-Mashambulizi ya Israel yanatoa mwanya kwa Muslim Brotherhood kuhalalisha 'Extremism' sasa.In fact mashambulizi haya yatakua mna madhara zaidi kwa utawala wa Benjamin Netanyahu na pia relation ya Israel na Egypt most probably it will suffer a setback.
-Naona hapa Iran itatumia Mwanya huo kuikomoa Israel kwa kusambaza silaha nzito hasa Tanks za kurusha Makombora ya masafa mafupi na Marefu.
-On the other hand Bashar Al Asad wa syria atapata Mwanya wa kufanya severe casuality kwa waasi na Attention itakua mgogoro wa Israel na Palestine in the coming days kama mambo hayatatutliwa mapema
-Naona huko baadae Egyptians wanaweza kurudi Tahrir Square kushinikiza Serikali yao kuchukua msimamo ambao pengine akina Morsi wasingependa mapema kiasi hiki juu ya kuchukua hatua dhidi ya maslahi ya Israel kinyume hata na mkataba wa Camp David
Shukran Ben, siyo tu kuwa mzozo utaondoa attention Syria bali pia Iran ambako mgogoro wa Nuke bado ni mbichi na unafukuta.
Inaelezwa na wachambuzi wa mambo ya kisiasa kuwa shambulio hilililiandaliwa na Israel ili kumjenga Netanyahu kisiasa.
Mwezi January wana uchaguzi na hivyo anakabiliwa na upinzani kutoka kwa waziri wake wa mambo ya nje.
Njia hii ni kutaka kumpiku kwa kuonyesha ubabe dhidi ya Gaza.
Jambo moja ambalo watu wengi sana wanalisahau ni kuwa mzozo huu wa siku tano sasa haukuanzishwa na HAMAS.
Umeanzishwa na Israel kwa kumuua kamanda wa kikosi cha anga cha HAMAS.
Sidhani kuwa kuna kikundi kingevumilia hali hiyo tena mauaji yalikuwa ''collective punishment' kwa yoyote aliyekuwa ndani ya jengo hilo.
Vyombo vya habari vimeshupalia kuwa HAMAS inamwaga maroketi na Israel ina haki ya kujilinda.
Huo si ukweli ni propaganda za Israel ambayo kwa namna fulani imepewa haki dhidi ya wanadamu wengine.
Kauli ya Rais Obama kuwa Israel ina haki ya kujilinda kutokana na mashambulio ni ''standard statement' ambayo inatumika iwe ndani ya senate, Congress au kwingineko. Hapo ndipo nguvu ya Waisrael katika Marekani inaonekana.
Ukweli ni kuwa Israel haina uwezo kiasi kinachodhaniwa bila mgongo wa Marekani.
Kinachotokea ni kuwa Waisrael wamejipenyeza sana katika vyombo muhimu kule Marekani na ndio wanaotoa kauli.
Kwakuwa ndio wanamiliki media, ukisikiliza CNN au Channel yoyote utasikia kuhusu maroketi ya HAMAS. Hutasikia nini kilianza hadi maroketi yakaanza kurushwa. Nani alianza uchokozi.
Tatizo linakuja pale Israel itakapovutika na kuingia katika mzozo na Iran. Kwasasa Iran inaonekana kuwa super power katika mashariki ya kati licha ya kudhoofika sana kiuchumi. Wao wana kundi la SHIA ambalo ni sehemu kubwa tu ya mideast.
Huko nyuma kulikuwa na tension kati ya Turkey na Israel hasa baada ya Flotila kushambuliwa.
Ukiiangalia jiografia kwa umakini Israel ipo katika mazingira yanayohitaji amani zaidi ya vita.
Ule ubabe wa piga piga utawaletea matatizo makubwa. Kizazi kilichopo ni tofauti na kile cha akina Gamal Abdul Nasar n.k.
Kibaya zaidi ni kuwa Brotherhood wenye ushawishi wa hali ya juu katika siasa za mashariki ya kati ndio wanaongoza Egypt yenye ushawishi mkubwa kama nchi. Hapo Camp David accord ipo lakini njia panda.
Jambo lingine ambalo watu pia hulisahau ni kuwa Gaza ni refugee camp. Hakuna kiingiacho Gaza bila kupitia Israel.
Inashangaza hata hizo Qasam na katushi wanapata wapi malighafi maana wamezungukwa kila kona.
Si sahihi kusema mapigano kati ya Israel na Palestine, ni mapigo ya Israel kwa Palestine kwasababu huwezi ukawa na laiser giuded missile kukabiliana na mtu mwenye jiwe!
Katika zaidi ya miaka 4 wakazi wa gaza wamelazimika kupunguza hata milo kwasababu ya ukosefu wa chakula na madawa kwa wagonjwa. Israel inazuia kila aina ya msaada.
In other words haya ni mauji ya kimya kimya!(cold masacre) na dunia haionekani kushtuka.
Dunia ina double standard kubwa sana. Israel imekaidi maazimio ya UN mengi tu na hakuna kinachotokea.
Hayo yakitokea akina Taylor na wenzake wapo the Hague.Hii si halalishi uhuni wa mauaji yoyote, ninachotaka kuonyesha hapa ni kuwa kuna stanadard za dunia kulingana na matakwa ya wakubwa na si makubaliano au taratibu
Nakumbuka enzi hizo ungewasikia akina Jose Broz Tito, Olf Palme, Indira Gandhi, Nyerere kwa uchache japo wakipaza sauti na kusema hivi si sahihi.
Leo nani aseme, kila mtu anataka kwenda shopping washington!