Dr. Slaa naomba maoni yako ktk hili

Dr. Slaa naomba maoni yako ktk hili

Magezi

JF-Expert Member
Joined
Oct 26, 2008
Posts
3,359
Reaction score
704
Mh. Dk Slaa nimewahi kutoa mawazo yangu kupitia forum hii ya JF nikisema kwamba wilaya, vijiji na hata mikoa kwa ujumla wake ile ambayo madini kama vile dhahabu, almasi, tanzanite na mengine yanapatikana ktk maeneo hayo basi wilaya na vijiji hivi vipewe japo asilimia 10 ya mrahaba utokanao na raslimali hiyo kwani wakazi wa maeneo hayo lazima wafaidike na mali iliyo ktk maeneo yao.

Sasa nimesikia serikali ya CCM hawataki kabisa jambo hilo, najiuliza ni kwa nini?

Kwa mtazamo wako wewe unalionaje hili??
 
Mh. Dk Slaa nimewahi kutoa mawazo yangu kupitia forum hii ya JF nikisema kwamba wilaya, vijiji na hata mikoa kwa ujumla wake ile ambayo madini kama vile dhahabu, almasi, tanzanite na mengine yanapatikana ktk maeneo hayo basi wilaya na vijiji hivi vipewe japo asilimia 10 ya mrahaba utokanao na raslimali hiyo kwani wakazi wa maeneo hayo lazima wafaidike na mali iliyo ktk maeneo yao.

Sasa nimesikia serikali ya CCM hawataki kabisa jambo hilo, najiuliza ni kwa nini?

Kwa mtazamo wako wewe unalionaje hili??


Kwa mtazamo wangu hili unalouliza Mkuu Magezi naona limo kwenye sera ya CHADEMA ya Majimbo. Mule wameeleza jinsi rasilimali za Taifa zinavyoweza kugawanywa kwenye majimbo ambayo rasilimali hizo zinapatikana. Angalia kwenye tovuti ya CHADEMA kwa maelezo zaidi nina imani itakuwepo.


 
S.S Pahres umejibu vema lakini pia aende kule kwenye sredi ya Dr Slaa kujibu hoja mablimbali iliyoanzishwa na Lunyungu ndi atapata majibu kirahisi kuliko kuanzisha nyu sredi.
 
Hakuna uchaguzi CHADEMA kwa sababu Slaa Katumwa na Mungu
 
Katika kampeni za uchaguzi mwaka 1995, bwana mapesa John Momose Cheyo akinadi sera za chama chake alisema: sehemu zenye dhahabu zifanane na dhahabu, akimaanisha maeneo husika yapate malipo kutokana na dhahabu inayochimbwa katika maeneo yao. Hili alilizungumza kwa raslimali zote. Kwa bahati mbaya au kwa ufinyu wa kuelewa, watu walimpuuza. Sasa miaka 15 baadae, hoja hii inarudi tena. Nimesikia hadi bungeni wakitaka sehemu ya mrahaba ipelekwe halmashauri ya wilaya! Kwa maana nyingine tuko nyuma miaka 15.
Naunga mkono hoja, badala ya kuishia ngazi ya halmashauri, basi twende chini zaidi hadi kwenye serikali ya kijiji.
 
Back
Top Bottom