Mtu aitwae
#Manyerere Jackton ameandika mambo yasiyofanana na chembe ya ukweli kuhusu KM Dk. Slaa.
Bado tuko Ofisini. Kazi zinaendelea.
Hicho alichokiandika labda kama kinatokea kwenye ofisi ya chama kingine anachokijua Manyerere na kwa mtu mwingine tofauti na Dk. Slaa, Katibu Mkuu wa CHADEMA.
Nimuombe Jackton Manyerere, mpiganaji ambaye anapaswa kuwa na heshima yake kwenye tasnia ya habari afanye atimize wajibu wa kitaaluma katika kukusanya na kupasha habari badala ya uzushi na maneno haya yasiyo ya kweli.
Labda kama wameanza tena kufanya Kazi ile ile waliyokuwa mwaka 2010 ambako walimzushia Katibu Mkuu Dk. Slaa kila aina ya uzushi ambao Watanzania waliukataa.
Habari hizi za kuzusha na kutengeneza ndizo zilizotumika pia katika kampeni za mwaka 2005 ambapo hawa wanaozizusha leo mitandaoni walikuwa ndiyo timu ya utawala huu ulioshindwa. Wakimpamba mfalme kuwa amevaa nguo wakati yu mtupu. Kwa kila mapambo kuficha uvundo uliokuwa ndani ambao hatimaye leo unanuka (kushindwa) kila mahali.
Makene