Binafsi nimesononeshwa na maelezo ya aliyekuwa waziri wa Mifugo David Matthayo ya kuwa ameonewa kutakiwa kujiuzulu. Ni kweli David Mathayo hahusiki moja kwa moja na makosa ya opareshini tokomeza kwasababu angefanya nini kilichotokea kisitokee kwa bajeti ndogo aliyotengewa.
Lakini, Mathayo asilaumu hata kidogo kwakuwa hata yeye hakuwa na mpango kazi unaolingana na bajeti aliyotengewa. Angekuwa mimi ningeleta effect japo kwenye mkoa mmoja tu kwa kutumia hela ndogo aliyokuwa nayo kwenye wizara. Randomly angechagua kanda, mkoa, wilaya au hata kata ambayo angefanya kitu kinachohitajika kwa ufugaji wa kisasa kabisa, ili watu waone na kuilaumu hazina kwa kumtengea hela isiyotosha kuihudumia nchi nzima kama alivyofanya kwenye kanda, mkoa, wilaya au kata ile. Badala yake vilio vya wafugaji vimetawanyika nchi nzima huku Mathayo akidai kapewa hela kidogo, huu ni udhaifu katika planing. Katika mifugo hakuna kanda, mkoa, wilaya wala kata isiyokuwa na malalamiko. Ona Magufuli alivyoona hakupewa hela ya kutosha wakati alipokuwa Wizara na Mifungo na Uvuvi aliamua kuleta effect kwenye uvuvi kwa kukamata wavuvi haramu kwa nguvu zake zote hadi akakamata hadi wachina waliokuwa wanavua isivyo halali (samaki wa magufuli, Je, ranchi, marambo, majosho, masoko, maduka ya nyama ya kisasa, ngozi za wanyama safi za David Mathayo ziko wapi?). Hili ni tatizo kwenye wizara nyingi nchini, Kama unapewa hela kidogo isiyokidhi mahitaji ya nchi nzima, bila upendeleo na kwa njia za wazi zinazowashirikisha wadau mbalimbali amua kuchagua eneo dogo la kufanyia kazi kwa mzuunguuko ili upate matokeo makubwa, ili ukipata hela nyingine uhamie eneo lingine la kazi. Hata huko Marekani majimbo yote hayalingani kwa maendeleo ya kitu kimoja. Kunatakiwa kuwe na coordination ya wizara zote, mfano, kama mkoa mmoja utaendelezwa kwenye shule, mwingine unaendelezwa kwenye mifugo, kama mkoa mmoja umeendelezwa kwenye huduma ya maji mwingine unaendelezwa kwenye huduma ya umeme, kilimo, mawasiliano, n.k hadi mzuunguko wa utoaji huduma unaenea kwa mikoa yote. Hata kwenye familia ukiwa na hela kidogo lazima uchague eneo la kuhudumia na kuleta effect, watoto wamekosa nguo za sikukuu lakini wamekula pilau na nyama ya kuku na soda hadi wakasaza hawatanung'unika sana kuliko ukawanunulia watoto mmoja malapa, mwingine shati tu, mwingine, kaptula tu bila shati na wa mwisho hijabu tu.