Dr. W. Slaa anaondoka CHADEMA

Manyerere Jackton

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
2,438
Reaction score
4,461
Najua wapo watakaobeza na hata kutukana lakini napata ushujaa wa kuyasema haya. Dk. Slaa usiku huu anaingia makao makuu kukabidhi gari, kadi, walinzi na cheo. Anajitoa CHADEMA. Naomba uzi huu uachwe hapa hapa ili baadaye nihukumiwe kwa haki.

Chanzo: Mimi mwenyewe.

 
Huyo Ndiyo Mwanaume na siyo wale akina Mbowe, Tundu Lisu,Lowasa &Co.!

Ndiyo Slaa wewe ndiyo ulipikwa na ukapikia na Unasimama kwa kile unachokiamini na siyo kuyumbishwa na kununulika Fedha, Mungu akutangulie kwenye safari yako, mchango wako unajulikana, na hakuna takataka yoyote yule atakayeweza kulifuta Hilo!

.
.
.
Respect!

 
Haya tunasubiri kwa tuone
 
Na wewe umeanza kuwa muhuni au mabange umeanza kuvuta
 
Haya tunasubiri tuona ukweli wake na ushujaa wako bwana Jackson Manyerere
 
wewe umeshawah kuleta uzushi humu mara nyingi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…