Much respect Ngongo. Tanzania haina upungufu wa mawazo wala gesi.Nilitarajia Prof Lipumba kwa usomi wake angetoa maoni nini kifanyike ili gesi iliyogunduliwa Mtwara isaidie kuinua kiwango cha maisha bora kupitia miradi ya kiuchumi kama ujenzi wa viwanda vidogo na vikubwa,ujenzi wa miundombinu ya kisasa reli,barabara na bandari itakayotoa huduma kwa wilaya na mikoa inayopakana na Mtwara.
Gesi ya Mtwara Ni nyingi sana kuna jarida niliwahi kulisoma wana sema gesi ni nyingi kuliko mahitaji ya Tanzania !.Kama ni kweli basi gesi ya Mtwara ni lazima isafirishwe sehemu mbali mbali za nchi si Dar bali mikoa mingine ya Tanzania ikichagizwa zaidi na sababu za kiuchumi zaidi.
Nilitarajia pia angezungumzia uwazi wa mikataba ya gesi,angezungumzia sera ya gesi,angezungumzia uimarishwaji wa TPDC kwa maana ya kujengewa uwezo wa kutafuata na kuchimba mafuta na gesi siku za usoni.
Hoja hizi nilitarajia zingetolewa na Prof Lipumba lakini kinyume chake kakimbilia kujivika umiliki wa gesi ya Mtwara na ukombozi wa waislam Tanzania
Mkuu Mchambuzi, CCM imepoteza matumaini ya wananchi wa Mtwara kwasababu nyingi.Mkuu Nguruvi3, per bandiko lako namba 263, is it pre mature to conclude kwamba katika sakata hili, ccm haina matumaini ya kurudisha imani za wana mtwara tena kama chama na badala yake, tumaini lililobakia kwa ccm kurudisha imani kwa wananchi ni kupitia chama cha CUF?
Vile vile kuhusiana na hoja yako juu ya kwanini tume maalum ya bunge ndio ishughulike na mtwara badala ya wabunge wa mtwara, je unajadili vipi hili katika muktadha wa Katiba ya JMT inayosema mbunge sio mwakilishi wa wananchi wa jimbo lake tu bali mbunge ni mwakilishi wa wananchi wa Tanzania nzima; Je kipengele hiki cha katiba kiliwekwa kwa ajili ya mambo kama haya au kiliwekwa kwa nia njema ila kinatumiwa vibaya?Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Mchambuzi,Habari yako Ndugu yangu,ni tumain langu kuwa ni u-bukheri wa afya,huku sisi hakuchi kunakucha,matumain tumepoteza na watawala hawa wa nchi hii...Mkuu Nguruvi3, per bandiko lako namba 263, is it pre mature to conclude kwamba katika sakata hili, ccm haina matumaini ya kurudisha imani za wana mtwara tena kama chama na badala yake, tumaini lililobakia kwa ccm kurudisha imani kwa wananchi ni kupitia chama cha CUF?
Vile vile kuhusiana na hoja yako juu ya kwanini tume maalum ya bunge ndio ishughulike na mtwara badala ya wabunge wa mtwara, je unajadili vipi hili katika muktadha wa Katiba ya JMT inayosema mbunge sio mwakilishi wa wananchi wa jimbo lake tu bali mbunge ni mwakilishi wa wananchi wa Tanzania nzima; Je kipengele hiki cha katiba kiliwekwa kwa ajili ya mambo kama haya au kiliwekwa kwa nia njema ila kinatumiwa vibaya?
Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
UZAO WA MTOTO FAMILIA YA KIFALME UINGEREZA
Prince William na mkewa Kate Middleton wanataraji kupata mtoto wa kwanza wakati wowote.
Hadi tunaandika bandiko hilo wawili hao bado wapo Hospitali na hakuna tangazo la uzazi.
Inasemekana tarehe za kuzaliwa mtoto zimepita kwa muda fulani jambo la kawaida katika uzazi
Wanahabari wamepiga kambi kupata habari za uzao wa mtoto huyo ambaye hadi sasa anajulikama kama baby Cambridge. Haijulikani ni wa kiume au wa kike.
Utaratibu wa kufuata katika kutangaza habari za uao ni kwa prince William kumpigia simu malkia kwanza halafu wana familia wa Buckingham kutoa taarifa za ujio wa mtoto katika familia ya malkia. Huyu atakuwa kitukuu cha malkia Elizabeth II
Imefika wakati watu kuhoji jina la mtoto huyo litakuwa ni nani huku kukiwa na orodha ndefu ya mapendekezo.
Swali kubwa linaloulizwa ni hili, kwanini mtoto huyo apewe 'attention' ili hali kuna mamia ya watoto wanazaliwa kila siku tena wengine katika hali ngumu zaidi?
Kuna majibu mengi juu ya hili.
1. Jambo linalohusu familia ya kifalme Uingereza hufungamanishwa sana na biashara.
Inasemwa kuwa ndoa ya Kate na William iliingiza mabilioni ya dola kupitia bidhaa, matangazo, utalii n.k.
Na hili halionekani kwenda mbali na ukweli huo. Bidhaa zinauzwa kuhusiana na mtoto huyo mtarajiwa na vyombo vya habari vikitoa makala na habari za kibiashara.
2. Waingereza ni wazuri wa kupiga debe katika mambo yao.
Wanapoamua kulifanya jambo dogo kuwa kubwa wanauwezo huo.
Hili linagusa sana tamaduni zao na ni moja ya mambo yanayowaunganisha waingereza.
3. Mtoto mtarajiwa ana uhusiano na siasa za nchi yake na za kimataifa.
Hapa ndipo tuanzie kwasababu ni sehemu muhimu sana ya uzao huu.
Kwanza, tuangalie kwa uchache kuhusu familia ya kifalme. Familia hii ndio inayotoa mkuu wa nchi ya falme za uingereza (United Kingdom).
kuna tofauti ya united kingdom na England na ni rahisi sana kuchanganya mambo hayo.
Waziri mkuu wa Uingereza ni mkuu wa serikali na siyo mkuu wa nchi. Yeye hupata ridhaa ya kutawala kutoka Buckingham Palace ndipo anaelekea number 10 Downing street.
Familia ya kifalme ndio pia wakuu wa kanisa la Uingereza la Church of England.
Kutokana na ukoloni tulikuwa na kanisa la England church ambalo limebadilika kwa jina kutokan sasa hivi linajulikana kama Anglican na sehemu nyingine wanaita African Inland church n.k.
Kwa muda wa miaka 300 taratibu za utawala zilihusisha unasaba wa damu, kwamba kurithi kiti cha enzi wanaume walipewa kipaumbele. Iwapo mfalme au malkia alikuwa na watoto 3 wakwanza wa kike na wa pili wa kiume, kiti cha enzi kilimruka mwanamke na kwenda kwa mwanaume(throne)
Malkia Elizabeth alikuwa mtoto pekee wa King George na hivyo hakukuwa na chaguo bali yeye.
Kuna mambo yasiyosemwa kuhusu yeye kurithi kiti hicho kwani aliyepaswa kwa taratibu alikuwa mwanafamilia wa ndugu ambaye alikuwa ni mwanaume. hilo tutalijadili wakati mwingine.
Katika familia zilizofuata utaratibu wa uzao ni ile ya Diana na Charles ambao walipata watoto wawili Harry na William,William ndiye mrithi wa kiti na Harry ni kama spea.
Kwavile falme ilikuwa inafuta utaratibu wa miaka 300 iliyopita, urithi wa malkia ulikuwa ufuate utaratibu wa Elizabeth II, Prince Charles, William na Harry.
Utaratibu huu uliwaruka watoto wa Elizabeth wasichana kwasababu watoto wa kiume walifuatana na wao ndio warithi.Kwa muktadha huo prince Harry ni mrithi wa tatu(3rd in throne).
Kumbuka hili lina umuhimu katika mjadala.
October 28 2011 ufalme ulibadili taratibu na kuwa urithi wa kiti sasa hautachagua jinsia tena.
Kwa maneno mengine kama mtoto wa kwanza atakuwa mwanake basi atakuwa malkia hata kama wanaomfuata ni wa kiume.
Hii maana yake ni nini?
Maana yake ni kuwa mtoto mtarajiwa wa William na Kate siku moja atakuwa mfalme au malkia wa Uingereza na hivyo kiti cha enzi kitafuta utaratibu ufuatao:
1. Prince Charles
2. Prince William
3. 'Babay Cambridge' ambaye hajazaliwa
4. Prince Harry
Kwamba nafasi ya prince Harry sasa ni namba 4 na si tatu kama tulivyosema hapo awali.
Kwa kuangalia umri wa maisha 'longevity' wa malkia Elizabeth ni wazi prince Harry hatakuwa mfame.
Baba yake ana zaidi ya miaka 60,kaka yake ni mdogo katika miaka 30 na sasa kichanga na kila mmoja atakula shea yake kabla ya Harry ambaye hataonja ufame labda tu litokee janga kubwa sana lisilotarajiwa.
Ni kwa muktadha huo baby cambridge anategemewa kukalia kiti cha enzi kama mfalme au malkia na hapo atakuwa mkuu wa Anglican, mkuu wa nchi na mkuu wa jumuiya ya madola
(commonwealth).
Hivyo msisimko ni wa jumuiya kubwa ya kimataifa ni kwasababu mtarajiwa atakuwa na ushawishi mkubwa katika medani za kiutawala na kiimani ndani na nje ya Uingereza, na hili hasa ndilo linaleta msisimko duniani.
Endapo baby cambridge atakuwa wa kike basi uwezekano wa kuitwa Elizabeth au Victoria ni mkubwa sana. Sababu kubwa ni kuwa Victoria ndiye malkia aliyeongoza Uingereza kwa muda mrefu akifuatiwa na Elizabeth wa sasa ambaye itakapofika september 5 mwaka 2015 ataukuwa ameifikia rekodi ya Victoria.
Kwa uchache mtoto mtarajiwa atakuwa sehemu yetu Watanzania na mataifa ya madola kwasababu ndiye atakayekuwa mkuu wa jumuiya hiyo hata kama ni miaka 100 ijayo.
Haya ndiyo yanajiri na tutaendelea kuwaletea habari zaidi kadri zitakavyopatikana.
Tusemezane
Mgeni wa leo
Katika majadiliano hapa JF kuna siku moja Mchambuzi aliuliza swali moja ambalo sina majibu kama walivyo wengi. Hivi hii gesi ni kwa matumizi yapi? Ni LNG! na matumizi yake hasa ni industrial au ni yaweza kuwa domestic au ni vipi.
Hakuna aliyejibu kama ambavyo viongozi hawawezi kuwaeleza wananchi.
Ndio maana nasema si Mtwara tu sote hatujui nguvu hii inayotumika katika miradi bila wananchi kujua inakusudia nini hasa. Mchambuzi hebu tusaidie kidogo maana eneo hili umewahi kulieleza vema sana.
Nguruvi3,
Karibu sana katika mjadala;Kimsingi, naunga mkono hoja zako zote katika bandiko namba 34, lakini nikienda mbali zaidi, inaamsha mawazo mengine ambayo nadhani ni muhimu kwa huu mjadala kama nitakavyo fafanua;
Kwanza - hoja zako zinatulazimisha pengine tuangalie kwa undani the socio-economic profile ya eneo husika (Mtwara) kisha tuoanishe na thamani ya gesi asilia from the business and economic point of view, hasa nini kinaweza kupatikana kama benefits kwa wananchi wa eneo husika - both directly and indirectly;
Kama nilivyokwisha jadili, future value ya gesi asilia ni kwenye suala la nishati ambalo demand yake itazidi kukua siku hadi siku, huku projections zikiweka wazi kwamba mahitaji ya umeme wa gesi will outstrip umeme wa makaa ya mawe, nuclear na hydro duniani in the next 30 years;kuna sababu nyingi kwanini ni hivi, na partially Waziri Muhongo alielezea jana katika kuhitimisha hoja yake kwamba ukiondoa umeme wa hydro, umeme wa gesi ni bei nafuu per unit, huku akijadili kwamba pamoja na umeme wa maji kuwa nafuu, gharama zake za uwekezaji na uendeshaji, ni kubwa kuliko gesi; hivyo ndivyo nilivyomuelewa; Kwa maana hii, nishati ya gesi ndio where the future of this resource holds, hivyo uwekezaji wetu pamoja na faida kwa maeneo husika ujikite zaidi huko.
Lakini haina maana kwamba uwekezaji kwenye LNG plants hauna maana, kwani maana ipo, lakini cha msingi hapa ni kwamba matumizi haya yatazidi kupotea with stages of economic development yani matumizi ya gesi kwa ajili ya residential, commercial, industrial, na world energy outlook wanaweka wazi jinsi gani demand ya gesi kwa ajili ya matumizi haya inafikia saturation point marekani na sehemu mbalimbali za EU; Point yangu ya msingi hapa ni kwamba tuendelee to take advantage ya demand ya gesi kwa ajili ya residential, commercial and industrial wakati bado tupo kwenye take off stage of economic development ili tuvuke low levels of development ya sasa; Lakini kwa manufaa ya vizazi vijavyo, mbali ya kuwekeza ipasavyo na kupata short term and medium term gains ambazo zitatunyayua pia, tusijisahau kujipanga kisera tukapitwa na suala la gesi as the major source of energy for the future relative to thermal, hydro and nuclear;
Pengine hoja yangu hapo juu itaeleweka zaidi nikifafanua kama ifuatavyo:
Energy/Nishati ni basic input ambayo inahitajika kukidhi mahitaji mbalimbali ya binadamu kama vile heating, motive power (e.g water pumps, transportation etc) and lighting; businesses, industry na public services za kisasa kama vile afya, elimu, mawasiliano vyote hivi vinategemea sana access to energy services;as a matter of fact, ukosefu wa huduma za nishati upo directly linked na matatizo ya umaskini kama vile high mortality rates, low life expectancy, illiteracy and many other poverty indicators; katika nchi nyingi maskini, ukosefu wa huduma ya nishati pia huchangia sana tatizo la rural - urban migration; Kwetu Tanzania, Nishati ya gesi ni fursa muhimu sana ya kutusaidia kutatua matatizo yote haya, sio tu kwa mtwara bali nchi nzima; Ni katika muktadha huu, Waziri Muhongo alijeng hoja wakati wa hitimisho la bajeti ya wizara yake kwa kusema kwamba gesi ni mwokovu wa maskini wa Tanzania na serikali yake imejipanga kuitumia rasilimali hii kuiandaa Tanzania sio tu ipande na kuwa nchi ya uchumi wa kati ifikapo 2025 lakini pia itatuandaa kuingia karne ya ishirini na mbili kama taifa imara na bora kabisa socially, economically n.k; Naungana na hoja hii ya Muhongo lakini only if we manage to invest vizuri on where the future holds when it comes to suala zima la matumizi ya gesi baina na energy na Matumizi mengine;
Nikiwa bado katika hoja hii kuhusiana na faida za gesi asilia kwa uchumi, nadhani ni muhimu tukafanya profiling ya mkoa wa mtwara ili tupate fursa ya kuelewa jinsi gani viongozi wetu wanaweza kukaa nao na kukubaliana katika mambo ya msingi kuliokoa taifa letu; kwa maana nyingine, wengi tunasahau kufanya a profile analysis na ndio maana we fall short of understanding jinsi gani tulimalize tatizo la mtwara na kurudisha taifa letu katika hali yake ya amani, umoja, upendo, mshikamano na utulivu tuliyoizoea;Nitagusia machache kwa haraka haraka ili hata huko mbeleni, yakitokea matatizo kama haya mikoa mingine basi tutazame masuala kama haya:
1. At the turn of the new millennium (the year 2000) mtwara ilikuwa ni the second smallest region in Tanzania after Kilimanjaro; Sasa kwa wale wenye hoja kwamba gawio la bajeti lazima liendane na ukubwa wa eneo husika, suala la kilimanjaro kuwa top ten consistently na mtwara kuwa bottom five in terms of mgawanyo wa keki ya taifa, katika hili hoja zao zinakosa mashiko;
2. Mgawanyiko wa eneo per square kilometa, masasi ina cover 53% ya mkoa mzima huku newala, mtwara vijijini na tandahimba iki share the remaining area; implicationa zake hapa ni nyingi na tutazijadili baadae;
3. About 85% ya ardhi mkoani mtwara ni arable land, huku chini ya 25% of the 85% ikiwa katika matumizi ya kilimo; zao kuu la kilimo cha biashara ni korosho lakini pia wanalima karanga, sorghum,mihogo, paddy, mahindi, millet na simsim; Tukumbuke pia kwamba mtwara wana historia kubwa sana ya baa ya njaa na ni moja ya mikoa ambayo bado haijitoshelezi kwa chakula pamoja na ukweli kwamba sehemu kubwa ya uchumi wake ni subsistence based;
4. Mtwara unapakana na mikoa minne ya Tanzania - Morogoro, DSM, Ruvuma na Lindi; ni muhimu kuangalia economic linkages kati ya mtwara na mikoa hii kwa undani ili kubaini kwamba wapi kuna inputs muhimu kwa wanamtwara in the context of natural resource base yao, hivyo kuwekeza huko accordingly badala ya kuamua tu kwamba DSM is the only choice;
5.Mtwara ni moja ya mikoa iliyoathirika sana na net migration - net lifetime migration ni moja ya the highest in the country; Hii ni kwasababu mkoa huu umekuwa very unattractive kwa vijana lakini pia vizazi vipya, kwahiyo wanaenda kwingineko for greener pasture and by coincidence, vivutio vikubwa kwa wanamtwara ni ile mikoa niliyojadili kwamba throughout history imekuwa inapewa kipaumbele when it comes to keki ya taifa (bajeti); ni kwa mantiki hii, hata tume ya mipango katika taarifa yake ya mkoa wa mtwara inawaita vijana wa mtwara wanaohamia miji mingine kwamba ni "ECONOMIC REFUGEES"; kumbuka, hii ni serikali; Katika hili, tume ya mipango inajadili kwa uwazi kabisa kwamba ili kutatua tatizo husika, ni muhimu kwa serikali kuwekeza ili kuvutia nguvu kazi ya mtwara ibakie mtwara; Tume ya mipango inaenda mbali zaidi na kutaja maeneo muhimu ya kufanya ili kuinua mkoa huu kwamba ni pamoja na development of infrastructure, viwanda based on "local available resources", n.k, huku ikijadili kwamba - "this will make mtwara attractive to youths so that they don't need to go beyond its borders to seek a secure economic future";
6. Mtwara wakati wa mwalimu nyerere ulikuwa na viwanda - agro based industries, vitano vya kubangua korosho, viwili vya mkonge ambavyo vilikuwa vinatoa ajira na kuleta economic benefits mbalimbali kwa mkoa; leo katika hili, hali ni mbaya;
Tume ya mipango katika ripoti zake miaka nenda miaka rudi imekuwa very optimistic na maendeleo ya mtwara and mentions potential areas kuwa ni pamoja na maendeleo ya tourism industry, kilimo, forestry, ufugaji nyuki, uvuvi na VIWANDA; Sasa kama haya yamekuwa yakiwekwa bayana na tume ya mipango (serikali), basi ujio wa gesi ni fursa muhimu ya kutekeleza kwa vitendo;
Nguruvi3, maeneo mengine uliyojadili ni suala la quality na ajira kwa mtwara; naunga mkono hoja, na kwa kuongezea, ni muhimu kwa taifa sasa kuanza kuwa serious na national innovation systems ambayo itajenga skills, capabilities and entreprenuership drive kwa wanamtwara na watanzania kwa ujumla katika maeneo ya gesi na mafuta; na kwa mtwara, seriousness ni muhimu ianze kwa serikali kujenga chuo kitakachotoa mafunzo ya gesi na ambacho wawekezaji watalazimika kukichangia na pia kukishirikisha katika shughuli zao; kwa kifupi - faida ya gesi kwa wanamtwara itakuwa na manufaa tu iwapo itajitokeza katika economic output ya mkoa na employment na haya yalenge katika value chain ya sekta ya gesi - exploration, extraction, production, transportation, storage, distribution, servicing, maintenance, legal services, well services, construction, power generation, engineering services etc;inawezekana kwa leo hakuna such skills lakini tukiwekeza sasa, mtwara can become the centre of excellence afrika mashariki na kati katika utaalam wa gesi within the next 25 years;"
gfsonwinZinedine bandiko lako #273 limenifanya nijiulize maswali makuu mawili hivi kwanini Bgamoyo?? huwa najiuliza sana sipati jibu kabisa. bandari mpya ijengwe Bagamoyo, EPZE ijengwe bagamoyo, barabara ya kwenda kaskazini ijengwe bagamoyo, hospitali kuu ya mkoa wa pwani ijengwe bagamoyo. hvi huko bagamoyo kuna nini??
ile evenly distruibution ya resources ipo kweli?? mbona siskii maeneo mengine jamani?? mbona singida siiskii kabisa?? ama wao hawaaitaji kufaidika na uwekezaji?? mbona tabora nako ama wao wabaki na asali tuuuuuuuu ambayo hata mnunuzi wa uhakika hakuna??
hii nchi inahitajika mapinduzi ya kifikra ya kikweli kabisa vinginevyo kuna watao neemeka zaid na wengine wabaki maskini kabisa.
gfsonwin
Heshima kwako Mkuu,nimekusoma kwa utuvu wa hali ya juu katika hilo bandiko lako la juu lililojaa uchambuz wa kina na wa hali ya juu,mimi sina mengi sana ya kusema,
Kwani mengi yameshasemwa sana,kikubwa kilichopelekea kufikia hali hii ni kama hiko ulichokisema "USHIRIKISHWAJI WA WANANCHI KATIKA ENEO HUSIKA"
Wananchi ama watanzania wengi wao tumekosa matumain na iman na serikali yetu hata pale inapokuwa na nia njema wakati mwingine kutokana na kukosa kwao uwajibikaji na uzalendo katika kusimamia rasilimali za taifa na madudu yao viongoz na wataalamu wetu katika kuingia kwao mikataba mibovu mibovu inayoliingizia taifa hili hasara kubwa,madeni na ugumu wa maisha kwa wananchi wa kipato cha chini,
Usishangae sana hili la bagamoyo,kwani Huyu Mkuu wa nchi anachokifanya sasa ni kuvutia kwake,ni mwamba ngoma mwenye nguvu za ziada kwa sasa ndan ya taifa hili,na unyonge huu tulionao watanzania pamoja na kukosa kwa uzalendo kwa hao wanaomzunguka ndio kwa maana ngozi hii inawambwa kuelekea bagamoyo katika miaka miwili hii ya kumalizia muhula wake,
Potelea mbali na ni hasara yake yule Chinga Mkapa kama yeye alidhani kwamba JK akija atakuja kuendeleza Plan ya Mtwara Corridor kama alivyokaisisi yeye,hasara iyo kaipata yeye,JK anachofanya kwa sasa ni kuvutia kwake kwa nguvu zake zote ili apate cha kukumbukwa na wakwere wenzake,kwani anajua fika kwa watanzania amefeli na hakuna atakaemkumbuka kama atavyokumbukwa kwao...
Shukrani sana...
ndugu yangu na kaka yangu THE BIG SHOW shukrani za dhati zikufikie kwa kutoa maoni yako juu ya post yangu.
hapo bold pamenifanya niwaze kitu cha tofauti kabisa na hapa nitaomba mnisahihishe. Hivi kila rais anayekuja madarakani huwa anakuja na priorities zake sio??Lakini je huwa hatakiwi pia kuvipa vipaumbele miradi iliyo asisisiwa na seniour wake??
nashindwa kuelewa na niliposoma bandiko lako #266 niliogopa kuuliza hivi ni ipi sababu ya Mtwara corridor kutokuisha??
sijui kama rais anapokuja madaraka huwa anakuja na washauri wapya kama ndivyo basi nisishangae kuona Mtwara corridor haijaisha, lakini kama washauri wa raisi hubaki wale wale nikiwa namaana kwamba ni watu wanaoajiriwa na katibu mkuu kiongozi sion sababu ya watu hawa kuwa waoga kumshauri rais juu ya kumalizia miradi iliyoachwa pending
lakini pia hebu tuhoji hizi Ilani za uchaguzi ambazo vyama vya siasa huwa inazitoa je huwa zina lenga nini hasa?? manake kwa staili ya utendaji wa serikali iliyko madarakani napata picha kwamba ilani hizi ni political themes ambazo ni ngumu kuwa implimented na hivyo kumfanya rais awajibike pasi action plan.
sasa kama kikwete anaondoka mwaka keshokutwa inamana hilo swala la bandari ya bagamoyo litafia hapo sio?? na mradi wa EPZE nawenyewe sio?? haya sasa ndio matumizi mabaya ya madaraka ya rais. ndo maana napenda hata kwenye katiba mpya tumpunguzie madaraka rais na action plan awe anapewa na katibu mkuu kiongozi na sio na chama chake.
Zinedine bandiko lako #273 limenifanya nijiulize maswali makuu mawili hivi kwanini Bgamoyo?? huwa najiuliza sana sipati jibu kabisa. bandari mpya ijengwe Bagamoyo, EPZE ijengwe bagamoyo, barabara ya kwenda kaskazini ijengwe bagamoyo, hospitali kuu ya mkoa wa pwani ijengwe bagamoyo. hvi huko bagamoyo kuna nini??
ile evenly distruibution ya resources ipo kweli?? mbona siskii maeneo mengine jamani?? mbona singida siiskii kabisa?? ama wao hawaaitaji kufaidika na uwekezaji?? mbona tabora nako ama wao wabaki na asali tuuuuuuuu ambayo hata mnunuzi wa uhakika hakuna??
hii nchi inahitajika mapinduzi ya kifikra ya kikweli kabisa vinginevyo kuna watao neemeka zaid na wengine wabaki maskini kabisa.