Dr. Shein kumuwakilisha Rais Magufuli katika ziara nchini Comoro

Taso

JF-Expert Member
Jun 12, 2010
2,503
2,378
cebee3e1-fcd6-401c-9f21-7fe62de6cb29.jpe


Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Mjumbe wa Baraza la Mawaziri ametumwa kumuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika ziara nchini Comoro.

Ikumbukwe Mambo ya nje, Mahusiano ya Kimataifa na Kikanda ni suala la Muungano. Rais wa Serikali ya Mapinduzi anatakiwa kugusa masuala ya Zanzibar tu, hagusi ya Muungano wala ya Tanganyika, kama ambavyo Magufuli hagusi masuala ya Zanzibar.

Iweje Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiuke kiapo chake cha kulinda Katiba ya nchi kwa kukasimu madaraka yake kwa mtu asiye na mamlaka ya kupewa majukumu hayo?
===========

Sahihisho. Dk Shein hakutumwa kumuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika ziara nchini Comoro.
Dk.Shein amekwenda Comoro kuiwakilisha Tanzania katika sherehe za kumuapisha Rais wa visiwa hivyo, ambavyo vina uhusiano mkubwa, wa karibu na wa asili na Zanzibar.

Sherehe hizo zinafanyika wakati huu na mara tu baada ya sherehe atarudi Zanzibar mchana huu!
 
hii ndo Tanzania bwana
kila rais anafanya kile anacho jisikia kufanya
kwa katiba ni mdudu fan?
ingekuwa inafatwa ujinga unaofanywa na manyangau wa CCM yasinge kuwepi
viva MAGU viva CCM
 
cebee3e1-fcd6-401c-9f21-7fe62de6cb29.jpe


Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Mjumbe wa Baraza la Mawaziri ametumwa kumuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika ziara nchini Comoro.

Ikumbukwe Mambo ya nje, Mahusiano ya Kimataifa na Kikanda ni suala la Muungano. Rais wa Serikali ya Mapinduzi anatakiwa kugusa masuala ya Zanzibar tu, hagusi ya Muungano wala ya Tanganyika, kama ambavyo Magufuli hagusi masuala ya Zanzibar.

Iweje Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiuke kiapo chake cha kulinda Katiba ya nchi kwa kukasimu madaraka yake kwa mtu asiye na mamlaka ya kupewa majukumu hayo?
Ule ujumbe katika baraza la mawaziri lililozungumziwa na katiba kwa Rais wa SMZ ni Jamhuri ya Muungano au ni wa Zanzibar?
 
Katiba na sheria vimewekwa kwa ajili ya kuwaminya masikini huku mbele ya vigogo vimegeuzwa kama nyoka au mbwa asiye na menu huku wakivitumia kama kinga na daraja la kujifanikisha katika mambo yao.
 
Tanganyika kwa sasa ni Mkoloni wa Zanzibar hivyo si lazima Magufuli afuate mkataba wowote wa muungano hasa ukizingatia kuwa Dr Shein kasimikwa ikulu ya Zanzibar kwa Nguvu za Tanganyika kupitia uchaguzi Haramu, hivyo atamtuma popote Duniani akijisikia.
 
Sasa ulitaka akuteue wewe kumuwakilisha ndiyo aonekane hajavunja katiba, hili jambo halina athari zozote tuache kuokoteza vijisababu, hakuna nafsi iliyokamilika.
 
Kwa hali ilivyo labda Shein anaweza kuteuliwa na JPM kuwa Mkuu wa Mkoa wa Darisalama. Lakini tuache utani jamani, hii inatisha!
 
Tusiwe watumwa saaanaaa, wa katiba, look at the act itself, is it good for the union or bad.
 
cebee3e1-fcd6-401c-9f21-7fe62de6cb29.jpe


Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Mjumbe wa Baraza la Mawaziri ametumwa kumuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika ziara nchini Comoro.

Ikumbukwe Mambo ya nje, Mahusiano ya Kimataifa na Kikanda ni suala la Muungano. Rais wa Serikali ya Mapinduzi anatakiwa kugusa masuala ya Zanzibar tu, hagusi ya Muungano wala ya Tanganyika, kama ambavyo Magufuli hagusi masuala ya Zanzibar.

Iweje Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiuke kiapo chake cha kulinda Katiba ya nchi kwa kukasimu madaraka yake kwa mtu asiye na mamlaka ya kupewa majukumu hayo?
Sio mara ya kwanza kuvunjwa katiba
 
Hiyo ziara inahusu nini? Kirafiki au uwekezaji Zanzibar? Vipi kama mambo yanahusiana na hiyo ziara yanaihusu Zanzibar, Magufuli kuhudhuria angekua kavunja katiba pia.
 
Nadhani ametumwa kama mjumbe wa baraza la mawaziri wa muungano, si mnakumbuka aliapa majuzi kati kuwa mjumbe wa baraza la mawaziri. No way kimuungano chetu ni shida kukitafsiri, mambo yanaenda tu hata Jecha anaweza tumwa na Makonda kuchunguza wafanyakazi hewa kwa DSM.
 
cebee3e1-fcd6-401c-9f21-7fe62de6cb29.jpe


Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Mjumbe wa Baraza la Mawaziri ametumwa kumuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika ziara nchini Comoro.

Ikumbukwe Mambo ya nje, Mahusiano ya Kimataifa na Kikanda ni suala la Muungano. Rais wa Serikali ya Mapinduzi anatakiwa kugusa masuala ya Zanzibar tu, hagusi ya Muungano wala ya Tanganyika, kama ambavyo Magufuli hagusi masuala ya Zanzibar.

Iweje Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiuke kiapo chake cha kulinda Katiba ya nchi kwa kukasimu madaraka yake kwa mtu asiye na mamlaka ya kupewa majukumu hayo?
Kumbe mnafahamu kuwa Magufuli hatakiwi kuingilia masuala ya Zanzibar!!!

Sasa kwa nini mlikuwa bize kutapika na kumtaka Magufuli aingilie uchaguzi Wa Zanzibar??

CHADEMA bwana.
 
Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Mjumbe wa Baraza la Mawaziri ametumwa kumuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika ziara nchini Comoro.

Ikumbukwe Mambo ya nje, Mahusiano ya Kimataifa na Kikanda ni suala la Muungano.
Mwenyewe umekiri kwamba:-
- Rais wa SMZ ni mjumbe wa Baraza la Mawaziri la JMT.
- Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa ni suala la Muungano.

Kutokana na maneno yako mwenyewe tafsiri yake inakuja hivi:-
  • Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri ni Rais wa JMT
  • Rais wa JMT anao uwezo wa kumtuma mjumbe kufanya jambo lolote kwa niaba yake.
  • Huyo mjumbe wa Baraza la Mawaziri la JMT amekwenda Comoro kumuwakilisha Rais wa JMT kwenye jambo linalohusu mambo ya muungano.
  • Rais Shein ametumia ndege ya serikali ya JMT kwenda huko Comoro na kwa gharama zote za JMT
  • Akiwa huko Comoro, Rais Shein (akiwa ni Mjumbe wa Baraza la Mawaziri) anatumia Bendera ya JMT, na kama utahitajika kupigwa wimbo wa taifa basi unaopigwa ni ule wa JMT.
  • Kila kitu anachokifanya akiwa huko kina sura ya JMT.
Pengine labda ungeweka Ibara ya Katiba ya JMT iliyokiukwa kwa kitendo cha Rais wa JMT kumtuma Nje ya Nchi Mjumbe huyu wa Baraza la Mawaziri la JMT aliyekula kiapo miezi michache iliyopita kule Dodoma, mjadala ungependeza zaidi. Mimi binafsi sijaona tatizo.
 
Unajua kwamba rais wa Zanzibar ni mjumbe wa Baraza la Mawaziri wa JMT? Mbona hilo hauhoji?
 
cebee3e1-fcd6-401c-9f21-7fe62de6cb29.jpe


Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Mjumbe wa Baraza la Mawaziri ametumwa kumuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika ziara nchini Comoro.

Ikumbukwe Mambo ya nje, Mahusiano ya Kimataifa na Kikanda ni suala la Muungano. Rais wa Serikali ya Mapinduzi anatakiwa kugusa masuala ya Zanzibar tu, hagusi ya Muungano wala ya Tanganyika, kama ambavyo Magufuli hagusi masuala ya Zanzibar.

Iweje Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiuke kiapo chake cha kulinda Katiba ya nchi kwa kukasimu madaraka yake kwa mtu asiye na mamlaka ya kupewa majukumu hayo?
Dr Shein kama Rais wa Zanzibar ni mmoja wa Baraza la Mawaziri.
 
Back
Top Bottom