Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,359
- 4,814
Rais wa Marekani Donald J Trump, ameliagiza shirika la fedha la nchi hiyo kutoa bima kwa bei nafuu kwa biashara zote za baharini, hasa mafuta yanayopitia mlango Bahari wa Hormuz unaomilikiwa na Iran huku akidai kuwa Marekani itahakikisha mafuta yanafika Duniani kote bila vikwazo.
Trump ameandika:" Kuanzia sasa, nimeagiza Shirika la Fedha la Maendeleo la Marekani (DFC) kutoa kwa bei nafuu sana, bima ya hatari ya kisiasa na dhamana kwa Usalama wa Kifedha kwa Biashara zote za Baharini, hasa Nishati, inayosafiri kupitia Ghuba.
Nafuu hii itapatikana kwa Meli zote za Usafirishaji wa mafuta, na endapo itahitajika, Jeshi la Wanamaji la Marekani litaanza kusindikiza meli za mafuta kupitia Mlango Bahari wa Hormuz, haraka iwezekanavyo.
Haijalishi chochote, Marekani itahakikisha Mtiririko mzuri wa nishati Duniani. NGUVU YA KIUCHUMI na KIJESHI ya Marekani ndiyo KUBWA ZAIDI DUNIANI" amesisitiza Rais wa Marekani DONALD J. TRUMP