ZeMarcopolo
Platinum Member
- May 11, 2008
- 14,279
- 7,685
- Thread starter
-
- #61
Wewe na maccm mnatofauti gani na makaburu ilhali mnawatenga wachaga kana kwamba si raia halali wa nchi hii? Si nyie kila siku mnakesha hapa kuwatenga wachaga mkijidai nyie ndo watanzania kuliko wachaga?
Una ushahidi wa hiki unachoandika?
Lete post moja tu inayoonyesha mimi kufanya hiki unachonilaumu nami nitawajibika.
Kuuona tu mtu ambaye mnafata itikadi moja anafanya kitu amabacho si cha kiungwana au yumkini naweza kusema kulea tabia hiyo katika kundi au chama hata kama wewe hujafanya moja kwa moja ni kuonyesha kuunga mkono jambo hilo. Unaweza kutuambia hapa kuwa watu mithili ya faizafoxy, ritz, chamviga, au kiujumla lumumba buku 7 guys huwa huwaoni wakifanya kuwatenga na kueabagua wachaga? Hujawaona wakitukana dini specificaly katoliki hapa? Mbona hujawai hata kuwakemea hata siku moja? Hiyo ni kuonyesha kwa njia moja au nyingine unawaunga mkono. Sipendi unafiki kama ulishawakanya lete hiyo posti hapa ili nikuondoe katika listi ya makaburu.
Mbona slaa na mbowe wanambagua zito kwahiyo ni makaburu?
ZeMarcopolo, Inawezekana ID imevamiwa na 'zuzu' la mtaani, maana haingii akilini kuwa unaweza kuandika hoja dhaifu kiasi hiki, imajaa contradiction. Tuanze:Msingi wa hoja yako ni, 'Dr. Slaa kusema kuwa matendo ya serikali ya CCM ni sawa na mfumo wa apartheid wa makaburu wa Afrika ya Kusini.'Tunajua Apartheid - ni mfumo wa kibaguzi kati ya mwa mwanadamu mmoja na mwingine kutokana na vigezo anavyoweka yeye 'mgabuzi', mfano Makaburi wa Afrika ya Kusini waliwabagua watu wale wote ambao hawakuwa na rangi nyeupe - yaani wazungu. Hapa Wahindi na Weusi (Waafrika) waliwekwa daraja la chini, na hivyo hawakuwa na haki sawa na wazungu kwa sababu tu ya rangi zao. Iwe elimu, matibabu, usafiri, na hata kupiga kura, Makaburu wa Afrika ya Kusini waliwapora haki watu waliowaona ni daraja la chini. Chama cha Mapinduzi - kama kilivyokuwa TANU - kiliundwa kwa misingi ya kutombagua binadamu mwenzio kwa namna yoyote ile, na ndio zamani (kwa waliokula chumvi) tulikuwa tunaimba binadamu wote ni sawa. Na tukaenda mbele zaidi kwa kuitana NDUGU fulani. Hali ikoje sasa? Kwanza tuna waheshimiwa! (ubaguzi). Kama mtu si mheshimiwa anakuwa nani? Na ana haki sawa na Mheshimiwa? Jibu- hapana. Kwa sasa tuna mfumo ambao watu fulani wana haki ya kutibiwa India, Afrika ya Kusini na kwingineko ambako wanaona 'kunawafaa' kwa fesha ya umma, lakini wengine wanapiga miayo kwenye Zahati ambao hata Asprin hakuna!. (ubaguzi) Kwa sasa, kuna mfumo ambao watu fulani wakitaka kufanya medical check-up wanapanda ndege, lakini wakina mama wanajifungulia sakafuni! (Ubaguzi)Kwa sasa tuna mfumo amabo baadhi ya watoto wanapitiwa na vibasi asubuhi wanapelekwa shule za St. St ... wakati wengine watembea 4km kwenda shule ambayo ni mbavu za mbwa na wanakalia mawe, hapo hujaongelea walimu. (ubaguzi). Zamani mtoto wa mama ntilie alikuwa anasoma shule moja - darasa moja na mtoto wa rais. (pitia orodha kwenye shule mfano Weruweru, Pugu, Ilboru, Umbwe Secondary, n.k. utakuta majina ya watoto wa viongozi wa juu kabisa enzi hizo! Zamani kulikuwa na mfumo ambao vyombo vya dola villikuwa vinamlinda kila raia na mali yake - mwenye kipato cha juu au cha chini, lakini sasa vyombo vya dola (i.e. polisi) vimekuwa ni kero kwa walala hoi (Soweto)Mfumo wa sasa ambao umejaa kasoro unawanyima raia haki ya msingi ya kupiga kura (pitia Hansard za bunge). Kule Zanzibar Sheha anaamua nani ana haki ya kupiga kura na nani hana haki, na kwa kiasi kikubwa maamuzi yake yanaegemea kwenye itikadi za siasa. (ukaburu)Mtu anapofananisha mfumo wa sasa na Apartheid ni kwa sababu haki za msingi zinatolewa kwa kimatabaka. Mzee Mandela alilipinga matabaka, TANU ilipinga matabaka na hata CCM (ya Mwl Nyerere) kiliyapinga matabaka. Kule Mara kuna watu wako korokoroni kwa sababu tu ya matabaka ya kisiasa. Kimatendo, mfumo wa nchi hii kwa sasa umejaa ubaguzi. Kwanini wagonjwa walale chini sakafuni, wakati wengine wanapelekwa India?
Acha porojo. Lete ushahidi wa tuhuma ulizo leta juu yangu.
Wewe na maccm mnatofauti gani na makaburu ilhali mnawatenga wachaga kana kwamba si raia halali wa nchi hii? Si nyie kila siku mnakesha hapa kuwatenga wachaga mkijidai nyie ndo watanzania kuliko wachaga?
Nachosema kama unaona wanachofanya makaburu hapo ccm ni sawa na hujawahi kuwakemea wewe ni kaburu tu. Haya basi wakemee sasa hivi hao ndugu zako wanaogawa taifa ili kwa kukashifu makabila mengine kama kweli wewe shujaa nikutoe kwenye hilo kund la makaaburu! Kama huwezi wewe ni kaburu tu
Sasa km uongozi wa juu wa ccm wote ni waislamu huoni km ni ubeberu huo
Survival of the fittest. Slaa was not fit, he couldnt survive in CCM.
Je, unadhani ilikuwa ni sahihi kwa Mandela kutumia njia za "kigaidi" kuuondoa mfuko wa apartheid?
Je, unadhani ni sahihi kwa Slaa kutumia njia za kigaidi kuuondoa CCM madarakani?
Twende kwa hoja...
ZeMarcopolo,
Ni hivi, you are either with Mandela or against him.
Kwa maneno mengine ni ama unasimama na Mandela au unaungana na Makaburu. Dr Slaa kasema anasimama upande wa Mandela, je, wewe unasimama upande upi? simple?
Mkuu ni heri uconcentrate kwenye shghuli yako inayokupatia kipato,kama humu ni mojawapo ya shghuli za kukupatia kipato,basi samahani sana sitoweza kujadiliana na wewe.Mimi hapa silipwi mkuu.Kwahiyo kuongea na Rostam Aziz ndio kosa la Wangwe!!!
Mushi siku hizi sijui nini kimekukuta...
Mkuu ni heri uconcentrate kwenye shghuli yako inayokupatia kipato,kama humu ni mojawapo ya shghuli za kukupatia kipato,basi samahani sana sitoweza kujadiliana na wewe.Mimi hapa silipwi mkuu.
Kama wewe uko kazini endelea tu,wengine purpose ya kujiunga humu ni ile ile,na ndiyo maana tuna mawazo huru.Wewe umekaririshwa na pengine ni kwasababu upo kazini.Samahani sitoweza kujadiliana na watu dizaini hiyo ya kwako.Mkuu Mushi,
Naona kuporomoka kwa Chadema na kubainika kwa ulaghai wake kumekuchanganya kabisa.
Pole sana. Ndio siasa zilivyo, kuna kupanda na kushuka.
Hujajibu swali.
Slaa hahasimama upande wa Mandela. Angekuwa upande wa Mandela asingefananisha maisha ya watanzania na hali aliyokabiliana na Mandela.
Slaa anapewa ruzuku na serikali ili afanye siasa, lakini anajifananisha na mtu aliyefungwa miaka 27 ili asifanye siasa.
Jibu swali twende kwa hoja...
Naunga mkono hoja,Slaa yuko desparate kwa kias kikubwa sana,
Na sisi watanzania sometimes tunakuwa mazuzu sana.
Mimi naomba niulize swali moja,
Hivi kama Dr.W.Slaa ameshindwa kuwa mtiifu kwenye kazi ya mungu na kutenda haki huko,na kufikia hatua hadi kuasi na kudondokea kwenye maisha ya kidunia yaliyojaa kila aina ya udandanyifu,
Ataweza vipi kutenda haki na usawa kwenye ufalme huu wa wanadamu?
Hata hili hatulion??
Slaa anayo mengi ya kutubia kabla hajaja hadharani na kuonesha boriti kwenye macho ya wenzake
Naona unatumia nguvu kubwa sana kuungaunga story lakini argument ya Dr Slaa iko very clear. Kwamba mfumo tulio nao sasa una elements za apartheid, unabagua watu kwenye haki za msingi. wengine wanakufa kwa kukosa dawa wakati wengine wanapelekwa india kwa matibabu.
Kumuunga mkono Mandela ni pamoja na kukubali kile alichokuwa anapigania - haki sawa.
Hoja yako ya pili kwamba Dr Slaa anapewa ruzuku na serikali ili afanye siasa lakini anajifananisha na Mandela, haina mashiko. Labda ufafanue siasa ni nini, siasa inafanywaje, na ni mambo yepi ni siasa au la? na je kujilinganisha na mtu ni kinyume na kufanya siasa?
Naunga mkono hoja,Slaa yuko desparate kwa kias kikubwa sana,
Na sisi watanzania sometimes tunakuwa mazuzu sana.
Mimi naomba niulize swali moja,
Hivi kama Dr.W.Slaa ameshindwa kuwa mtiifu kwenye kazi ya mungu na kutenda haki huko,na kufikia hatua hadi kuasi na kudondokea kwenye maisha ya kidunia yaliyojaa kila aina ya udandanyifu,
Ataweza vipi kutenda haki na usawa kwenye ufalme huu wa wanadamu?
Hata hili hatulion??
Slaa anayo mengi ya kutubia kabla hajaja hadharani na kuonesha boriti kwenye macho ya wenzake