Duniani tuko kwa ajili gani ............

Duniani tuko kwa ajili gani ............

sandpiper

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2018
Posts
209
Reaction score
186
Ingawa kuna majibu mengi sana kuhusiana na maisha yetu hapa Duniani. Kuna mengi tunayoweza kujifunza kwa mfano kuna mtu aliyejlikana kama Steve Paul Jobs wakati akiwa kitandani kwa ugonjwa wa kansa aliacha usia huu;
Nimefika kwenye kilele cha mafanikio kweye ulimwengu wa biashara . Kwa mtizamo wa wengine maisha yangu wanayatamani kuyaishi.
Lakini Zaidi ya kazi , nina furaha kidogo sana , Mwisho wa maisha utajiri ni hali tu ya maisha niliozoea
Kwa wakati huu , nikiwa nimelala kwenye kitanda cha wagonjwa na kukumbuka maisha yangu yote , nimegundua kwamba kujulikana kwangu na utajiri nilionao vitu ambavyo nilijivunia vimepauka na vimekuwa havina maana yoyote kwenye hali hii ya kuwa marehemu mtarajiwa.
Kwenye giza hili , nikiangalia taa za kijani kutoka mashine za kunisaidia kuhema na nasikia mvumo wa sauti wa mashine ukilia , Nahisi pumzi za izraili akiwa ananisogelea….
Sasa najua , tukishajikusanyia utajiri wa kutosha kwenye maisha yetu , tunatakiwa kuanza kutafuta vitu vingine ambavyo havina uhusiano na utajiri.
Inatakiwa kitu ambacho kina umuhimu Zaidi,
Labda mahusiano, au Sanaa au hata ndoto zako ulivyokuwa kijana.
Kutafuta utajiri bila kuchoka kutakufanya uwe mtu alie wa ajabu kituko kama mimi.
MUNGU ametupa hisia tuweze kuhisi upendo moyoni na sio ubatili unaoletwa na utajiri
Utajiri wangu niliopata kwenye maisha siwezi kwenda nao huko kuzimu, ninachoweza kwenda nacho ni kumbukumbu tu iliosababishwa na upendo
Huo ndio utajiri wa kweli utakaokufata , kukupa kampani , kukupa nguvu na mwanga wa kuendelea mbele.
Upendo unaweza kusafiri maelfu ya kilometa , maisha hayana mpaka , nenda unapotaka kwenda , fikia kilele cha juu unachotaka , ni wewe tu vyote vipo mikononi mwako na moyoni mwako.

Kitanda gani unakilipia gharama kubwa kuliko vyote ?
Kitanda cha hospitalini…..
Unaweza kumuajiri mtu kukuendeshea gari , kukuzalishia pesa lakini hakika huwezi kumuajiri mtu kuumwa kwa ajili yako
Vitu vilivyopotea vinaweza kupatikana , lakini kuna kitu kimoja kamwe hakiwezi kupatikana kikipotea- Nacho ni uhai
Mtu akiwa anaenda kufanyiwa operesheni , atagundua kwamba kuna kitabu ambacho alitakiwa kukisoma nacho ni kitabu cha uzima
Hajalishi tuko kwenye hatua gani ya maisha kwa wakati huu , baada ya muda itabidi kukabiliana na ile siku ya mwisho wa maisha yetu
Thamini upendo kwa familia yako , upendo kwa mwenza wako na upendo kwa marafiki zako ,
Jipe raha mwenyewe huku ukithamini wenzako pia.

“I reached the pinnacle of success in the business world. In others’ eyes, my life is an epitome of success.
However, aside from work, I have little joy. In the end, wealth is only a fact of life that I am accustomed to.
At this moment, lying on the sick bed and recalling my whole life, I realize that all the recognition and wealth that I took so much pride in, have paled and become meaningless in the face of impending death.
In the darkness, I look at the green lights from the life supporting machines and hear the humming mechanical sounds, I can feel the breath of god of death drawing closer …
Now I know, when we have accumulated sufficient wealth to last our lifetime, we should pursue other matters that are unrelated to wealth …
Should be something that is more important:
Perhaps relationships, perhaps art, perhaps a dream from younger days
Non-stop pursuing of wealth will only turn a person into a twisted being, just like me.
God gave us the senses to let us feel the love in everyone’s heart, not the illusions brought about by wealth.
The wealth I have won in my life I cannot bring with me. What I can bring is only the memories precipitated by love.
That’s the true riches which will follow you, accompany you, giving you strength and light to go on.
Love can travel a thousand miles. Life has no limit. Go where you want to go. Reach the height you want to reach. It is all in your heart and in your hands.
What is the most expensive bed in the world?
Sick bed …
You can employ someone to drive the car for you, make money for you but you cannot have someone to bear the sickness for you.
Material things lost can be found. But there is one thing that can never be found when it is lost — Life.
When a person goes into the operating room, he will realize that there is one book that he has yet to finish reading — Book of Healthy Life.
Whichever stage in life we are at right now, with time, we will face the day when the curtain comes down.
Treasure Love for your family, love for your spouse, love for your friends.
Treat yourself well. Cherish others.”
 
Binadamu wakiwa hai huwa wanajisahau sanaa sanaa.. Ila ni vyemah sana kumkumbuka Mungu tukiwa hai na kuishi kwa kufata kanuni za Mungu... Mungu tusaidie..
 
Duniani tupo ili tuishi kwa furaha. Na hapa ndipo tatizo linapoanzia.kila mtu furaha anaitafsiri kwa namna yake.
 
Duniani tupo kwa ajili gani?
Ninavyoelewa kwa mazoeya yetu katika maisha Ni kuwa hakuna jambo/kitu kinachoweza kuwa bila ya kuwepo muwezeshaji. Gari, Ndege, Simu n.k vyote vina watengenezaji. Na kila mtengenezaji hutoa muongozo wa jinsi gani ya kukitumia kwa ufanisi kifaa alichokitengeza. Na baadhi ya wakati hao watengenezaji wanatuletea wataalamu ili waje kutufahamisha matumizi sahihi ya vifaa vyao na kufunza watu wengine katika jamii ili wakiondoka wao kuwepo watu wengine wa kuelekeza watu wao.
Mwanaadamu ni mbora zaidi kuliko vifaa anavyovitengeza. Kwa ubora wetu Mwenyezi Mungu anasema yeye ndiye aliyetuumba.
Tutathibitishaje kama Mwenyezi Mungu ndiye aliyetuumba. Tunathibitisha hilo kupitia vitabu vinne vitakatifu ambayo alituletea kupitia Wajumbe wake kwetu.
1. ZABURI - DAUDI (AS)
2. TAURATI - MUSSA (AS)
3. INJILI - ISSA (AS)
4. QURAN - MUHAMMAD (SAW)
Vitabu hivyo kama MTU atavisoma kwa makini na kutuliza ufahamu wake atabaini kuwa yupo Mungu Muumba wa ulimwengu na vilivyomo na vyote vinakwenda kwa muongozo wake. Mungu mmoja mwenye nguvu, asiyezaa wala kuzaliwa na hafanani na chochote.
Vitabu hivyo ndivyo vimeelekeza NINI LENGO LA SISI BINAADAMU KUWEPO HAPA DUNIANI.
...VITABU VINASEMA TUPO KWA AJILI YA "KUMUABUDU MUNGU MUUMBA'
KUABUDU MAANA YAKE NI KUTENDA NA KUACHA KUTENDA kwa mujibu ya muongozo wake. Nao unapatikana kupitia hivyo vitabu na mitume ndio wakwanza ku-practice hiyo miongozo na hoatoria zinathibitisha kuwa waliishi maisha mema, wakapenda nao kupendwa na wanajamii walioishi nao.
Wasalaam.
 
Steve Jobs alizaliwa February 24, 1955 na alifariki October 5, mwaka 2011. Ametoa mchango mkubwa sana kwenye maendeleo ya sayansi na technologia hasa computer
Je kweli huo wosia alioutoa ndiyo yalikuwa ni maneno yake ya mwisho, ama kilikuwa ni kiwewe tu cha maumivu na baadaye akaendelea kudunda hadi alipokuja kufa kivingine?
 
Je kweli huo wosia alioutoa ndiyo yalikuwa ni maneno yake ya mwisho, ama kilikuwa ni kiwewe tu cha maumivu na baadaye akaendelea kudunda hadi alipokuja kufa kivingine?
Baada ya maneno hayo alikuja kufa muda si mrefu baada ya kushindwa kupumua. Kansa ya kongosho ilikuwa imemmaliza kabisa. Ila cha muhimu ni somo tunalotakiwa kujifunza kwenye maisha yetu . Tuweke upendo mbele ya yote , tupendane sisi kwa sisi .Utakuta mtu anakiri kabisa kwamba anamchukia fulani bila hata sababu ya msingi. Love is easy but hate has a price . Haya maisha ni mafupi sana
 
Back
Top Bottom