Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 359,959
- 828,683
Wahenga wanasema kwa mwoga kilienda kicheko kwa shujaa kilienda kilio. Maana yake ni nini?
Ni usemi wa vitani wakati wa mapigano. Mwoga alijificha nyuma ya wenzake hakwenda mstari wa mbele kwenye hatari zaidi ya kufa. MWOGA SI MZALENDO.
Shujaa yeye kwa moyo mmoja alienda mstari wa mbele akapambana na adui kwa maslahi ya nchi na taifa lake. Lakini katikati ya mapambano makali adui akamuwahi na risasi moja na kummaliza.
Majeshi yaliporudi nyumbani. Kwa mwoga kulienda kicheko na chereko kwakuwa hakufia vitani na karudi kuungana tena na familia yake. Kwa shujaa kulienda kilio kwakuwa shujaa alifariki kwenye mapigano na familia yake ikakabidhiwa mwili wa mpendwa wao.
Maisha yana pande mbili. Daima kila mmoja wetu ana upande wake. Unaweza kuchagua upande wa MWOGA lakini uishi kwa aibu ama uchague upande wa SHUJAA ili ufe with DIGNITY.
Kwa fisadi kulienda kicheko. Kwa MZALENDO kulienda HESHIMA. KESHO NI KUBWA KULIKO LEO
Ni usemi wa vitani wakati wa mapigano. Mwoga alijificha nyuma ya wenzake hakwenda mstari wa mbele kwenye hatari zaidi ya kufa. MWOGA SI MZALENDO.
Shujaa yeye kwa moyo mmoja alienda mstari wa mbele akapambana na adui kwa maslahi ya nchi na taifa lake. Lakini katikati ya mapambano makali adui akamuwahi na risasi moja na kummaliza.
Majeshi yaliporudi nyumbani. Kwa mwoga kulienda kicheko na chereko kwakuwa hakufia vitani na karudi kuungana tena na familia yake. Kwa shujaa kulienda kilio kwakuwa shujaa alifariki kwenye mapigano na familia yake ikakabidhiwa mwili wa mpendwa wao.
Maisha yana pande mbili. Daima kila mmoja wetu ana upande wake. Unaweza kuchagua upande wa MWOGA lakini uishi kwa aibu ama uchague upande wa SHUJAA ili ufe with DIGNITY.
Kwa fisadi kulienda kicheko. Kwa MZALENDO kulienda HESHIMA. KESHO NI KUBWA KULIKO LEO

