LiverpoolFC
JF-Expert Member
- Apr 12, 2011
- 11,348
- 3,219
Nikiwa nyumbani nikiwa najiliwaza kwa hili na lile baada ya kutoka church,nikafungulia Radio One mambo mseto na ndipo nikapata kumsikiliza yule mtangazaji wa radio one toka Morogoro akitoa vihoja ya kweli toka huko mkoani Moro na akimimina aliyoyaona baada driver wa lori moja waliokuwa wanasafiri naye na konda wake kupaki na wakateremka kwenda kupata moja baridi na moja moto na ndipo walipomaliza na kurudi kwenye gari na kujaribu kuwasha bila ya mafanikio konda naye akajaribu kuwasha bila ya kuwaka na ndipo wakafikia maamuzi ya kumtafuta fundi naye akaja akajaribu kulikagua gari akasema haoni tatizo na ndipo wakabaki wakiduwaa bila ya kujua la kufanya na ndipo wakapiga simu kwa office na akaja fundi wa kampuni lengwa la gari naye akajaribu kulikagua naye haoni tatizo,na ndipo akagundua ya kwamba dereva na konda wake wote wamelewa na ndipo akaingia mwenyewe na kuliwasha na gari likakubali na safari ikaendelea. Swali! Mi nafikiri hilo gari ni la Kichina maana mtangazaji ajasema ni aina gani zaidi ya kusema lori,kwanini yasiletwe mengi hapa Nchi na ajali mbona ingepungua? Ama kama ni chombo cha kufunga kwenye magari,si ingefungwa ktk magari madogo na makubwa kana kwmb driver akigusa tu ingali amekunywa pombe na gari hata lisifunguke mlango licha ya kuwaka. Mi ningependa hili sana! Ni hayo tu wanaJF na niwatakieni J'pili njema. Source Radio One: