Edward Lowassa na Wanaomzunguka

Edward Lowassa na Wanaomzunguka

"If you want to judge others, start yourself"
Think big and ask yourself how good you are than others?

rangau I.q yako ni kubwa mno!
wapo watu wenye akili nzito,na nyepesi kimaamuzi!
 
Last edited by a moderator:
Nyie lieni tu lakini watanzania wameshasema,awe mchafu awe msafi wameshamtaka mtu wao,matope yote aliyopakwa lowassa miaka nane iliyopita sasa amesafishwa na wale wale waliomchafuwa
 
Hii ni kawaida kutokea hasa ktk nchi za Afrika.Mmesahau Rais Jacob Zuma Wa South Afrika,alituhumiwa kukwiba hela pamoja na uasherati, Hadi akatimuliwa umakamu Wa Rais na Rais Wa wakati ule bwana Thabo Mbeki?.Mfano mwingine ni Kenya,Rais Uhuru Kenyata alishtakiwa ICC kwa kushiriki kikamilifu ktk mauaji wakati Wa uchaguzi 2007, Lakini Leo ndie Rais Wa Kenya, sasa ajabu iko wapi kwetu sisi watanzania kuongozwa na Edward Lowasa? Kwani sisi tumestaarabika kuliko hao wenzetu?
 
Tatizo la Lowasa ni nyota,yani hata muongee nini Ikulu ni ya Lowasa mungu ndo ameamua hivyo
 
Sio tu wanaomzunguka hata yeye mwenyewe ni mashaka matupu
 
Alienda kuleta wawekezaji kwenye mvua ya kutengeneza Thailand, ili Mtera yajae maji, umeme uzalishwe... na pia barabara ya Bagamoyo/Ali Hassan Mwinyi aliifanya njia tatu, foleni ikapungua....; alifinyanga kama udongo shule za kata...na mwisho alijiuzulu kwa kuwa akina Sitta walikuwa wanamuonea gele na uwaziri mkuu......JUST IMAGINE hayo ndo maamuzi magumu hadi inakuwa kete ya kupata Urais!!!!
 
"If you want to judge others, start yourself"
Think big and ask yourself how good you are than others?

Mheshimiwa Rangau, tumia kiswahili ili ueleweke vema na wana jukwaa wote. Kiingereza ilichoandika hakipo sahihi.

Sina chuki na Edward Lowassa. Nina shida na nafasi anayoitaka kwa sababu hafai.
 
Kule China mafisadi wanapigwa risasi bila kujali vyeo vyao.
Kuwa fisadi ni uamuzi mgumu. Maamuzi magumu ya Lowassa anayo jinasibu nayo zaidi ya ufisadi siyaoni.
 
Anaposema anauchukia umaskini anamanisha kabisa. Ni tajiri kupindukia.
Sijui wangapi wanaelewa kwamba kawa tajiri at our expense! Sehemu ya kubwa ya umaskini wetu ni matokeo ya ufisadi wa watu kama yeye.
Akiwa Rais, tutatoka kwenye umaskini hadi ufukara wa kutupwa.
 
ameisha waambia mlete ushahidi wapi kala rushwa na ningapi na nani kampa. sasa mbona hamtaki kuelewea. kama hamna ushahidi mnatuandikia ngonjela na hadithi za kusadikika tu.


Nachelea kusema kwamba, Edward Lowassa amezungukwa na watu wanaotiliwa shaka na taifa. Wengi wao ni watuhumiwa wa ukiukwaji wa maadili ambayo ni msingi muhimu wa uongozi. Katika mazingira kama haya, Edward Lowassa hawezi kukwepa kuitwa si mwadilifu ikiwa rafiki zake si waadilifu.

Nitaendela........[/QUOTE]
 
Kuna dhana mbalimbali zimejengeka juu ya mtangaza nia ndugu Edward Lowassa. Dhana hizo kwa ufupi ni kama uwezo wa kuchukua maamuzi magumu ambayo kimsingi hayawekwi wazi ni yapi. Pia kuna dhana ya uchapa kazi ambayo imekua ikitetewa zaidi na watu wa kambi yake kwa kutolea mifano isiyojitosheleza kimaudhui. Vilevile, kabla na wakati wa mchakato mzima wa kuitangaza safari ya matumaini, tumeshuhudia vitendo mbali mbali vinavyoashiria jeuri yake pamoja na wanaomzunguka dhidi ya mamlaka ya chama na serikali. Kwa ufupi ni mambo mengi yametokea na yataendelea kutokea kuelekea ukingoni mwa mchakato mzima wa kumsaka mrithi wa Jakaya Kikwete.

Nikiwa kama mtanzania kijana mwenye matumaini makubwa na Tanzania ijayo, nakumbwa na mashaka sana na ushabiki unaoendelea juu ya dhana ya maamuzi magumu ya ndugu Edward Lowassa. Mara nyingi nimemsikia akizungumzia dhana hii bila kufafanua maamuzi magumu yanalenga shabaha gani katika kuondokana na umaskini uliokithiri hapa nchini. Kwa mfano, alipokua akitangaza nia ya kuomba ridhaa ya wana CCM kugombea kiti cha urais mkoani Arusha, kauli ya maamuzi magumu ilisababisha uwanja wa Amri Abeid kulindima kwa shangwe za hali ya juu. Mimi binafsi nilibaki nimeduaa nisijue maana halisi ya shangwe hizi. Kwa maoni yangu, nadhani hayo ndio mazingira yanayopelekea watu kuamini kwamba ndugu Edward Lowassa ananunua watu wanaohudhuria mikatano yake. Ni mtu aliyenunuliwa au mwenye uwezo mdogo wa kufikiri anayeweza kushabikia vitu asivyoviamini.

Nadhani shabaha ya dhana ya uchapakazi inalenga kuonyesha ni kwa jinsi gani ndugu Edward Lowassa anafaa kua kiongozi wetu kwa sasa kuliko wakati wowote ule. Kwa maana nyingine ni kutaka kuonyesha kwamba watanzania hawawezi kuhamasika kufanya kazi mpaka wapate rais mchapa kazi kweli kweli. Utata mwingine unaibuka ni kwa jinsi gani tunajua kupima uchapakazi wa mtu, je ni kukesha ukifanya kazi yenye matokeo hafifu au ni kufanya kazi kwa ufanisi? Rafiki zangu wengi wanamzungumzia Edward Lowassa kama mchapakazi asiye na mfano, kwa kiingereza tuseme kwamba, "he is a job addict".

Kimsingi dhana hii ya uchapakazi ni sehemu tu ya vigezo vingi vya kiongozi bora. Tanzania ya sasa inahitaji kiongozi mwenye maono anayeweza kulihamasisha taifa kuamini kwamba maendeleo ya kweli yataletwa na watanzania wenyewe kwa kufanya kazi kwa bidii na maarifa. Hatuhitaji kiongozi wa staili ya Edward Lowassa ambaye wakati wa uongozi wake kama waziri mkuu aliwatisha watendaji wake badala ya kuwahamasisha wafanye kazi kwa bidii na maarifa.

Suala tata zaidi juu ya mtia nia huyu ni tabia ya watu wanaomzunguka. Ni kana kwamba uchaguzi huu unapitia vita kali kati ya kundi la wenye kipato kisicho halali dhidi ya wanaojipambanua kua wazalendo wa kweli. Ni kama vile wale tunaowajua kwamba ni mafisadi wanataka kusimamisha uongozi wa kifisadi ili kulinda maslahi yao. Na upande mwingine wa shilling ni kwamba kundi la wazalendo limejipanga kuingia madarakani kwa nia moja kubwa, nayo ni kuwashughulikia mafisadi. Hii ni vita kubwa sana na bahati mbaya wahanga ni maskini wale wale wanaoshabikia mambo wasiyoyajua.

Nachelea kusema kwamba, Edward Lowassa amezungukwa na watu wanaotiliwa shaka na taifa. Wengi wao ni watuhumiwa wa ukiukwaji wa maadili ambayo ni msingi muhimu wa uongozi. Katika mazingira kama haya, Edward Lowassa hawezi kukwepa kuitwa si mwadilifu ikiwa rafiki zake si waadilifu.

Nitaendela........
mimi nilikwenda kumsikiliza wala sio mshabiki wake na sikuwa nimehongwa kwa hiyo hoja ya kwamba wote waliokwenda kumuona wamenunuliwa sio kweli na sio vizuri kujenga hoja kwa misingi ya uzushi na uongo
 
mimi nilikwenda kumsikiliza wala sio mshabiki wake na sikuwa nimehongwa kwa hiyo hoja ya kwamba wote waliokwenda kumuona wamenunuliwa sio kweli na sio vizuri kujenga hoja kwa misingi ya uzushi na uongo

Ndugu gnassingbe,

Pole sana. Nadhani nimekukwaza kwa kuandika juu ya umpendaye. Bahati mbaya sana suala la urais ni zito na linagusa maisha ya kila mtanzania. Mimi kama mtanzania ni wajibu wa kutoa maoni yangu juu ya rais ajaye. Hii si dhambi.

Naomba usome vizuri andiko langu. Sijasema Edward Lowassa anawalipa pesa wanaohudhuria mikutano yake. Lakini mazingira ya mikutano yake yanapelekea watu waamini hivyo. Huyu jamaa hana hoja nzito lakini watu wanashangilia kupita kiasi. Hapa pana walakini. Inaewezekana watu wanalipwa kushangilia au upeo wao wa kuchambua mambo ni mdogo.
 
Back
Top Bottom