Aliyekuwa mgombea ubunge wa CDM jimbo la Igunga Joseph Kashindye amesema baada ya matokeo kutangazwa na kumpa ushindi batili mgombea wa CCM hakujua hatima yake itakuwaje.
Hata hivyo amesema Dr Slaa alimtaka kukata rufaa mara moja mahakamani kupinga ushindi wa CCM.Kashindye ameendelea kusema kuwa alisita kutokana na kwamba hakuwa na fedha.Baada ya kumueleza katibu mkuu huyo hana fedha haraharaka Dr Slaa alimjibu maneno yafuatayo'' Wewe nenda kafungue kesi kwani hiyo kesi si yako bali ni ya wananchi wa Igunga,wao ndiyo watakaoisimamia wenyewe''
Kashindye amedai baada ya maneno hayo mazito kutoka kwa mtu anayependwa na watanzania alienda kufungua kesi,na baada ya kufungua wananchi wa Igunga wameisimamia kesi yao wenyewe,wamemlisha na kumpa malazi akifuatilia kesi mjini Tabora muda wote wa kesi na kubwa zaidi wamemchangia fedha taslim sh milioni 6 hatimaye ushindi ukapatikana.
Hata hivyo amesema Dr Slaa alimtaka kukata rufaa mara moja mahakamani kupinga ushindi wa CCM.Kashindye ameendelea kusema kuwa alisita kutokana na kwamba hakuwa na fedha.Baada ya kumueleza katibu mkuu huyo hana fedha haraharaka Dr Slaa alimjibu maneno yafuatayo'' Wewe nenda kafungue kesi kwani hiyo kesi si yako bali ni ya wananchi wa Igunga,wao ndiyo watakaoisimamia wenyewe''
Kashindye amedai baada ya maneno hayo mazito kutoka kwa mtu anayependwa na watanzania alienda kufungua kesi,na baada ya kufungua wananchi wa Igunga wameisimamia kesi yao wenyewe,wamemlisha na kumpa malazi akifuatilia kesi mjini Tabora muda wote wa kesi na kubwa zaidi wamemchangia fedha taslim sh milioni 6 hatimaye ushindi ukapatikana.