Dua nzito kwa shekh khassan makarama

Dua nzito kwa shekh khassan makarama

Joined
Dec 4, 2016
Posts
66
Reaction score
145
Naam tumemaliza salama lakini niwataarifu na niwaombe muhudhurie katika Dua itakayofanyika jumamosi hii ya tarehe 20/01/2018 ufanye huu mwaka kuwa ni mwaka wa mafanikio kwako kwa kutaka radhi za mola wako na baraka zake ktk maisha yako.Dua itafanyika katika viwanja vya Shekh Khassan Makarama bingwa Wa kutafsiri ndoto na nyota.Anapatikana Tanga mjini mtaa wa Mikanjuni kituo cha wapendanao
a25d7df642f7079fa9171f52ebe1efa3.jpg
.
7fffc6051bea4ee57a5dcf0dd56b630e.jpg
. Mawasiliano what up 0656228832 call0659130640
 
Acha kula Mali za watu kwa dhulma!! Dua'a ya kisharia ni surat fat'ha 7 , Surat nnasi 3,surat falaq 3 na ikhlaaswi 3!! wewe ni mpigaji mche Allah ni bora ukalichukua jembe lako ukaenda lima mpunga kuliko kuibia watu kwa mgongo wa dini
 
Na hizo picha za wamama wa kiislamu zitoe Kwenye tangazo lako la biashara!! Hili ni tangazo la biashara!! Acha kudharirisha mama na dada zetu wakiislam!
 
Daaah... Astaghfir ! Naona mnaigiza mila za Wagalatia. Kwanza calendar husika haifuatwi na ulimwengu wa kiislaam
 
Ndugu yetu Kaka Hassan Kamara mche mola wako. Sina uhakika na usahihi wa unachokifanya, bali namili zaidi kusema ni makosa kisheria. Kwanza ilmu ya nyota haina asli kutoka kwa mtume sala na salam zimfikie bali ni ilmu ya makuhani na hata amesema mwanazuoni Al kahtwani katika nuniya yake علم النجوم وعلم شرع محمد في قلب رجل واحد ليس يجتمعان akimaanisha elimu ya nyota na ilmu ha sheria ya muhammad hazikutani katika moyo wa mtu mmoja. Hivyo eidha mtu awe kuhani au awe shekh aliesoma ilmu ya sheria ya muhammad ili aweze kuunufaisha ummah.
Jambo lingine kuna namna ya kujizakkiy katika tangazo lako kwanza mtu kujiita Shekh ni katika kujitukuza na hilo pia kosa kubwa tu bali ikifikia mtu kujiita shekh tayar ameshakosa sifa hiyo maana mashekh ni wenye kumcha Allah zaidi na wenye kuumcha Allah zaidi hawasifiki na kujitukuza
 
Jumamosi Dua nzito na visomo mbali mbali tukutane pale pale kwa Shekh Khassan Makarama Tanga Mikanjuni kituo cha wapendanao
 
Ndugu yetu Kaka Hassan Kamara mche mola wako. Sina uhakika na usahihi wa unachokifanya, bali namili zaidi kusema ni makosa kisheria. Kwanza ilmu ya nyota haina asli kutoka kwa mtume sala na salam zimfikie bali ni ilmu ya makuhani na hata amesema mwanazuoni Al kahtwani katika nuniya yake علم النجوم وعلم شرع محمد في قلب رجل واحد ليس يجتمعان akimaanisha elimu ya nyota na ilmu ha sheria ya muhammad hazikutani katika moyo wa mtu mmoja. Hivyo eidha mtu awe kuhani au awe shekh aliesoma ilmu ya sheria ya muhammad ili aweze kuunufaisha ummah.
Jambo lingine kuna namna ya kujizakkiy katika tangazo lako kwanza mtu kujiita Shekh ni katika kujitukuza na hilo pia kosa kubwa tu bali ikifikia mtu kujiita shekh tayar ameshakosa sifa hiyo maana mashekh ni wenye kumcha Allah zaidi na wenye kuumcha Allah zaidi hawasifiki na kujitukuza
Tukutane katika Dua nzito siku ya jumanosi hii karibu
 
Acha kula Mali za watu kwa dhulma!! Dua'a ya kisharia ni surat fat'ha 7 , Surat nnasi 3,surat falaq 3 na ikhlaaswi 3!! wewe ni mpigaji mche Allah ni bora ukalichukua jembe lako ukaenda lima mpunga kuliko kuibia watu kwa mgongo wa dini
Nashkuru kuona ni msomaji wa posti zangu karibu katika Dua nzito na visomo vikali vya majini
 
Acha kula Mali za watu kwa dhulma!! Dua'a ya kisharia ni surat fat'ha 7 , Surat nnasi 3,surat falaq 3 na ikhlaaswi 3!! wewe ni mpigaji mche Allah ni bora ukalichukua jembe lako ukaenda lima mpunga kuliko kuibia watu kwa mgongo wa dini
Unawasaidiaje wasiojua kusoma hizo sura.Usikurupuke kuna watu hawakusoma kama wewe hivyo hawajui kama wewe lakini karibu katika Dua.Wakati we unapiga kelele kama hizi Mimi naendelea kuwasaidia watu
 
wewe ni jahil muraqqabu, Acha wizi bora kulima kuliko kuishi kwa ujanja...
ﺑَﺎﺏُ ﻣَﺎ ﺟَﺎﺀَ ﻓِﻲ ﺍﻟْﻜُﻬَّﺎﻥِ ﻭَﻧَﺤْﻮِﻫِﻢْ
Kuhusu Makuhani Na Mfano Wao
ﺭَﻭَﻯ ﻣُﺴْﻠِﻢٌ ﻓِﻲ ﺻَﺤِﻴﺤِﻪِ ﻋَﻦْ ﺑَﻌْﺾِ ﺃَﺯْﻭَﺍﺝِ ﺍﻟﻨَّﺒِﻲِّ ‏( ﺻَﻠَّﻰ ﺍﻟﻠَّﻪُ ﻋَﻠَﻴْﻪِ ﻭَﺳَﻠَّﻢَ ‏) ﻋَﻦِ ﺍﻟﻨَّﺒِﻲِّ ‏( ﺻَﻠَّﻰ ﺍﻟﻠَّﻪُ ﻋَﻠَﻴْﻪِ ﻭَﺳَﻠَّﻢَ ‏) ﻗَﺎﻝَ : )) ﻣَﻦْ ﺃَﺗَﻰ ﻋَﺮَّﺍﻓًﺎ ﻓَﺴَﺄَﻟَﻪُ ﻋَﻦْ ﺷَﻲْﺀٍ ﻓَﺼَﺪَّﻗَﻪُ، ﻟَﻢْ ﺗُﻘْﺒَﻞْ ﻟَﻪُ ﺻَﻼﺓٌ ﺃَﺭْﺑَﻌِﻴﻦَ ﻳَﻮْﻣًﺎ ((
Amesimulia Muslim katika Swahiyh yake kutoka baadhi ya wake wa Nabiy ( ﺻﻠﻰ ﺍﻟﻠﻪ ﻋﻠﻴﻪ ﻭﺁﻟﻪ ﻭﺳﻠﻢ ) kwamba Nabiy ( ﺻﻠﻰ ﺍﻟﻠﻪ ﻋﻠﻴﻪ ﻭﺁﻟﻪ ﻭﺳﻠﻢ ) amesema: ((Atakayemwendea mtabiri akamuuliza kitu kisha akamuamini, haitokubaliwa Swalaah yake siku arubaini))
[Muslim]
ﻭَﻋَﻦْ ﺃَﺑِﻲ ﻫُﺮَﻳْﺮَﺓَ ‏( ﺭَﺿِﻲَ ﺍﻟﻠَّﻪُ ﻋَﻨْﻪُ ‏) ﻋَﻦِ ﺍﻟﻨَّﺒِﻲِّ ‏( ﺻَﻠَّﻰ ﺍﻟﻠَّﻪُ ﻋَﻠَﻴْﻪِ ﻭَﺳَﻠَّﻢَ ‏)
ﻗَﺎﻝَ : )) ﻣَﻦْ ﺃَﺗَﻰ ﻛَﺎﻫِﻨًﺎ، ﻓَﺼَﺪَّﻗَﻪُ ﺑِﻤَﺎ ﻳَﻘُﻮﻝُ ﻓَﻘَﺪْ ﻛَﻔَﺮَ ﺑِﻤَﺎ ﺃُﻧْﺰِﻝَ ﻋَﻠَﻰ ﻣُﺤَﻤَّﺪٍ ﺻَﻠَّﻰ ﺍﻟﻠَّﻪُ ﻋَﻠَﻴْﻪِ ﻭَﺳَﻠَّﻢَ (( ﺭَﻭَﺍﻩُ ﺃَﺑُﻮ ﺩَﺍﻭُﺩَ
Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah ( ﺭَﺿِﻲَ ﺍﻟﻠَّﻪُ ﻋَﻨْﻪُ ) kutoka kwa Nabiy ( ﺻﻠﻰ ﺍﻟﻠﻪ ﻋﻠﻴﻪ ﻭﺁﻟﻪ ﻭﺳﻠﻢ ) amesema:
((Atakayemkaribia kuhani na kuamini anayoyasema basi amekanusha aliyoteremshiwa Muhammad ﺻﻠﻰ ﺍﻟﻠﻪ ﻋﻠﻴﻪ ﻭﺁﻟﻪ ﻭﺳﻠﻢ )) [Abuu Daawuwd]
ﻭَﻟِﻸَﺭْﺑَﻌَﺔِ ﻭَﺍﻟْﺤَﺎﻛِﻢِ ﻭَﻗَﺎﻝَ : ﺻَﺤِﻴﺢٌ ﻋَﻠَﻰ ﺷَﺮْﻃِﻬِﻤَﺎ ﻋَﻦْ ﺃَﺑِﻲ ﻫُﺮَﻳْﺮَﺓَ : )) ﻣَﻦْ ﺃَﺗَﻰ ﻋَﺮَّﺍﻓًﺎ ﺃَﻭْ ﻛَﺎﻫِﻨًﺎ ﻓَﺼَﺪَّﻗَﻪُ ﺑِﻤَﺎ ﻳَﻘُﻮﻝُ ﻓَﻘَﺪْ
ﻛَﻔَﺮَ ﺑِﻤَﺎ ﺃُﻧْﺰِﻝَ ﻋَﻠَﻰ ﻣُﺤَﻤَّﺪٍ ﺻَﻠَّﻰ ﺍﻟﻠَّﻪُ ﻋَﻠَﻴْﻪِ ﻭَﺳَﻠَّﻢَ ((
Na wasimuliaji wengine wanne wa Hadiyth na Al-Haakim wamenakilii Hadiyth ya Abuu Hurayrah( ﺭﺿﻲ ﺍﻟﻠﻪ ﻋﻨﻪ) na wameikiri ni Swahiyh kwa mujibu wa masharti yao kwamba: ((Atakayemwendea m tabiri au kuhani akamwamini ayasemayo basi amekanusha aliyoteremshiwa Muhammad ﺻﻠﻰ ﺍﻟﻠﻪ ﻋﻠﻴﻪ ﻭﺁﻟﻪ ﻭﺳﻠﻢ ))
ﻭَﻷَﺑِﻲ ﻳَﻌَﻠَﻰ ﺑِﺴَﻨَﺪٍ ﺟَﻴِّﺪٍ ﻋَﻦِ ﺍﺑْﻦِ ﻣَﺴْﻌُﻮﺩٍ ﻣِﺜْﻠُﻪُ ﻣَﻮْﻗُﻮﻓًﺎ
Na Abuu Ya’laa ameripoti Hadiyth kama hiyo kutoka kwa Ibn Mas’uwd kwa isnaad nzuri lakini ni Hadiyth Mawquwf.
ﻭَﻋَﻦْ ﻋِﻤْﺮَﺍﻥَ ﺑْﻦِ ﺣُﺼَﻴﻦٍ ﻣَﺮْﻓُﻮﻋًﺎ : )) ﻟَﻴْﺲَ ﻣِﻨَّﺎ ﻣَﻦْ ﺗَﻄَﻴَّﺮَ ﺃَﻭْ ﺗُﻄُﻴِّﺮَ ﻟَﻪُ، ﺃَﻭْ ﺗَﻜَﻬَّﻦَ ﺃَﻭْ ﺗُﻜُﻬِّﻦَ ﻟَﻪُ، ﺃَﻭْ ﺳَﺤَﺮَ ﺃَﻭْ ﺳُﺤِﺮَ ﻟَﻪُ، ﻭَﻣَﻦْ ﺃَﺗَﻰ ﻛَﺎﻫِﻨًﺎ ﻓَﺼَﺪَّﻗَﻪُ ﺑِﻤَﺎ ﻳَﻘُﻮﻝُ، ﻓَﻘَﺪْ ﻛَﻔَﺮَ ﺑِﻤَﺎ ﺃُﻧْﺰِﻝَ ﻋَﻠَﻰ ﻣُﺤَﻤَّﺪٍ ﺻَﻠَّﻰ ﺍﻟﻠَّﻪُ ﻋَﻠَﻴْﻪِ ﻭَﺳَﻠَّﻢَ (( ﺭَﻭَﺍﻩُ ﺍﻟْﺒَﺰَّﺍﺭُ ﺑِﺈِﺳْﻨَﺎﺩٍ ﺟَﻴِّﺪٍ
Na Imepokelewa toka kwa ‘Imraan bin Huswayn Hadiyth Marfuw’: ((Si miongoni mwetu anayetafuta au anayebashiriwa Atw-Twiyaarah (mkosi, nuksi) au akafanya ukuhani au akafanyiwa ukuhani, au anayefanya uchawi au anayefanyiwa uchawi, na atakayemwendea kuhani
akamwamini ayasemayo basi amekanusha aliyoteremshiwa Muhammad ﺻﻠﻰ ﺍﻟﻠﻪ ﻋﻠﻴﻪ ﻭﺁﻟﻪ ﻭﺳﻠﻢ )) [Al-Bazaar kwa isnaad nzuri]
ﻭَﺭَﻭَﺍﻩُ ﺍﻟﻄَّﺒَﺮَﺍﻧِﻲُّ ﻓِﻲ ﺍﻟْﺄَﻭْﺳَﻂِ ﺑِﺈِﺳْﻨَﺎﺩٍ ﺣَﺴَﻦٍ ﻣِﻦْ ﺣَﺪِﻳﺚِ ﺍﺑْﻦِ ﻋَﺒَّﺎﺱٍ ﺩُﻭﻥَ ﻗَﻮْﻟِﻪِ : )) ﻭَﻣَﻦْ ﺃَﺗَﻰ (( .. ﺇِﻟَﻰ ﺁﺧِﺮِﻩِ
Hadiyth hiyo hiyo ameinakili Atw-Twabaraaniy katika Al-Awsatw kwa isnaad nzuri kutoka kwa Ibn ‘Abbaas bila ya kauli ya mwisho: ((Na atakayemwendea…))
ﻗَﺎﻝَ ﺍﻟْﺒَﻐَﻮِﻱُّ : ﺍﻟْﻌَﺮَّﺍﻑُ ﺍﻟَّﺬِﻱ ﻳَﺪَّﻋِﻲ ﻣَﻌْﺮِﻓَﺔَ ﺍﻷُﻣُﻮﺭِ ﺑِﻤُﻘَﺪِّﻣَﺎﺕٍ ﻳُﺴْﺘَﺪَﻝُّ ﺑِﻬَﺎ ﻋَﻠَﻰ ﺍﻟْﻤَﺴْﺮُﻭﻕِ ﻭَﻣَﻜَﺎﻥِ ﺍﻟﻀَّﺎﻟَّﺔِ ﻭَﻧَﺤْﻮِ ﺫَﻟِﻚَ
Al-Baghaawiy amesema: Al-‘Arraaf (mtabiri) ni ambaye anadai ujuzi wa mambo fulani kama vile yanayohusu vitu vilivyoibiwa, wapi vipo vitu hivyo, au mnyama aliyepotea na kama hayo kwa njia ya uchawi.
ﻭَﻗِﻴﻞَ ﻫُﻮَ ﺍﻟْﻜَﺎﻫِﻦُ، ﻭَﺍﻟْﻜَﺎﻫِﻦُ ﻫُﻮَ ﺍﻟَّﺬِﻱ ﻳُﺨْﺒِﺮُ ﻋَﻦِ ﺍﻟْﻤُﻐَﻴَّﺒَﺎﺕِ ﻓِﻲ ﺍﻟْﻤُﺴْﺘَﻘْﺒَﻞِ
Wengine wamesema yeye ndiye kuhani, na kuhani ni anayetoa khabari za mustaqbal (za mbele) zilizofichikana.
ﻭَﻗِﻴﻞَ ﺍﻟَّﺬِﻱ ﻳُﺨْﺒِﺮُ ﻋَﻤَّﺎ ﻓِﻲ ﺍﻟﻀَّﻤِﻴﺮِ
Na wengine wamesema ni ambaye anayetoa yaliyo katika dhamira ya mtu (siri moyoni).
ﻭَﻗَﺎﻝَ ﺃَﺑُﻮ ﺍﻟْﻌَﺒَّﺎﺱِ ﺍﺑْﻦُ ﺗَﻴْﻤِﻴَّﺔَ ﺍﻟْﻌَﺮَّﺍﻑُ ﺍﺳْﻢٌ ﻟِﻠْﻜَﺎﻫِﻦِ، ﻭَﺍﻟْﻤُﻨَﺠِّﻢِ ﻭَﺍﻟﺮَّﻣَّﺎﻝِ
ﻭَﻧَﺤْﻮِﻫِﻢْ ﻣِﻤَّﻦْ ﻳَﺘَﻜَﻠَّﻢُ ﻓِﻲ ﻣَﻌْﺮِﻓَﺔِ ﺍﻷُﻣُﻮﺭِ ﺑِﻬَﺬِﻩِ ﺍﻟﻄُّﺮُﻕِ
Na Abul-‘Abbaas, Ibn Taymiyyah kasema: Al-‘Arraaf ni jina la kuhani, na Al-Munajjim (mtabiri wa nyota) na Ar-Rammaal (mpiga ramli) na kama hao wanaojidai kuyajua mambo kwa njia hizo.
ﻭَﻗَﺎﻝَ ﺍﺑْﻦُ ﻋَﺒَّﺎﺱٍ ﻓِﻲ ﻗَﻮْﻡٍ ﻳَﻜْﺘُﺒُﻮﻥَ : ﺃَﺑَﺎ ﺟَﺎﺩٍ . ﻭَﻳَﻨْﻈُﺮُﻭﻥَ ﻓِﻲ ﺍﻟﻨُّﺠُﻮﻡِ ﻣَﺎ ﺃَﺭَﻯ ﻣَﻦْ ﻓَﻌَﻞَ ﺫَﻟِﻚَ ﻟَﻪُ ﻋِﻨْﺪَ ﺍﻟﻠَّﻪِ ﻣِﻦْ ﺧَﻼﻕٍ
Na Ibn ‘Abbaas akasema kuhusu watu wanaoandika ‘Abaa-Jaad’ (alfabeti kutumilia utabiri, uaguzi) na wanatazamia nyota kuamini athari zake ardhini. “Sioni kuwa wana fungu lolote mbele ya Allaah.”
.........NJOO UJIBU KAMA UNAJIWEZA KIELIMU SIO UNABAKI NA HOJA ZAKUBAMBANYA
 
Huyu ni tapeli kama matapeli wengine tu!!.
Maana ya unajimu ni elimu ya nyota. Unajimu ni elimu ambayo ni nzuri katika Uislamu na kwa ajili ya kuwa na elimu hiyo Waislamu waliweza kusafiri na majahazi na meli kuelekea sehemu nyingi baharini na kwa ajili hiyo Waislamu waliweza kueneza Uislamu na kufanya biashara bila ya matatizo yoyote.
Hata hivyo, wapo baadhi ya Waislamu na wasiokuwa Waislamu wanatumia nyota kutabiri mambo yatakayokufika au yatakayotokea. Kusoma elimu hiyo kwa sababu hiyo ni ushirikina na hivyo dhambi kubwa mbele ya Uislamu. Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ametuhimza sana tusiwe ni wenye kwenda kwa wapiga bao, ramli au kutizamia kwa kutumia nyota au mkono kwani mwenye kufanya hivyo atakuwa amekufuru kwa aliyokuja nayo Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom