Hili la kuahirisha uchaguzi haliwezi kufanyika mpaka katiba ya sasa ibadirishwe ili kuongeza possibilibility ya raisi kuongoza katika circumstance za aina hii. Isitoshe kama unaweza kuextend Utawala wa CCM bila kulazimika kupigiwa kura ni sawa sawa na umempa Fisi bucha akulindie, kwa sababu bila ya uchaguzi mpya CCM watabaki na wingi wao, na still nao wakiamua kukwamisha katiba mpya wanaweza, na kwa kuwa hutaki uchaguzi unakuwa huna leverage yoyote dhidi yao kwa kuwa CCM watakuwa hawana cha kuogopa!!
Tukiangalia trend ya taasisi za kijamii kati ya wale 201 ambao wengi miongoni mwao waliobaki bungeni, na pia tukiangalia viongozi wa madhehebu yenye watu wengi ikiwemo Bakwata, Catholics, Lutheran na wengineo, wapo Upande wa CCM. hawa nyuma yao wana watu wanaowasikiliza sana na ni base nzuri sana ya kura kwa CCM iwapo Ukawa wataendelea na siasa zao za kimatukio katika suala hili la katiba.
Kama alivyojadili
Nguruvi3 Hapa na kwingineko,Katiba iliyopo haina uhalali tena kisheria na kisiasa. Katiba iliyopo inaendelea kuitambua Zanzibar kama "sehemu ya jamhuri ya muungano". Katiba hiyo pia inaelekeza serikali ya mapinduzi ya zanzibar kutekeleza kazi na majukumu yake kwa mujibu wa masharti ya katiba hiyo ya JMT (1977) pamoja na katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984. Tukizidi angalia kwa undani, katika ibara ya 103(2) ya katiba hii ya Jamhuri ya Muungano inasema hivi:
"Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kabla ya kushika madaraka yake ataapa mbele ya Jaji Mkuu wa Zanzibar kiapo cha kulinda Katiba ya JAMHURI YA MUUNGANO na kiapo kingine kingine chochote kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar kinachohusika na uutendaji wake.
Kiongozi wa Zanzibar atashika na kutekeleza madaraka hayo kwa mujibu wa masharti ya katiba hii na Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984."
Ni katiba hii hii Kinana na Nape miezi kadhaa iliyopita Walisema Kwamba haina haja ya kubadilishwa. Tunashangaa kinana anatafuta nini Dodoma kwenye vikao vya maridhiano. Katiba Aliyosema kinana Kwamba haina haja ya kubadilishwa, haina ubavu tena mbele ya Katiba ya Zanzibar.
Kinana na nape baadae wakaenda znZ Kujibu mapigo ya ukawa waliotoka bungeni. Umati wa wananchi waliojitokeza kuwasikiliza akina kinana na nape uliwaona viongozi Hawa sio lolote zaidinyabwageni kutoka nchi jirani ya Tanganyika. Kwani Katiba ya Zanzibar, ambayo katiba ya kina Nape (JMT 1977) inasema kwamba Zanzibar ni "sehemu ya jamhuri ya muungano", inatamka wazi kwamba "Zanzibar ni Nchi". Katiba ya Zanzibar (tofauti na ile iliyopigiwa debe na kinana na nape) inasema kwamba "Mipaka ya taifa la zanzibar ni eneo lote la visiwa vya unguja na pemba, pamoja na visiwa vidogo vilivyoizunguka, bahari yake ambayo kabla ya kuundwa kwa jamhuri ya muungano, ikiitwa Jamhuri ya watu wa Zanzibar". Ibara ya kwanza ya Katiba ya Zanzibar inaweka wazi kwamba:
"Zanzibar ni miongoni mwa nchi mbili zinazounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania."
Nchi ya pili ni ipi? Akina Nape, Wassira, Sitta na kinana hadi leo hawana majibu.
Tukiangalia masharti haya ya katiba ya zanzibar, tunaona wazi kwamba yanaenda kinyume na matakwa ya katiba ya kina nape (JMT 1977), katika ibara yake kwa kwanza ambayo inaendelea kutamka wazi kwamba:
"Tanzania ni nchi moja na ni Jamhuri ya Muungano"
Tukienda kwenye ibara ya 33(2) ya katiba ya kina nape (JMT 1977) inasema kwamba:
"Rais wa Jamhuri ya Muungano Ndiye Mkuu wa nchi, Kiongozi wa serikali na Amiri Jeshi Mkuu."
Kifungu hiki kinapingana na ibara ya 26 ya katiba ya zanzibar ambacho kinatamka kwamba:
"Rais wa Zanzibar ni mkuu wa nchi ya Zanzibar".
Tukienda kwenye ibara ya 2(A) ya katiba ya Zanzibar, inatamkwa kwamba, kwa ajili ya utekelezaji bora wa shughuli za serikali, rais aweza kuigawa Zanzibar katika mikoa, wilaya na maeneo mengineyo kwa kufuata utaratibu uliowekwa na sheria iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi.
Masharti haya yanaenda kinyume na katiba ya kina Nape ambayo katika ibara ya 2(2) inasema kwamba:
"kwa ajili ya utekelezaji bora wa shughuli za serikali ya Jamhuri ya Muungano au Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar, rais aweza kuigawa Jmahuri ya Muungano katika mikoa, wilaya na maeneo mengineyo kwa kufuata utaratibu uliowekwa na sheria iliyotungwa na Bunge"
Maswali kwenu nyinyi CCM conservatives:
Tutaingia vipi Katika uchaguzi mkuu mwakani na Madudu haya?
Je kutakuwa maridhiano mapema baina ya ukawa na CCM lakini pia baina ya CCM na waandaaji wa katiba ya Zanzibar 2010?
Rais Kikwete miezi kadhaa iliyopita Alitamka Kwamba kuba uwezekano wa katiba ya sasa kuendelea kutumika katika uchaguzi mkuu ujao (2015). Sina uhakika Kama chama cha mapinduzi kinajua au Kinajali Kwamba iwapo uchaguzi utafanyika chini ya katiba ambayo itaendelea kupingana na katiba ya znZ,Rais ajaye (2015) ataingia madarakani huku madaraka yake yakiwa yameporwa na katiba ya zanzibar (2010).
Tatizo lililopo ambalo Wanasiasa wababe ndani ya CCM - Wassira, nape, Sitta aidha hawalijui au wanalipuuza ni kwamba - Katiba ya JMT na Katiba ya Zanzibar zina hadhi zinazopishana. Katiba ya JMT inatakiwa isomwe na kuendana pamoja na katiba ya Zanzibar, sio vinginevyo. Hivyo ndivyo muungano baina ya Zanzibar na Tanganyika unapotimia. Lakini kwa hali ya sasa, Ni kama vile katiba ya muungano haipo tena. Katiba hii imevunjwa, imefukiwa, hivyo kutubakisha na muungano wa maneno na mazoea tu. Vinginevyo muungano umeshatoweka.
Conservatives na wababe ndani ya CCM wanasahau jambo moja muhimu sana, nalo ni kwamba, tukiingia katika uchaguzi mkuu ujao chini ya katiba ya JMT inayopingana na Ile ya znZ, uwezekano wa kutokea mgogoro wa kikatiba na hata machafuko ni mkubwa.
Upo uwezekano wa serikali ya Jamhuri ya Muungano kushindwa kufanya uchaguzi mwakani (2015). Hii ni kwa sababu Rais ajaye bila ya kujalisha atatokea chama gani cha siasa, hatoweza kula kiapo kuilinda katiba ambayo tayari inakinzana na katiba ya nchi jirani ya Zanzibar.
Kwa mfano - Rais wa Muungano atatakiwa kuapa kuilinda katiba kwa sababu yeye ndiye mkuu wa nchi, Kiongozi wa serikali na amiri jeshi mkuu, lakini kwa upande wa zanzibar pia, Katiba yake inamtambua Rais wa Zanzibar kama mkuu wa "nchi" ya Zanziba na mkuu wa majeshi ya serikali ya mapinduzi.
Kutokana na mkinzano huu, itakuwa ni vigumu sana kwa uchaguzi mkuu ujao kufanyika bila ya aidha katiba ya
Zanzibar kufanyiwa marekebisho irudi katika hali yake ya kabla ya 2010, au Katiba ya JMT (1977) ifanyiwa marekebisho kukidhi haja za Zanzibar.
Lakini sote tunajua kwamba: Hakuna kiongozi yoyote wa CCM ambaye anaweza irudisha zanzibar nyuma. Hii ni kwasababu wazanzibari walishaamua kupitia kura ya maoni. Na ili zanzibar iweze kufanyia katiba yake mabadiliko itahitaji tena theluthi mbili ya kura ya maoni jambo ambalo halitatokea.
Lakini vilevile, kuirekebisha katiba ya JMT iendane na mabadiliko ya katiba ya zanzibar (2010) ni kuvunja muungano kwa mlango wa nyuma. Hii ni kwa sababu serikali mbili "zilizoboreshwa" ni suala ambalo halita tekelezeka, sana sana litazidisa migogoro na kero kwa pande zote mbili za muungano, na hatimaye kuvunja muungano.
CCM inaweza kufanikiwa kuwa at an advantage iwapo bunge la katiba litavunjwa, lakini mafanikio hayo yatakuwa "short lived" kwani hayatajibu sehemu kubwa ya kero za muungano za zaidi ya miaka 30 zinazotishia uhai wake. Sana sana, CCM kupitia kina Kinana, Wassira, lukuvi, Sitta, Nape watatumia fedha za walipa kodi wa Tanganyika kuwapa zanzibar kila watachotaka ili mradi tu waridhie serikali mbili zilizoboreshwa kuelekea uchaguzi mkuu ujao. Lakini Ukweli ni Kwamba Serikali hizi zitaishia kuzidi kuwaamsha watanganyika kutoka usingizini na kupelekea watanganyika kutambua jinsi gani serikali mbili zinavyowanyima haki yao kama mshirika wa pili wa muungano. Hali hii itajenga chuki kubwa baina ya wananchi wa pande zote mbili ambapo kwa upande wa zanzibar, serikali mbili zilizoboreshwa zitawapa mamlaka kwa mkono wa kulia na kuwapokonya kwa mkono wa kushoto na kwa upande wa watanganyika, gharama za kubeba nchi jirani badala ya kodi zao kutumika katika huduma za kijamii na kiuchumi kupitia Tanganyika as a subnational government kama ilivyo kwa SMZ ni suala ambalo litawasukuma wananchi wa upande wa bara kudai Tanganyika yao. Kitendo cha ccm kuwakatalia Haki yao hii ya kikatiba kitapelekea muungano kuvunjika.
Mwisho - ingawa Mkinzano uliopo kikatiba utaweza pelekea kutofanyika kwa uchaguzi wa serikali ya Jamhuri ya Muungano, chini ya katiba ya zanzibar (2010), nchi hii jirani haita athirika na hali hii. Kwa maana nyingine, uchaguzi wa Serikali ya muungano unaweza kukwama iwapo mabadiliko ya kikatiba hayata tokea, lakini hali hii haitazuia nchi jirani ya zanzibar kufanya uchaguzi wake mwakani (2015). Hii ni kwa sababu, ukitazama katiba ya Zanzibar katika ukurusa wa 17-18, inajadili ukomo wa rais na sababu za kushindwa kufanyika kwa uchaguzi mkuu zanzibar. Ibara ya 29 ya katiba hiyo inatamka kwamba:
"Ikiwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imo katika VITA na ikiwa Rais anaona kuwa ni muhimu kuzuia uchaguzi, baraza la wawakilishi linaweza kupitisha azimio, kuzidisha muda wa miaka mitano uliotajwa kwenye kijifungu (2) cha 28 katika kipindi hadi kipindi lakini hakutakwa na kipindi kitakachozidi miezi sita mfululizo.".
Kwa maana hii, iwapo uchaguzi wa serikali ya muungano utakwama mwakani kwa sababu tulizojadili awali, Zanzibar wataendelea na uchaguzi wao, vinginevyo kukwama kwa uchaguzi wa serikali ya muungano kuambatane na "vita". Ukawa wajiadhari na kusingiziwa Kwamba ni chanzo cha vita na machafuko.
]
Sent from my iPhone using JamiiForums