Mkuu Nguruvi3, hongera sana kwa kazi pevu ya kuichambua na kuijadili rasimu ya katiba; kabla sijaenda mbali, ningependa kujua - je, ni sahihi kwamba washiriki wa muungano ni Tanzania Bara na Zanzibar?
Kwanini isiwe Tanganyika na Zanzibar? Kwa maana nyingine, serikali ya tatu inayopendekezwa ni ya Tanzania bara au Tanganyika?
Serikali ya Tanganyika in practice imeendelea kuwepo tangia muungano uanzishwe 1964 na imekuwa ikongozwa na rais wa JMT; Kwa maana nyingine, mambo yote yasiyokuwa ya muungano (ya TANGANYIKA)yamekuwa chini ya rais wa JMT kwa miaka 49 huku pia akisimamia masuala ya muungano; nachojaribu kueleza hapa ni kwamba kuna kiini macho cha miaka 49 cha serikali tatu huku rais wa JMT akiwa ni kiongozi wa Tanganyika ambayo anaitumia kuongoza serikali ya muungano na ya zanzibar kwa gharama kubwa sana; baada ya wajanja kuliona hili, kiini macho sasa kinapatiwa ufumbuzi lakini kwa kuendelea kumkataa mzazi wa Tanzania (Tanganyika) kama serikali kamili kama alivyotambulika chini ya hati na sheria ya muungano, na badala yake anaitwa Tanzania bara chini ya katiba mpya, jina ambalo Tanganyika alibatizwa rasmi chini ya katiba ya 1977; Kwanini basi na zanzibar asiitwe Tanzania visiwani, ili awe sawa na mwenzake Tanzania bara?
Hauwezi mwacha mzazi mmoja wa 1964 aendelee na jina lake (Zanzibar) huku mzazi mwenza (Tanganyika, yeye akibatizwa jina lipya la Tanzania bara;Zanzibar chini ya katiba ya JMT 1977 walifutwa na kupewa jina jipya - Tanzania visiwani lakini wakagundua kiini macho husika na kupigania jina lao lirudi kwa mujibu wa katiba kwani lina implications kubwa katika kujitawala kisiasa, na kiuchumi na kijamii; Inawezekana sijaeleweka katika hoja yangu hii lakini kwa mwelewa, suala hili lina implications na pia complications kubwa sana kwa suala zima la serikali tatu ijayo; nauliza tena, rasimu ya katiba inatambua washiriki wa muungano kama zanzibar na Tanzania bara? Kama ni sahihi, basi hili ni tatizo kubwa, hatuta tatua kero za muungano zilizopo bali kuhairisha tu matatizo;