Hivi karibuni kumezuka maneno mengi,hasa baada ya Mufti kuwaasa waislam wasijiunge na maandamano ya kisiasa.Dr.Slaa akimjibu mufti kwa kuwa chadema ndio inayohusika na maandamano alisema Mufti hakufanya utafiti.Mi nikajiuliza mbona kuna mambo mengi tu mufti hakusema na kama angeyasema na kuonesha ushahidi sijui Dr.Slaa angejibu nini? Mfano hadi sasa inaonekana Dr.Slaa alikurupuka kuchukua mwanamke ambaye anamwenyewe, na katika sheria za kanisa ndoa ikishafungwa basi hiyo haivunjiki.Kwa hilo Dr.hakufanya utafiti wa kina.Siku za karibuni pia Dr.Slaa alimzushia kifo Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mh.Yohana Balele,pia hapa hakufanya utafiti.Kwa kweli kwa msomi wa kiwango cha Dr.Slaa hii ni aibu.Ombi langu kwa Dr.Slaa badala ya kulalamika ni aende kumuona Mufti wazungumze ana kwa ana badala ya kujibizana kwenye vyombo vya habari.