Dr Slaa na kisa cha mwana mpotevu

Dr Slaa na kisa cha mwana mpotevu

kidole007

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2012
Posts
3,094
Reaction score
1,877
amani iwe nanyi,

kwa wasio faham kisa cha mwana mpotevu kwa muda wenu mkasome luka 15:11-32

lengo la threed si kuzungumzia kisa cha mwana mpotevu

lengo ni kumzungumzia kaka wa mwana mpotevu ambae kwa maisha ya sasa nna kila sabab ya kumfananisha na dr slaa

siku mwana mpotevu alipo rudi nyumbani na kufanyiwa sherehe kaka mtu alikasirika na kukataa kuhudhuria sherehe

baba yao alipo muuliza akasema kuwa yeye alikuwepo nyumbani kwa miaka mingi lakini hajawah kufanyiwa sherehe.

tuje kwa slaa nmesikiliza hotuba ya slaa ya pale serena amelia lia sana amesema chadema ambayo ameijenga kwa DAMU leo wanasahau yote na kuchukua watu wasio na maadili na mambo mengine aliyo washutumu hasa Lowasa

slaa kma aliyo kaka wa mwana mpotevu roho ya ubinafsi, umimi imempofusha na kusahau kua siku zote alikua chadema na ufalme wa chadema ulikua wake

kma kaka wa mwana mpotevu alivyo susia kuingia kwenye karamu slaa ameona ni heri atumie mgongo wa kujitoa kwenye siasa za vyama kuliko kukaa karamu moja na lowasa

mwisho yoyote asiye kua nasi basi yuko kinyume nasi

slaa ni mbinafsi na mtu wa kujikweza

wanamabadiliko wote tumchukulie slaa kma ni adui wa mabadiliko
 
well said mkuu, afu nashauri tuache kumzungumzia tena huyu bwana, tumpuuze ndio njia pekee anayostahili
 
Biblia ina utajiri mkubwa sana wa mifano,na misemo watz wataifaidi san amuda huu.pengine wengine watageuza Novel ya kusoma sana.
 
Excellent! What a a good matching stories! Ama kweli wewe umejua kulengesha.

Kwa kifupi Dr Slaa jana ni kama alijivua nguo tu. Aliwa huzunisha (dissapoint) sana kuanzia Wana CHADEMA na mamillioni ya umma wa WaTanzania ulio mwaminia na kumpenda kwa mapenzi mema kabisa. Kauli zake na tuhuma zake zilikuwa all over the places na 'very reckless'. Kwani zimejuruhi hisia na imani (trust) za watu wa kada mbali mbali katika jamii ambao walikuwa washirika na mtaji wake wa kisiasa kwake ambao aliwataja ama kuakiwahusisha na mambo mbalimbali.

Kwa kifupi kama Dr Slaa alidhani ataipasua CHADEMA na UKAWA amekosea sana bali amepasua 'future' yake ya kisiasa na ya kijamii.Kwa hakika WaTanzania wanahitaji MABADILIKO kuliko wanavyo muhitaji Dr. Slaa wakati huu.
 
Back
Top Bottom