SOCIOLOGISTTZ
JF-Expert Member
- Jun 16, 2013
- 2,615
- 929
Wote tunajua kwamba ndege ya Malaysia imepotea takrabani wiki mbili sasa na wala haijulikani mahali ilipo. Kuna juhudi mbalimbali za mataifa ya magharibi na mashariki yanaangaika kuitafuta lakini bila mafanikio. Kwa sasa mimi kama mwananchi wa dunia ya tatu au nchi zinazoendelea nimejiuliza maswali mengi sana;
- 1. Kama nchi zilizoendelea zimeshindwa kuipata hiyo ndege duniani kuna usalama gani? Hapa ina maana kwamba nchi zilizoendelea zimejiimarisha zaidi kiteknolojia, wameweka rada na setelaiti kila mahali hasa kwenye anga za juu ili waone kila kitu kinachoendelea duniani.
- 2. Sasa dunia tujue lipi? Abiria wapo hai au wamekufa? Kama wamekufa maiti zao ziko wapi?
- 3. Malaysia ni nchi ambayo imepiga hatua sana katika maendeleo ijapokuwa kwenye miaka ya 1960 ilikuwa karibu sawa na Tanzania, hata matokeo makubwa sasa (the big results now) Tanzania iliiga kwao, sasa na wao walifanya juhudi gani kuhakikisha usalama wa abiria na mali zake? Kwani hawakujua hujuma zilizokuwepo kabla (if any)? Au wanategemea mataifa ya magharibi yaangalie usalama wao?
- 4. Nchi za dunia ya tatu ikiwemo Tanzania tumejifunza nini kutokana na mkasi huu? Kuna haja ya kuendelea kuzitegemea tena nchi za magharibi kwenye maswala yetu mbalimbali ikiwamo maswala ya ulizi na usalama?
- 5. Je Tanzania ni salama kwa Utegemezi wa Marekani?