Nimeishawasilisha malalamiko yangu tangu mwezi wa Nne (April) hadi sasa mwezi huu wa saba (Julai), bado nasubiri majibu. Hii sio sawa kabisa, Kila siku serikali inahamasisha matumizi ya tehama (mifumo) ili kurahisisha mambo ila serikali yenyewe haiko active katika mifumo yao hiyo.
Hii ni aibu sana. Hapo mfumo huu ulitumia pesa nyingi za walipa kodi watanzania, cha ajabu haufanyi kazi. Tunaomba serikali angalieni hili kama tatizo ni watumishi badilisheni watumishi wengine. Yaani unawasilisha lalamiko unasubili zaidi ya miezi mitatu, sasa si afadhari tuwe tunawafuata huko ofisini hakuna haja ya hii mifumo, ni uharibifu tu wa pesa za watanzania.