Duniani tunapita tu

pwilo

JF-Expert Member
May 27, 2015
10,098
12,473
Ikiwa imebaki siku moja kabla ya kuingia mwaka 2024 na kuuaga mwaka 2023 kwangu mimi naweza kusema mwaka 2023 ulikuwa mzuri na ulikuwa na maumivu pia ndani yake.

UZURI.
mwaka 2023 nilibahatika kuoa baada ya kusua kusua na familia kupiga kelele kwa mda mrefu nikaamua kuo siwezi sema nilishinikizwa ila nilikuwa nishajipanga sema kuna mambo tu hayakukaa sawa ya kikazi ndio ilikuwa kikwazo.

Niliamua kuanza maisha mapya na mpaka sasa tunaendelea vizuri na mke wangu na mungu akijalia mwakani tunatarajia mtoto. Ilikuwa furaha kwa familia ndugu na marafiki lakini hasa wazazi wangu akiwemo mama yangu mzazi baba yangu mzazi pamoja na bibi na babu yanga na ndugu zangu wakizaliwa tumbo moja.

Sikutaka harusi ya gharama na niliwaambiwa nyumbani wafanye sherehe ya kawaida na hata michango sikuchangisha kwasababu nilikuwa sitaki harusi ya show off lakini familia na ndugu walikataa wakasema mimi nitulie niwaachie wao swala hilo mimi nisubirie kuchukua mke tu hakika harusi ilifanya licha ya kutotaka michango na kuchangisha hela ila marafiki zangu na ndugu walipopata taarifa walinipigia simu wakilalamika kwa nini sijawaambia mapema na wengine kuahidi kunichangia kidogo walichojaaliwa na kweli walifanya hvyo.

Harusi ilifanyika kwa siku tatu siku ya kwanza ilikuwa maulidi siku ya pili ilikuwa mziki siku ya tatu ilikuwa after party kwa kweli ndugu na familia walifurahi sana na hata mimi nilifurahi sana hasa baada ya marafiki zangu ambao tulikuwa na kusoma pamoja kujitokeza licha ya kutowasiliana kwa mda mrefu nilifurahi sana nikikumbuka ile misafara ya boda boda na magari kwakweli ilikuwa siku ya furaha sana.

HUZUNI.
Mzee wangu alikuwa anaumwa mda mrefu sana alikuwa anasumbuliwa na sukari na moja kati ya kauli zake ilikuwa ananiambia mwanangu fanya uoe au unataka mpaka wazazi wako tufariki ni moja kati ya kauli ambayo naikumbuka mpaka leo hii. Mimi naishi mbali na familia hivyo baada ya harusi tukaagana na kupeana mikono kumbe ilikuwa ndio tunaagana.

Ni miezi miwili sasa baada ya mzee kutangulia mbele ya haki mungu amlaze mahala pema maana alichokitaka kwa mda mrefu alikishuhudia.

Pumzika kwa amani mzee wangu.
 
Ikiwa imebaki siku moja kabla ya kuingia mwaka 2024 na kuuaga mwaka 2023 kwangu mimi naweza kusema mwaka 2023 ulikuwa mzuri na ulikuwa na maumivu pia ndani yake.

UZURI.
mwaka 2023 nilibahatika kuoa baada ya kusua kusua na familia kupiga kelele kwa mda mrefu nikaamua kuo siwezi sema nilishinikizwa ila nilikuwa nishajipanga sema kuna mambo tu hayakukaa sawa ya kikazi ndio ilikuwa kikwazo.

Niliamua kuanza maisha mapya na mpaka sasa tunaendelea vizuri na mke wangu na mungu akijalia mwakani tunatarajia mtoto. Ilikuwa furaha kwa familia ndugu na marafiki lakini hasa wazazi wangu akiwemo mama yangu mzazi baba yangu mzazi pamoja na bibi na babu yanga na ndugu zangu wakizaliwa tumbo moja.

Sikutaka harusi ya gharama na niliwaambiwa nyumbani wafanye sherehe ya kawaida na hata michango sikuchangisha kwasababu nilikuwa sitaki harusi ya show off lakini familia na ndugu walikataa wakasema mimi nitulie niwaachie wao swala hilo mimi nisubirie kuchukua mke tu hakika harusi ilifanya licha ya kutotaka michango na kuchangisha hela ila marafiki zangu na ndugu walipopata taarifa walinipigia simu wakilalamika kwa nini sijawaambia mapema na wengine kuahidi kunichangia kidogo walichojaaliwa na kweli walifanya hvyo.

Harusi ilifanyika kwa siku tatu siku ya kwanza ilikuwa maulidi siku ya pili ilikuwa mziki siku ya tatu ilikuwa after party kwa kweli ndugu na familia walifurahi sana na hata mimi nilifurahi sana hasa baada ya marafiki zangu ambao tulikuwa na kusoma pamoja kujitokeza licha ya kutowasiliana kwa mda mrefu nilifurahi sana nikikumbuka ile misafara ya boda boda na magari kwakweli ilikuwa siku ya furaha sana.

HUZUNI.
Mzee wangu alikuwa anaumwa mda mrefu sana alikuwa anasumbuliwa na sukari na moja kati ya kauli zake ilikuwa ananiambia mwanangu fanya uoe au unataka mpaka wazazi wako tufariki ni moja kati ya kauli ambayo naikumbuka mpaka leo hii. Mimi naishi mbali na familia hivyo baada ya harusi tukaagana na kupeana mikono kumbe ilikuwa ndio tunaagana.

Ni miezi miwili sasa baada ya mzee kutangulia mbele ya haki mungu amlaze mahala pema maana alichokitaka kwa mda mrefu alikishuhudia.

Pumzika kwa amani mzee wangu.
Kweli Binadamu tunapita, ila naomba vile tulivyovikuta hapa duniani "mali/ukwasi" vipitie kwangu kabla ya mimi kupita duniani.
 
2023 ni mwaka wa baraka kwa wapalestina kuuawa zaidi ya elfu 23 wengi wao watoto na wanawake. Na labda idadi itaongezeka ikapita elfu 25 inshallah.

Kwa upande mwengine 2023 ulikuwa mwaka wa huzuni. Maelfu na maelfu ya watoto na wanawake waafrika weusi waislam Darfur Sudan wameuwawa na waislam wenzao waarabu na hakuna yoyote ameandamana na kuilaani mauaji hayo.

JUSTICE FOR JOSHUA AND CLEMENCE.

Sir
robert Kennedy Bwana Utam baba-mwajuma ITR incharge Alwaz green rajab Ritz FaizaFoxy Accumen Mo Kambaku 100 others
 
Back
Top Bottom