wameuawa katika matukio ya ujambazi yaliyoambatana na uporaji wa mali zao.
Mwenyekiti wa wafanyabiashara hao, Huo Jin Feng, alisema Wachina wanaofanyabiashara zao katika eneo la Kariakoo, wamepoteza imani ya kulindwa na askari kwa kuzingatia kuwa matukio hayo yanazidi kukithiri.
"Tangu Machi mwaka jana hadi leo, Wachina 12 wameuawa na majambazi wengi wao wakiwa ni wafanyabiashara na mafundi wa barabara. Lakini pia wengine wameporwa mali mbalimbali zikiwemo fedha, jambo linatishia amani yetu na ndiyo maana wengi wanatamani kurudi kwao na kama wasingekuwa na mizigo mikubwa ya biashara wangesharudi,'' alisema Jin Feng
Jin Feng alisema usiku wa Februari 28 mwaka huu, katika Mitaa ya Agrey na Lumumba Kariakoo, majambazi yalimuua mwenzao, Xu Shouxi (60) ambaye mwili wake, unasubiri maamuzi ya mtoto wake kuhusu ama uzikwe nchini au upelekwe China.
Katika mkutano huo, ofisa mmoja wa polisi ambaye hakutaka jina lake litajwe, alisema mkakati umeanza wa kuimarisha doria katika eneo la Kariakoo na maeneo mengine ili kuondokana na adha ya kuvamiwa kwa raia wa China na wananchi kwa jumla.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, katika kipindi cha kati ya , Novemba mwaka jana hadi mwishoni mwa wiki iliyopita, raia wanane wa China, walikuwa wameuawa katika matukio ya ujambazi yaliyoambatana na uporaji wa mali zao.
Mwenyekiti wa wafanyabiashara hao, Huo Jin Feng, alisema Wachina wanaofanyabiashara zao katika eneo la Kariakoo, wamepoteza imani ya kulindwa na askari kwa kuzingatia kuwa matukio hayo yanazidi kukithiri.
"Tangu Machi mwaka jana hadi leo, Wachina 12 wameuawa na majambazi wengi wao wakiwa ni wafanyabiashara na mafundi wa barabara. Lakini pia wengine wameporwa mali mbalimbali zikiwemo fedha, jambo linatishia amani yetu na ndiyo maana wengi wanatamani kurudi kwao na kama wasingekuwa na mizigo mikubwa ya biashara wangesharudi,'' alisema Jin Feng
Jin Feng alisema usiku wa Februari 28 mwaka huu, katika Mitaa ya Agrey na Lumumba Kariakoo, majambazi yalimuua mwenzao, Xu Shouxi (60) ambaye mwili wake, unasubiri maamuzi ya mtoto wake kuhusu ama uzikwe nchini au upelekwe China.
Katika mkutano huo, ofisa mmoja wa polisi ambaye hakutaka jina lake litajwe, alisema mkakati umeanza wa kuimarisha doria katika eneo la Kariakoo na maeneo mengine ili kuondokana na adha ya kuvamiwa kwa raia wa China na wananchi kwa jumla.