Possibles
JF-Expert Member
- Sep 22, 2011
- 1,942
- 2,469
Ndugu yangu nakumbuka alimkunja daktarii hapo kwa maana mtoto wake alikaa siku 2 bila huduma zaidi ya kupewa dawa za kushusha homa tu.Ilipofika siku ya pili dogo akalegea kabisa, baba mtu(ambaye ndio ndugu yangu) akaenda kumsihi daktari amuangalie mtoto wake maana anakatisha tamaa.Daktari akamwambia asubiri mpaka muda wa kuzungukia wagonjwa ufike. Jamaa akasubiri.
Baada ya muda mfupi dogo akakata kauli, mama yake akaanza kulia huko wodini. Baba mtu akamuomba daktari kama amebanwa basi ampe rufaa mtoto ili apelekwe Muhimbili.Daktari akakataa kwamba hata rufaa ataitoa atakapofanya ziara wodini.
Hapo ndipo baba mtoto uvumilivu ukamshinda akamkunja daktari. Daktari akapiga kelele kuita mlinzi naye akapigwa. Mlinzi akaita wenzake wawili kutoka getini huko ikawa mshikemshike wakamkamata wakampeleka kwa mganga mkuu.
Mganga mkuu akamsikiliza akakimbia kumuona mtoto, akaamuru apelekwe Muhimbili na baba mtoto apelekwe polisi kwa kuleta vurugu. Mama mtoto akapewa ambulance mpaka Muhimbili mtoto akatibiwa akapona baada ya siku chache. Wengine tukaenda kuyamaliza na utawala huko Oysterbay police.
Cha kushangaza hakutokea daktari wala yeyote pale polisi mpaka polisi wakamruhusu baba mtoto ajiondokee zake.
Si njia nzuri kushinikiza madaktari kwa njia hiyo lakini ni muhimu tujue kuwa hata miongoni mwa madaktari wako pia ambao hawana utu na ukiwaogopa hawa wanakupotezea maisha.
Nawapongeza madaktari wazuri wanaojali uhai wa wagonjwa wao na wenye kuvumilia ugumu wa kazi zao.
Baada ya muda mfupi dogo akakata kauli, mama yake akaanza kulia huko wodini. Baba mtu akamuomba daktari kama amebanwa basi ampe rufaa mtoto ili apelekwe Muhimbili.Daktari akakataa kwamba hata rufaa ataitoa atakapofanya ziara wodini.
Hapo ndipo baba mtoto uvumilivu ukamshinda akamkunja daktari. Daktari akapiga kelele kuita mlinzi naye akapigwa. Mlinzi akaita wenzake wawili kutoka getini huko ikawa mshikemshike wakamkamata wakampeleka kwa mganga mkuu.
Mganga mkuu akamsikiliza akakimbia kumuona mtoto, akaamuru apelekwe Muhimbili na baba mtoto apelekwe polisi kwa kuleta vurugu. Mama mtoto akapewa ambulance mpaka Muhimbili mtoto akatibiwa akapona baada ya siku chache. Wengine tukaenda kuyamaliza na utawala huko Oysterbay police.
Cha kushangaza hakutokea daktari wala yeyote pale polisi mpaka polisi wakamruhusu baba mtoto ajiondokee zake.
Si njia nzuri kushinikiza madaktari kwa njia hiyo lakini ni muhimu tujue kuwa hata miongoni mwa madaktari wako pia ambao hawana utu na ukiwaogopa hawa wanakupotezea maisha.
Nawapongeza madaktari wazuri wanaojali uhai wa wagonjwa wao na wenye kuvumilia ugumu wa kazi zao.