KERO DSE na VERTEX Securities wanaua Soko la Hisa na Kudhulumu Wagonjwa – Mifumo Imekufa, Pesa Zinapotea!

KERO DSE na VERTEX Securities wanaua Soko la Hisa na Kudhulumu Wagonjwa – Mifumo Imekufa, Pesa Zinapotea!

  • Thread starter Thread starter Anonymous (c723)
  • Start date Start date
Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Wakuu, nipo kitandani nikiugua, lakini roho inaniuma kuona jinsi uwekezaji wangu unavyoliwa na 'mchwa' mchana kweupe. Mimi ni mwekezaji (CDS No: 811....), nimeuza hisa mara nne ili nipate pesa za matibabu, lakini Vertex International Securities wameamua kunizungusha na kunitapeli.

Jana baada ya kelele nyingi, walidanganya DSE kuwa watalipa deni langu la 83,000/+, lakini wakatuma 16,448/- tu! Huu ni uhujumu uchumi na unyama dhidi ya mgonjwa. Lakini tatizo ni kubwa zaidi; Mifumo ya DSE imekuwa ikifeli na kuanguka kila siku, jambo linalosababisha pesa za wawekezaji kupotea katika mazingira ya kutatanisha.

Uzembe huu wa DSE na brokers wao umesababisha wawekezaji kulikimbia soko. Matokeo yake sasa soko limevamiwa na 'Panic Selling' ambapo kila mwekezaji anauza hisa na hakuna wanunuzi, hali inayopelekea hisa za makampuni makubwa kuporomoka thamani. Je, DSE mnasubiri mwekezaji afe kwa kukosa dawa ndipo mfanye kazi? Je, mnasubiri soko life kabisa?

Nahitaji pesa yangu yote LEO, na madai yangu ya fidia yapo palepale kwa usumbufu huu wa kikatili.

Majina na mawasiliano yangu nimewapa mods wa JF
 
Masoko ya fedha na mitaji Kuna namna wanapaswa kijirekebisha padogo tu watapata support kubwa kutoka kwa wadau.
 
Pole sana kama uatakua hujapata msaada hadi sasa naomba tuwasiliane +255 625 748 339 (WhatsApp)
 
Yaani uuze hisa utapeliwe fedha……Mbona kama ndo nasikia kwako hii kitu. Nipo kwenye game kitambo na sijawahi sikia hii issue! Shida inakuja kuna baadhi ya hisa hapo nyuma zilifanya double trading so watu wakajiona wana hisa nyingi kuliko halali yao so ukiuza hisa zako broker akafanya reconcilliation ndipo unajulikana una hisa pungufu kuliko hisa zilizoonekana ubaoni. Nadhani shida kubwa ipo hapo!
 
Shida inakuja kuna baadhi ya hisa hapo nyuma zilifanya double trading so watu wakajiona wana hisa nyingi kuliko halali yao so ukiuza hisa zako broker akafanya reconcilliation ndipo unajulikana una hisa pungufu kuliko hisa zilizoonekana ubaoni. Nadhani shida kubwa ipo hapo
Huu si ndio wizI wenyewe
Kwanini zisome nyingi halafu ukitaka kuuza uambiwe ni chache
 
Back
Top Bottom