Duni Hajji ashindwa kusuluhisha UKAWA - Mtama

Duni Hajji ashindwa kusuluhisha UKAWA - Mtama

Livejr

JF-Expert Member
Joined
Feb 6, 2014
Posts
2,073
Reaction score
2,812
Kufuatia ziara za mgombea mwenza mikoa ya kusini Lindi na Mtwara asubuhi ya leo amekutana na kizingiti baada ya kushindwa kutoa ufafanuzi nani awe mgombea kupitia UKAWA baada ya CHADEMA na CUF kila mmoja kusimamisha mgombea jimboni hapo.

CHADEMA imemsimamisha Ndg Selemani Methew Luwongo ambaye alikosa nafasi hiyo kupitia CCMna wakati huo huo Chama cha Wananchi CUF kimemsimamisha ndg Isihaka Mchinjita.

Hali hiyo imejitokeza leo asubuhi wakiwa kwenye vikao vya ndani ambapo wagombea Ubunge kila mmoja yeye anaweza kupambana na Nape, kwenye mkutano uliofaonyika baada ya vikao vya ndani Duni Hajji alishindwa kumtangaza mgombea kupitia UKAWA hali ambayo imepelekea kuwagawa watu wa Ukawa kuhusu nani wampigie Kura oktoba Kati ya hao wawili.

Hali hii ikiendelea namuona Nape akichukua jimbo kabla ya saa mbili asubuhi.

Nb: Jimbo la Mtama lipo chini ya CUF kwenye mgawanyo wa majimbo wa UKAWA.
 
Chadema are in dilemma as awareness of Fisadi is becoming more conspicuous and irreputable.
 
Kuna makosa ya kiufundi hapo Mtama. Viongozi wana tatizo sio wananchi.
 
Chadema are in dilemma as awareness of Fisadi is becoming more conspicuous and irreputable.
Rep power: 0, need I say more? If only idiocy was painful...
 
Hii ya kuachiana majimbo ni mtahani mkubwa ambao ukawa wamejitahidi na jitihada zimeonekana

Hakuna jimbo lilikuwa mtihani kama segerea kwa mtatiro
 
Huyo Mathew ana nguvu sana hapo wangemuachia tu, wangeulizwa wana ukwa wa hapo wenyewe
 
Ukawa tunaomba mjipange kwanza mpaka 2020 ndio tutawafikiria kwa sasa hamjajipanga kuingia Ikulu
 
Hii ya kuachiana majimbo ni mtahani mkubwa ambao ukawa wamejitahidi na jitihada zimeonekana

Hakuna jimbo lilikuwa mtihani kama segerea kwa mtatiro

Hivi jana uliangalia taarifa ya habari mbona yule dada amejitokeza tena kwamba lile ni jimbo lake
 
Ccm mnajitahidi kutushauri na kutufuatilia asanteni sana, kumbukeni na kumnadi mgombea wenu
 
Rep power: 0, need I say more? If only idiocy was painful...

Ulitakiwa kuonyesha jinsi hoja yake haina mashiko.
Hatuko kwenye mashindano ya rep power..
Kwa hiyo ukiwa ana rep power kubwa ndo tukukubalie vitu vya kizushi au visivyokuwa na matiki?
Hoja inatenguliwa kwa hoja sio rep power....
 
Mtwara mjini!!!!

Masasi!!!!!!

Nanyumbu!!!!

Mtama!!!!!

Tunasubiri suluhu siku ya uchaguzi
 
Ccm mnajitahidi kutushauri na kutufuatilia asanteni sana, kumbukeni na kumnadi mgombea wenu

Sio kila anayeshaur au kutoa hoja kuhusu Ukawa ni Ccm ungejaribu kufuatilia kama ni kweli au sio kweli ndio ujibu hivyo. Au haujui kuwa Duni yupo kusini kwenye kampeni..?
 
Huyo Mathew ana nguvu sana hapo wangemuachia tu, wangeulizwa wana ukwa wa hapo wenyewe

Hiv unafikiri unaweza kupima kukubakika kwa mtu kwenye kata moja Kati ya 20..? kama vikao vya ndani vimeshindwa itakuwaje kwa wanachama ambao wapo Ukawa..? Methew anawarubuni vijana wamzomee Mchinjita eti kisa amekataa kumuachia jimbo kupitia Ukawa anasahau kuwa wakati Mchinjita anajenga Upinzani Mtama Methew alikuwa yupo CCM.
 
Back
Top Bottom