EATV ni kituo bora kuliko Clouds Tv

LICHADI

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2015
Posts
4,717
Reaction score
13,439
Wakuu nimefuatilia vipindi vya clouds TV na EATV lakini naona EATV wako vizuri sana katika vipindi vyao.

Clouds tv utoto ni mwingi sana

Kama juzi tu taarifa yao ya habari walisoma watoto..kwa kisingizio kuwa ilikuwa ni siku ya mtoto..Hivi mlishawahi ona kipindi muhimu kuliko vyote kama taaarifa ya habari wanaendesha watoto?

Hata CNN,ITV,TBC,BBC sijawahi ona bali nnavyojua mimi watoto huwa wana vipindi vyao maalum
EATV kituo bora cha burudani
 



Bado unaangalia clouds??

Si bora ukaangalia ngoma za vigodoro
 
Hii kali. Yaani EATV inakuwa bora kuliko Clouds TV kwasababu tu Clouds TV iliweka watoto kusoma habari siku ya watoto Afrika?! Very insuffient and weak argument indeed. Sasa kama hiyo ni sababu, mbona kuna TV stations nyingi tu hazikuweka watoto kusoma habari siku hiyo? Kwanini hukuzilinganisha hizo na Clouds badala ya EATV?
 
Clouds na Uhuru pamoja na TBC ni kampuni moja tu.....wote waganga njaa wa Lumumba
 
Ulikuwa unafananisha EATV na Clouds TV! EATV wako mbali sana kwa ubora katika vipindi vyao kuliko hao clouds labda kwa sababu clouds bado wachanga wanaweza kuimprove siku za usoni.
 
Sasa utalinganisha vipi Tv ya ya East Africa na hiyo local channel. Ambayo hata haipo kwenye baadhi ya ving'amuzi hapo Tz.
 
Hivi unajua clouds ni anaiga vipind kutoka EATV? Eatv huwez fananisha na uchafu wa clouds... Clouds labda radio tu ndo inawapa jina
 
Msifananishe eatv na vitu vya kijinga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…